Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Maftaha Abdallah Nachuma

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mtwara Mjini

Primary Question

MHE. MAFTAHA A. NACHUMA aliuliza:- Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa Mwanza alipiga marufuku na kuziagiza mamlaka zinazohusika kuacha kuwasumbua wafanyabiashara wadogo wadogo maarufu kama Wamachinga:- Je, Serikali inatekeleza agizo hilo kwa kiwango gani?

Supplementary Question 1

MHE. MAFTAHA A. NACHUMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba niulize maswali mawili madogo ya nyongeza. Nimesikitishwa sana na maelezo ya Mheshimiwa Naibu Waziri pale alivyoeleza kwamba Manispaa ya Mtwara Mikindani imetenga maeneo kama vile Likonde, Mbae na Mjimwema.
Mheshimiwa Naibu Spika, ikumbukwe maeneo haya ni Tarafa mbili tofauti; na siku ya tarehe 21 mwezi wa Nane, Serikali iliweza kubomoa vibanda vidogo vidogo ambavyo vimejengwa katika Kata ya Jangwani, Tarafa ya Mikindani ambapo ni kilometa takribani 10 kwa maeneo aliyoyataja ambapo kuna akinamama wafanyabiashara wadogo wadogo wanauza samaki kihalali kabisa katika maeneo yale. Cha ajabu wale samaki wao wamevunjwavunjwa na kumwagwa. Akinamama wale walikopa pesa kutoka katika mabenki na taasisi mbalimbali za kifedha na mpaka hivi sasa ninavyozungumza hawana uwezo wa kulipa mikopo ambayo wamekopa.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu ni kwamba, Mheshimiwa Naibu Waziri yuko tayari hivi sasa afuatane na Mbunge wa Jimbo la Mtwara Mjini ambaye anazungumza, aje kuangalia mazingira yale ambayo wale akinamama wamebomolewa maeneo yao ya kuuza samaki ambapo ni mbali takriban kilometa 10 kutoka eneo ambalo amelitaja yeye?
Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

himiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Maftaha yuko pale site; na hapa nimesema majibu ya msingi ya Serikali ni kwamba lazima Halmashauri zitenge maeneo. Hata hivyo, tumezielekeza Halmashauri kwamba, maeneo watakayotenga lazima waangalie kile kitu kinaitwa accessibility, yaani ni jinsi gani yatafikika? Ndiyo maana Halmashauri mbalimbali tumezielekeza kwamba ziwasiliane na SUMATRA katika maeneo hayo kwamba kuwe na uwezekano hata wa daladala ziweze kufika kwa sababu maeneo mengine unakuta watu wanashindwa kwenda kwa sababu daladala hakuna.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naomba nimhakikishie kwamba, jana nilipokuwa nikijibu hapa maswali mbalimbali nikasema Mkoa wa Mtwara ni mkoa wangu wa kipaumbele, ni mkoa wa kwanza. Naomba niseme kwamba nimekubali ombi lake, tutakwenda site, lengo kubwa ni kuwasaidia hawa Watanzania wadogo wanaotaka kujikomboa katika suala la uchumi. Kwa hiyo, hilo, aondoe shaka ndugu yangu, mimi nitafika site, tutakwenda pamoja katika hilo.

Name

Stanslaus Shing'oma Mabula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyamagana

Primary Question

MHE. MAFTAHA A. NACHUMA aliuliza:- Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa Mwanza alipiga marufuku na kuziagiza mamlaka zinazohusika kuacha kuwasumbua wafanyabiashara wadogo wadogo maarufu kama Wamachinga:- Je, Serikali inatekeleza agizo hilo kwa kiwango gani?

Supplementary Question 2

MHE. STANSLAUS S. MABULA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Nami naomba niulize swali dogo la nyongeza. Kutokana na sababu ya msingi kwamba tatizo la Machinga, yaani wafanyabiashara ndogo ndogo pengine linaweza kuwa endelevu, hasa kwenye Halmashauri zenye miji mikubwa ikiwemo Halmashauri ya Jiji la Mwanza ambayo ipo Jimbo la Nyamagana, napenda tu kuiuliza Serikali kwamba, pamoja na utaratibu huu mzuri ambao inaelekeza, Halmashauri zetu zimekuwa na changamoto kubwa ya kifedha. Je, Serikali sasa iko tayari kupitia Wizara ya TAMISEMI kuzisaidia Halmashauri kwa namna moja au nyingine kuweza kuboresha maeneo haya na yawe rafiki kwa hawa wafanyabiashara?
Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mabula kwamba siku zote Ofisi ya Rais, (TAMISEMI) iko tayari. Ndiyo maana katika nyakati tofauti tumekuwa tukitoa maelekezo mbalimbali, lakini siyo maelekezo ya maneno peke yake, mpaka ya kiutaalam. Ndiyo maana kuna Halmashauri mbalimbali hivi sasa, wengine wapo katika suala zima la uwekezaji kupitia asasi mbalimbali lakini wanaleta madokezo mbalimbali na miradi yao pale Ofisi ya Rais, (TAMISEMI), lengo ni kwamba tunayapima, yale ambayo yanaonekana kabisa kama jambo hili litasaidia Halmashauri lakini bila kukwaza Halmashauri hiyo kutokuingia katika mgogoro, tumekuwa tukizisaidia Halmashauri hizo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Stanslaus kwamba ofisi yetu sisi itashirikiana na Halmashauri zote. Tunajua kwamba zikipata uchumi wa kutosha zitaweza kujiendesha, zitapata own source ya kutosha, akinamama na vijana watapata mikopo, uchumi utabadilika. Kwa hiyo, sisi tupo tayari muda wote kuhakikisha Halmashauri zinafanya kazi zake vizuri.

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Naibu Waziri, Mheshimiwa Jafo, nataka niongezee kwenye swali lililoulizwa na Mheshimiwa Mabula kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli Serikali inatambua ukuaji wa miji hii mikubwa na ongezeko la watu wengi wanaokimbilia mijini kwa ajili ya kutafuta riziki, ikiwemo na shughuli hizi zinazofanywa na wafanyabiashara wadogo wadogo. Hata hivyo, Serikali ina programu inayoendelea sasa ya miji mikubwa ya kimkakati ikiwemo na Mwanza ambapo tunatumia kiasi cha karibu shilingi bilioni 350 kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika kupanga vipaumbele hivyo, Halmashauri walihusishwa na walibainisha maeneo kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu hiyo. Namwomba tu Mheshimiwa Mbunge kwamba wajitahidi sana katika kuhakikisha kwamba watakapowapangia wafanyabiashara wadogo maeneo ya kufanyia biashara, basi wahakikishe kwamba mabasi madogo madogo yanayoweza kupeleka watu yanaweza kufika katika maeneo hayo. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo, ni kweli kwamba wamachinga au wafanyabiashara wadogo wadogo ni muhimu sana katika uchumi wa nchi yetu kwa sababu ni wengi na wanafanya shughuli ambazo zinasaidia uchumi wetu. Hata hivyo, niwasihi na niwaombe wajitahidi kufanya biashara katika maeneo yaliyopangwa. Kufanya biashara kwenye kila eneo ikiwemo barabarani na kuziba barabara ili watumiaji wengine wasitumie barabara, inaathiri shughuli nyingine za kiuchumi na kwa hiyo faida yao inakuwa haionekani kwa sababu inazuia shughuli nyingine za watu wengine.
Mheshimiwa Naibu Spika, busara hii wakiwa nayo, pia busara hiyo hiyo ya wajibu wa Serikali kwa maana ya Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya kwa kushirikiana na Halmashauri zao kuwapangia maeneo mbadala yanayofikika na yanayofaa kwa biashara zao, jukumu hilo ni muhimu sana kufanywa na Serikali za maeneo hayo.

Name

Joseph Osmund Mbilinyi

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Mbeya Mjini

Primary Question

MHE. MAFTAHA A. NACHUMA aliuliza:- Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa Mwanza alipiga marufuku na kuziagiza mamlaka zinazohusika kuacha kuwasumbua wafanyabiashara wadogo wadogo maarufu kama Wamachinga:- Je, Serikali inatekeleza agizo hilo kwa kiwango gani?

Supplementary Question 3

MHE. JOSEPH O. MBILINYI: nakushukuru sana dada yangu Mheshimiwa Naibu Spika na Mbunge wa Viti Maalum Kinondoni. (Kicheko)
Mheshimiwa Naibu Spika, suala la Wamachinga siyo eneo, ni mazingira ya biashara. Nimekuwa nalisema hili mara zote. Ndiyo maana tulikuwa wakati ule tukisafiri kwenda China, Beijing, mimi kazi ya kwanza naangalia mazingira ya Wamachinga, wapo hawapo? Unakuta wapo. Ukienda New York unaangalia Wamachinga; wapo? Unakuta wapo. Kinachotakiwa ni mazingira ya kibiashara.
Mheshimiwa Waziri, naomba ukae kidogo. Kwa ajili ya kuweka kumbukumbu sawasawa, mimi ni Mbunge wa kuteuliwa na Mheshimiwa Rais, sio Mbunge wa Viti Maalum. Kwa hiyo, lazima kumbukumbu zikae sawasawa.

Name

George Boniface Simbachawene

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibakwe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kama anavyosema Mheshimiwa Mbilinyi, kwamba tatizo la wafanyabiashara wadogo wadogo wanaojulikana…(Kelele)
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, nimemwelewa Mheshimiwa Mbilinyi kwamba Wamachinga tatizo lao siyo kuwajengea, ila tatizo lao ni mazingira yanayofaa kwa biashara zao.
Mheshimiwa Naibu Spika, nami nataka nikubaliane naye kabisa kwa sababu Wamachinga hata ukiwajengea sehemu nzuri namna gani, kwa sababu wateja wa Wamachinga wanajulikana. Kama wateja wale hawafiki, ni kazi bure. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, niziombe Mamlaka za Serikali za Mitaa nchini, Mheshimiwa Rais amesema wasibugudhiwe hawa; maana yake nini? Watafutiwe maeneo yanayofaa kama anavyosema Mheshimiwa Mbunge; yanayofaa kwa shughuli zao. Kwa hiyo, naweza kusema nimeelewa swali la Mheshimiwa Mbunge na kwamba Mamlaka za Serikali za Mitaa zinafahamu wajibu wao na zilikwishaelekezwa na Mheshimiwa Rais alikwishasema kwamba watengewe maeneo yanayofaa kwa shughuli zao.