Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Stephen Hillary Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Korogwe Vijijini

Primary Question

MHE. STEPHEN H. NGONYANI aliuliza:- Shamba la Mkonge la Hale Mwakinyumbi lilimilikiwa na Chavda Ltd. lakini Serikali ililitoa shamba hilo kwa wananchi wa Hale kwa matumizi yao lakini hulimwa huku wakiwa na wasiwasi kila wakati. Je, kwa nini Serikali isiwakabidhi rasmi wananchi wa Hale shamba hilo ili wawe na utulivu wanapoendelea na shughuli zao za kilimo?

Supplementary Question 1

MHE. STEPHEN H. NGONYANI: Mheshimiwa Spika, kwanza nimshukuru sana Naibu Waziri kwa majibu yake mazuri sana yenye matumaini kwa wananchi wa Jimbo la Korogwe Vijijini, pia nimpongeze kwa safari alizofanya katika Jimbo langu. Nina maswali mawili ya nyongeza.
Kwa kuwa Naibu Waziri umefika na kuliona shamba hili ambalo limetelekezwa zaidi ya miaka 22, ni kwa nini sasa Serikali isiwakabidhi wananchi wakalitumia kwa shughuli zao mbadala? (Makofi)
Swali la pili, kwa kuwa mashamba mengi yamechukuliwa mikopo kwenye mabenki na sasa hivi yametelekezwa, nini kauli ya Serikali kwa yale mashamba ambayo yalichukuliwa mikopo, hayaendelezwi na yametelekezwa mpaka muda huu?

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Spika, swali lake la kwanza anataka kufahamu ni lini Serikali itakabidhi sasa wananchi hao mashamba hayo ambayo yametelekezwa muda mrefu ili waweze kuyatumia.
Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema katika jibu langu la msingi, ni kwamba utaratibu ili uweze kumnyang’anya mtu huyu ni lazima ule utaratibu wa kisheria ufwatwe, na ndiyo maana nimesema katika hatua za awali ambazo Serikali imechukua ni kutoa notice kwa hawa ambao wametelekeza mashamba na siyo huyo mmoja tu, yapo mashamba zaidi ya 22 ambapo baada ya ziara yangu wamepewa notice.
Kwa hiyo, niseme tu kwamba taratibu za Serikali zinaendelea, muda ule ukishakwisha ni jukumu la Halmashauri husika kuweza kupendekeza kwa Mheshimiwa Waziri ili na yeye aweze kumshauri Rais kubatilisha, ni lazima ule mchakato wa kisheria utimizwe. Kwa sababu wenzetu wa Korogwe wameshaanza nina imani litafikia mahali pazuri.
Mheshimiwa Spika, swali lake la pili anasema mashamba mengi yamekuwa mapori lakini pia inafahamika kwamba mengine yamechukuliwa mikopo mabenki na nini sasa Serikali inasema nini.
Mheshimiwa Spika, niseme haya yamekuja kuahamika na kuthibitika rasmi baada ya Wizara yangu kuanza kutoa ilani kwa wale ambao wameyatelekeza mashamba yao, lakini kama Serikali tunachofanya sasa ni kuhakikisha tunafanya kazi sambamba na mabenki ili fedha za umma zisipotee, kwa sababu dhamana za hati zile zimewekwa na zimechukuliwa mikopo, lakini pengine mikopo ili haikwenda kunufaisha katika yale maeneo.
Kwa hiyo, jukumu letu sisi tunalofanya, pamoja na ilani zinazotolewa katika mashamba haya, lakini bado kama Serikali tunafanya kazi kwa karibu sana na mabenki ili kuhakikisha kwamba kama zile dhamana walizokuwa wameweka pengine zinakwenda kubatilishwa sasa tujue ni namna gani yale mabenki yataweza kupata pesa zake. Kwa hiyo hili tunalifanya kwa uangalifu ili kuona kwamba pesa za Umma hazipotei lakini pia haki ya wananchi au ya wamiliki wale pia inakwenda sambamba kisheria ili tusijikute kwamba tumekwenda nje ya utaratibu. (Makofi)

Name

Mary Pius Chatanda

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Korogwe Mjini

Primary Question

MHE. STEPHEN H. NGONYANI aliuliza:- Shamba la Mkonge la Hale Mwakinyumbi lilimilikiwa na Chavda Ltd. lakini Serikali ililitoa shamba hilo kwa wananchi wa Hale kwa matumizi yao lakini hulimwa huku wakiwa na wasiwasi kila wakati. Je, kwa nini Serikali isiwakabidhi rasmi wananchi wa Hale shamba hilo ili wawe na utulivu wanapoendelea na shughuli zao za kilimo?

Supplementary Question 2

MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza.
Kwa kuwa suala la mashamba ya mkonge kwa upande wa Korogwe Vijijini inafanana na Korogwe Mjini, na kwa kuwa Korogwe Mjini tayari ilishaingia kwenye mpango kabambe wa masterplan, na kwa kuwa mji huu una mashamba ya mkonge nayo ambayo hayaendelezwi na tayari tulishaleta mapendekezo ya kuomba mashamba hayo yafutwe.
Je, Serikali inatuambiaje na hasa ikizingatia kwamba tupo kwenye ule mpango kabambe wa masterplan kuhakikisha kwamba mashamba hayo yanafutwa ili maeneo hayo yaweze kutumika katika huu mpango kabambe ambao umeandaliwa?

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Spika, naomba nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba hayo mashamba ambayo tayari wao wameleta mapendekezo kwa Waziri ili na yeye aweze kumshauri Rais ayabatilishe ni yale pia katika mchakato ambayo pengine tunasema kwamba kuna maeneo mengine ambapo wamekopea pesa benki.
Kwa hiyo, mchakato unafanyika ili kuweza kujua, na pale pale tunaangalia ile ilani ambapo kama imekwenda sawasawa kisheria, kwa sababu mashamba ni mengi na yote yanahitaji pia umakini katika kuyabatilisha.
Kwa hiyo, tusingependa kutoa ushauri ambao pengine unaweza ukampotosha Mheshimiwa Rais akaja akalaumiwa, tunataka kujiridhisha na masharti yote yaliyopo pale kama yamezingatiwa lakini pia na kuangalia fedha za Umma zisije zikapotea kwa sababu tu hawa watakuwa wamebatilishiwa umiliki wao.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo hilo tunalifanyia kazi na nimwahidi Mheshimiwa Mbunge tutakwenda kuiangalia orodha ya mashamba ambayo anayasema tuweze kuona yamefikia katika utaratibu gani ili hatua nyingine ziweze kuendelea.

Name

Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Primary Question

MHE. STEPHEN H. NGONYANI aliuliza:- Shamba la Mkonge la Hale Mwakinyumbi lilimilikiwa na Chavda Ltd. lakini Serikali ililitoa shamba hilo kwa wananchi wa Hale kwa matumizi yao lakini hulimwa huku wakiwa na wasiwasi kila wakati. Je, kwa nini Serikali isiwakabidhi rasmi wananchi wa Hale shamba hilo ili wawe na utulivu wanapoendelea na shughuli zao za kilimo?

Supplementary Question 3

MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi hii niulize swali dogo tu la nyongeza.
Mheshimiwa Spika, matatizo yaliyopo huko Korogwe yanafanana sana na matatizo yaliyopo katika Jimbo la Itigi; kuna shamba lililokuwa la Shirika la Tanganyika Packers lipo katika eneo la Kitaraka, lilitelekezwa na shirika hili baada ya shirika hili kufilisika mwishoni mwa miaka ya 1980.
Mheshimiwa Spika, wananchi wa maeneo yale katika vijiji vya Kitaraka, Kaskazi Stesheni, Doroto, Majengo, Tambukareli, Kihanju na Sanjaranda wamelitumia shamba lile kulima na linawasaidia sana kupata mahitaji yao ikiwemo mazao ya chakula pamoja na mazao ya biashara, lakini kuna taarifa kwamba Serikali ina mpango wa kulibinafsisha shamba lile kwa wawekezaji.
Je, ni nini kauli ya Serikali kwamba haitaonesha inaleta mgogoro na wananchi ambao shamba lile sasa linawanufaisha wananchi wengi sana wazawa na wananchi wa nchi hii kuliko kuweka mwekezaji, ni nini kauli ya Serikali juu ya suala hilo?

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Spika, ni kweli anachokizungumza kwamba wananchi wamekuwa wakilitumia lile shamba na ametaja vijiji vinavyohusika. Naomba nimfahamishe Mheshimiwa Mbunge kwamba nia ya Serikali ni njema na kama kuna hatua ya kuweka mwekezaji vilevile pia itakuwa ni kwa ajili ya manufaa ya wananchi wa Jimbo lake.
Mheshimiwa Spika, tunachotaka afahamu ni kwamba Serikali haiko pale kunyang’anya wananchi ardhi na kuwaacha wakiteseka. Kitakachofanyika ni kwamba watakaokuwa wa kwanza kufikiriwa ni wale wananchi walioko pale na kwa sababu shamba lile lilikuwa linamilikiwa na Serikali tangu awali kwa maana hiyo Serikali kulipangia matumizi mengine ni sahihi. Tutakachofanya kabla halijapewa mwekezaji lazima yale maridhiano ya awali katika kukubaliana namna ya kuweza kufanya ile kazi yaweze kukubalika kwa sababu wao pia wanatambua hawako pale kihalali kulingana na umiliki wa shamba lile.