Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Livingstone Joseph Lusinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtera

Primary Question

MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE aliuliza:- Upo mradi wa kilimo cha umwagiliaji katika Kijiji cha Mpwayungu kwa jina maarufu Mgangalenga wa muda mrefu na Serikali imegharamia fedha nyingi sana. Je, Serikali ina mpango gani wa kukamilisha mradi huo ili wananchi waweze kunufaika nao?

Supplementary Question 1

MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Spika, kwanza nimshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu, hata hivyo naomba niulize maswali madogo mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Spika, kwa kuwa Mkoa mzima wa Dodoma hakuna sehemu ambayo tuna mto unaotiririsha maji mwaka mzima, na kwa kuwa mradi ule haukuzingatia uchimbaji wa bwawa kwa maana ya kuyahifadhi maji ili baadaye wananchi waweze kuyatumia kwa kumwagilia.
Je, Mheshimiwa Waziri anatuambia nini juu ya uchimbwaji wa bwawa ili tuweze kuvuna maji na baadae tuweze kuyatumia na ili ule mradi uweze kuleta ufanisi?
Swali la pili, kwa kuwa kwenye majibu ya Serikali kuna baadhi ya vitu vingi vimeachwa, Naibu Waziri yuko tayari kuongozana na mimi kwenda kujionea kwa macho hali ilivyo kwenye mradi huo? Ahsante (Makofi)

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Spika, swali la kwanza ni kweli Mkoa wa Dodoma hauna mito ambayo inatiririsha maji mwaka mzima na ndiyo maana Mheshimiwa Lusinde wewe ni shahidi, kupitia Bunge la Bajeti ambalo limeisha juzi juzi hapa la mwaka huu wa fedha tuliagiza kwamba kila Halmashauri ifanye usanifu wa bwawa moja kila mwaka kwa ajili ya kuvuna maji ya mvua na pia kukinga maji ya mifereji au mito ili tuwe na maji toshelezi kwa ajili ya matumizi ya binadamu mifugo na kilimo cha umwagiliaji.
Pamoja na hilo Awamu ya Tano kupitia Wizara ya Maji tumeeamua kwamba miradi yote mikubwa ya maji kuanzia sasa tutakuwa tunaweka mabomba mawili, bomba la maji safi ya kunywa pamoja na bomba kwa ajili ya umwagiliaji na kwa kuanza, mradi ambao unakuja ambao utahusisha ujenzi wa Bwawa la Farkwa kwa ajili ya maji ya Dodoma tumesanifu na tumeweka mabomba mawili, moja kwa ajili ya maji masafi ya binadamu na maji ya umwagiliaji.
Mheshimiwa Spika, swali la pili umeuliza kama niko tayari kuongozana na wewe kwenda kwenye eneo lako kwa sababu sasa hivi ni kipindi cha Bunge, Mheshimiwa Spika kwa ruksa yako niko tayari, lakini baada ya Bunge basi itabidi nipewe ruhusa na Waziri wangu wa Maji na Umwagiliaji.

Name

Joseph Roman Selasini

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Rombo

Primary Question

MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE aliuliza:- Upo mradi wa kilimo cha umwagiliaji katika Kijiji cha Mpwayungu kwa jina maarufu Mgangalenga wa muda mrefu na Serikali imegharamia fedha nyingi sana. Je, Serikali ina mpango gani wa kukamilisha mradi huo ili wananchi waweze kunufaika nao?

Supplementary Question 2

MHE. JOSEPH R. SELASINI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana, Jimbo la Rombo kama yalivyo Majimbo mengine tuna shida kubwa sana ya maji, shida yetu hasa inatokana na kampuni ambayo inasambaza maji katika Jimbo letu Kili Water kuwa na ukata mkubwa baada ya GTZ waliokuwa wafadhili wake kujiondoa. Halmashauri tangu awamu iliyopita imeleta maombi katika Wizara ya Maji ili tuweze kuanzishiwa mamlaka kwa sababu mamlaka ina uwezo wa kukopa kuanzisha vyanzo vipya vya maji ili iweze kusimamia vizuri hali ya maji katika Jimbo letu. Hivi majuzi nimemkumbusha Waziri kuhusu hitaji hilo.
Sasa nataka nijue, je, Serikali ni lini watatusaidia kwa kushirikiana na TAMISEMI ili tuweze kuwa na mamlaka ya maji katika Wilaya ya Rombo itakayoweza kusimamia vizuri usambazaji wa maji yaliyopo na kuanzisha vyanzo vipya vya maji?

Name

Eng. Gerson Hosea Lwenge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Spika, ni kweli kwenye Sera yetu ya Maji ya mwaka 2002 miradi ya maji ni shirikishi kati ya Serikali na wananchi, Serikali inajenga wananchi wanaiendesha kwa mfumo wa kutengeneza hizi mamlaka ndogo ndogo na mamlaka kubwa.
Kwa hiyo, zipo taratibu naomba nimhakikishie Mheshimiwa Selasini kwamba tutakwenda kuliangalia ombi lake viability ya Halmashauri yake kuweza kuendesha huo mradi badala ya Kili water. Kwa hiyo, hilo tunalichukua na tutakwenda kulifanyia kazi. (Makofi)

Name

George Malima Lubeleje

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpwapwa

Primary Question

MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE aliuliza:- Upo mradi wa kilimo cha umwagiliaji katika Kijiji cha Mpwayungu kwa jina maarufu Mgangalenga wa muda mrefu na Serikali imegharamia fedha nyingi sana. Je, Serikali ina mpango gani wa kukamilisha mradi huo ili wananchi waweze kunufaika nao?

Supplementary Question 3

MHE. GEORGE M. LUBELEJE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi na mimi niulize swali moja la nyongeza.
Kwa kuwa, Wilaya ya Mpwapa na Kongwa kuna mabonde mazuri sana ya maji na yanatiririsha maji mwaka mzima. Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga scheme ya umwagiliaji katika vijiji vya Godegode, Nzovu, Bori, Msagali, Tambi, Mang’weta, Chamkoroma, Mseta na maeneo mengine ili scheme hii iweze kusaidia kilimo cha umwagiliaji na kusaidia kuondoa tatizo la njaa, katika maeneo hayo?(Makofi)

Name

Eng. Gerson Hosea Lwenge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Spika, mapendekezo yake ya kutaka scheme hizo za Godegode na zingine mara nyingi tunaziandaa wakati tunatayarisha bajeti, kwa mwaka huu katika mapendekezo ambayo tulikuwa tumeyapitisha kwenye bajeti kwanza ni kuendeleza na kukamilisha scheme ambazo tayari zilikuwa zinaendelea na zina makandarasi, tukasema awamu hii tutaendelea kwanza tufanye usanifu katika miradi mingine itakayofuata baada ya kukamilisha hii ambayo inaendelea. Kwa hiyo Mheshimiwa, Godegode kwanza tuangalie zile scheme ambazo tayari tunazikamilisha halafu tutaanzisha na hizo zingine mpya. Tutazifanyia usanifu Tume ya Umwagiliaji ndiyo kazi kubwa itakayofanya mwaka huu wa fedha katika kuhakikisha maeneo mengi ambayo yanaweza kufanyiwa umwagiliaji tuweze kuyafanyia kazi.