Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 4 Sitting 7 Water and Irrigation Wizara ya Maji 88 2016-09-15

Name

Livingstone Joseph Lusinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtera

Primary Question

MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE aliuliza:-
Upo mradi wa kilimo cha umwagiliaji katika Kijiji cha Mpwayungu kwa jina maarufu Mgangalenga wa muda mrefu na Serikali imegharamia fedha nyingi sana.
Je, Serikali ina mpango gani wa kukamilisha mradi huo ili wananchi waweze kunufaika nao?

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji na Umwagiliaji naomba kujibu swali la Mheshimiwa Livingstone Joseph Lusinde, Mbunge wa Mtera, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, scheme ya umwagiliaji ya Mpwayungu ilijengwa kupitia Mradi Shirikishi wa Kuendeleza Kilimo cha Umwagiliaji (PIDP) mwaka 2005/2006. Ujenzi wa scheme hii ulihusisha ujenzi wa banio na kuchimba mifereji ya kufikisha maji mashambani. Scheme hii ina eneo linalofaa kwa kilimo cha umwagiliaji lenye hekta 160. Eneo lililoendelezwa kwa kufikiwa na mifereji ya udongo linafika hekta 140 ambalo ni kwa ajili ya kilimo cha mpunga lakini kwa sasa eneo linalotumika ni chini ya hekta 25. Kwa sasa Serikali inaendelea na juhudi za kuhamasisha wakulima kulitumia eneo hilo ambalo limeshaendelezwa kwa kilimo cha umwagiliaji.
Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Tume ya Umwagiliaji itafanya mapitio ya usanifu wa mradi huu katika mwaka wa fedha 2016/2017 kwa nia ya kuongeza ufanisi wake.