Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Susan Limbweni Kiwanga

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Mlimba

Primary Question

MHE. SUSAN L. KIWANGA aliuliza:- Serikali imetwaa maeneo ya vijiji katika Kata za Idete, Namwala, Mofu, Mbinga, Igima, Mchombe, Mngeta, Kalengakelu, Mlimba, Kamwene, Chita na Utengule kwa madai kwamba ni maeneo ya hifadhi bila kuwashirikisha wananchi, jambo ambalo limefanya wananchi kushindwa kuendeleza shughuli zao za kilimo na ufugaji na hivyo kuendelea kuwa maskini. Je, Serikali itakuwa tayari kushirikisha wananchi ili kuweka mipaka kati ya maeneo ya kilimo na ufugaji na yale ya Hifadhi ya Taifa ili kuondoa mgogoro wa ardhi uliopo hivi sasa kwa wananchi kukosa maeneo ya kilimo na malisho ya mifugo?

Supplementary Question 1

MHE. SUSAN L. KIWANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti ahsante. Mimi nilifuata utaratibu nimeuliza swali fupi sana, lakini ukiona majibu marefu ujue hapa kuna udanganyifu. Sasa nina maswali mawili ya nyongeza. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimeuliza hili swali tangu nikiwa Mbunge wa Viti Maalum na Ofisi ya Wanyamapori wakati huo alikuwa Ndugu Sarakikya alinijibu kwamba walienda kupima na nikaenda Ofisi ya Ardhi Kilombero wakasema wananchi hawajashirikishwa. Baada ya kuwabana sana mkasema kwamba mnasubiri hela kutoka Ubelgiji na mmeshapata shilingi milioni 100 na sasa mnaaenda kushirikisha na mpaka kwenye Halmashauri yetu tunazo hizi taarifa, mnaenda mkashirikishe vijiji mkapime upya leo unaniletea majibu marefu. Nakuambia mradi wa ardhi hauendi kutatua migogoro unaenda kupima vipande vya ardhi ambavyo havina migogoro, Mheshimiwa Lukuvi huyu hapa. Sasa haya majibu yako mimi siyakubali, hiyo moja. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini sasa kuna barua ninayo hapa, Meneja wa Ramsar ametoa barua iko Kilombero anasema wataenda kutatua hiyo migogoro…
MWENYEKITI: Mheshimiwa Susan nenda kwenye swali.
MHE. SUSAN L. KIWANGA: Sasa ni lini mtaenda kutatua ile migogoro na mmeruhusu wafugaji waende kule kwa wakulima, magomvi karibu yatatokea, ardhi mmeitwaa, mmeenda kufanya nini? Lini mtaenda kurekebisha ile mipaka? Ninachotaka ni safari ya kwenda Kilombero. Mimi nasemea Kilombero lakini kuna Wilaya tatu, Ulanga na Malinyi, kuna vijiji 126 mmechukua bila idhini yao. Nendeni mkafanye kazi, hilo ndilo swali langu, ndiyo, lini mtaenda Kilombero na barua mnayo?

Name

William Vangimembe Lukuvi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ismani

Answer

WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi tunaomjua Mheshimiwa Susan ndiyo lugha yake, hatumshangai.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na maelezo marefu ya Mheshimiwa Susan ni kweli kwamba tunayo migogoro mingi sana na Serikali tunajua kwamba tunayo migogoro mingi. Iko migogoro inayoweza kutatuliwa na Wizara moja moja, lakini iko migogoro ambayo haiwezi kutatuliwa na Wizara moja moja. Juzi nimetoka Kilombero yale yanayonihusu mimi nimejaribu kuyatatua, lakini hayo mengine anayoyasema sisi Serikali tumeunda timu. Hivi sasa tumekutana mimi na mwenzangu Waziri wa Mifugo, Waziri wa Maliasili na TAMISEMI tumeunda timu ziko mtaani huko mikoani na huko Kilombero watafika na nimewaambia hata juzi kwamba haya anayoyasema hayo siyo yangu, kuna Madiwani wameniambia kama alivyoniambia Mheshimiwa Susan.
Kwa hiyo, nimewaambia hili si letu kwa sababu haiwezekani Lukuvi anayekwenda siku moja akatatua mgogoro. Kwa hiyo, tumeunda timu ya wataalam wa Wizara nne wanapitia kuangalia namna bora ya kutushauri sisi Mawaziri tuamue juu ya migogoro hiyo mikubwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Waheshimiwa Wabunge wanakumbuka wakati uliopita tuliwapa fomu fulani mkatupa ile migogoro iko, Mheshimiwa Susan ameandika kwenye kile kitabu. Kwa hiyo, kutokana na kile kitabu sasa tumeunda timu, nataka kukuhakikishia hata sisi kama Serikali tumejiwekea lengo katika miaka hii mitano lazima tuwe tumemaliza migogoro yote. Kwa hiyo, nataka tu kumueleza Mheshimiwa Susan kwamba migogoro ilikuwepo na itaendelea kuwepo lakini tumeamua kuikabili kisayansi.

Name

Venance Methusalah Mwamoto

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. SUSAN L. KIWANGA aliuliza:- Serikali imetwaa maeneo ya vijiji katika Kata za Idete, Namwala, Mofu, Mbinga, Igima, Mchombe, Mngeta, Kalengakelu, Mlimba, Kamwene, Chita na Utengule kwa madai kwamba ni maeneo ya hifadhi bila kuwashirikisha wananchi, jambo ambalo limefanya wananchi kushindwa kuendeleza shughuli zao za kilimo na ufugaji na hivyo kuendelea kuwa maskini. Je, Serikali itakuwa tayari kushirikisha wananchi ili kuweka mipaka kati ya maeneo ya kilimo na ufugaji na yale ya Hifadhi ya Taifa ili kuondoa mgogoro wa ardhi uliopo hivi sasa kwa wananchi kukosa maeneo ya kilimo na malisho ya mifugo?

Supplementary Question 2

MHE. VENANCE M. MWAMOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri, Jimbo la Mlimba na Jimbo la Kilolo ni majimbo yanayopakana. Kwa kuwa vijiji vingi ambavyo vinapakana na hifadhi huwa haviruhusiwi kufanya shughuli zozote za kibinadamu ndani ya hifadhi lakini tembo wamekuwa kero kwenye vijiji hivyo, kwa mfano, Kata ya Ruaha Mbuyuni, Mahenge na Nyanzo hivi ninavyozungumza uharibifu mkubwa wa mazao umefanyika. Je, Serikali itakuwa tayari sasa kutoa tamko lolote leo?

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la wanyama waharibifu kuvamia mashamba, ni kweli Serikali inazo taarifa kutoka katika vijiji mbalimbali vinavyopakana na hifadhi juu ya usumbufu wa wanyamapori wanaoharibu mazao ya wananchi. Siku za nyuma tulikuwa tukijikita zaidi katika kutumia vikosi vya Askari wa Wanyamapori kupambana na wanyama hao, lakini pale inapotokea wameshafanya uharibifu tulikuwa na ule utaratibu wa vifuta jasho.
Hata hivyo, Serikali imeshaona kwamba kutumia vikosi tu vya Askari wa Wanyamapori nguvu hiyo haitoshi lakini pia kusubiri mpaka wanyama wawe wameshafanya uharibifu ndipo tulipe vifuta jasho nao pia siyo mkakati mzuri kwa sababu siyo endelevu wakati mwingine gharama zinakuwa kubwa kuliko bajeti ya Serikali. Kwa hiyo, kuanzia sasa Serikali imejipanga upya kubadilisha ulinzi ule wa kutegemea tu Askari wa Wanyamapori na kwenda kwenye ulinzi shirikishi au kufanya uhifadhi shirikishi. Vijiji vyote vinavyopakana na hifadhi kutapatikana askari ambao watawezeshwa kwa kupewa elimu na silaha kwa utaratibu ambao utaonekana unafaa ili ulinzi sasa ufanyike kwa njia ambayo ni pana zaidi ili kuweza kuzuia zaidi kuliko kusubiri kutibu baada ya kutoa vifuta jasho