Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hamida Mohamedi Abdallah

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Lindi Mjini

Primary Question

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH aliuliza:- Katika karne hii ya sayansi na teknolojia, mawasiliano ya simu za mkononi ni muhimu sana katika kurahisisha na kuharakisha huduma mbalimbali kwa watumiaji wakiwemo wavuvi, wakulima, wafanyabiashara, wafanyakazi, wasanii na kadhalika:- Je, ni lini Serikali itaboresha ujenzi wa minara ya huduma ya mawasiliano ya simu katika Vijiji vya Mkoa wa Lindi?

Supplementary Question 1

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Namshukuru sana Mheshimiwa Waziri kwa majibu yake mazuri, majibu yenye matumani makubwa katika Mkoa wetu wa Lindi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza niipongeze Serikali kwa kuanzisha Mfuko huu wa UCSAF. Kwa utekelezaji wake katika Mkoa wetu wa Lindi ni kata 25 na vijiji 99 ambavyo tunavitarajia vianze kupata mawasiliano. Ningependa kujua ni kwa namna gani Serikali watapeleka msukumo kwa watoa huduma hii ya mawasiliano ili vijiji hivi 99 na kata 25 za Mkoa wa Lindi ziweze kupata mawasiliano?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa juhudi zake za kufuatilia suala hili. Alikuja ofisini na alikutana na Waziri wangu na kwa kweli pamoja na Wabunge wengine wa Mkoa wa Lindi wanalifuatilia sana suala hili ikiwa ni pamoja na Mheshimiwa Waziri Mkuu.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuthibitisha kwamba tutayafuatilia haya makampuni yanayotoa huduma. Kwa wale ambao hawana huduma za kutosha tutahakikisha UCSAF inaingilia ili yapatikane mawasiliano kama ambavyo tumekusudia kutoa mawasiliano kwa vijiji vyote vya Tanzania.

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, nimesema kwamba tutazifuatilia hizi kampuni kuhakikisha kwamba zinatimiza wajibu wake wa kupeleka mawasiliano katika vijiji husika vya Mkoa wa Lindi vyote 99 katika kata 25 pamoja na vijiji vyote Tanzania nzima.

Name

Anna Richard Lupembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nsimbo

Primary Question

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH aliuliza:- Katika karne hii ya sayansi na teknolojia, mawasiliano ya simu za mkononi ni muhimu sana katika kurahisisha na kuharakisha huduma mbalimbali kwa watumiaji wakiwemo wavuvi, wakulima, wafanyabiashara, wafanyakazi, wasanii na kadhalika:- Je, ni lini Serikali itaboresha ujenzi wa minara ya huduma ya mawasiliano ya simu katika Vijiji vya Mkoa wa Lindi?

Supplementary Question 2

MHE. ANNA R. LUPEMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa Mkoa wa Katavi, Wilaya ya Mlele, Kata ya Ilunde imesahaulika kabisa kwa mawasiliano. Je, Serikalini ni lini watapeleka mawasiliano Kata ya Ilunde?

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI, UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyosema katika jibu langu la msingi, tunakusudia kupeleka mawasiliano vijiji vyote Tanzania nzima. Namhakikishia hicho Kijiji cha Ilunde kitapata mawasiliano. Kumwambia lini, naomba anipe muda zaidi niwasiliane na yule mtu anayehusika kupeleka mawasiliano tupate uhakika, nitakuja kujibu nikishapata majibu sahihi. Namhakikishia mawasiliano yatapatikana katika kata hiyo na nitafuatilia kwa makini. Nakushukuru sana kwa juhudi zako za kufuatilia suala hili.

Name

Omary Tebweta Mgumba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini Mashariki

Primary Question

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH aliuliza:- Katika karne hii ya sayansi na teknolojia, mawasiliano ya simu za mkononi ni muhimu sana katika kurahisisha na kuharakisha huduma mbalimbali kwa watumiaji wakiwemo wavuvi, wakulima, wafanyabiashara, wafanyakazi, wasanii na kadhalika:- Je, ni lini Serikali itaboresha ujenzi wa minara ya huduma ya mawasiliano ya simu katika Vijiji vya Mkoa wa Lindi?

Supplementary Question 3

MHE. OMARY T. MGUMBA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi hii ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa matatizo yaliyopo katika Mkoa wa Lindi yanafanana kabisa na yaliyopo katika Mkoa wa Morogoro kwenye Jimbo la Morogoro Kusini Mashariki hasa kwenye Kata za Maturi, Mkulazi, Seregeti na Tununguo. Je, Serikali ina mpango gani wa kuweka minara katika kata hizi na Vijiji vyake vile vya Usungura, Kidunda na vinginevyo ili kuimarisha mawasiliano katika vijiji hivyo?

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba tena kuchukua fursa hii kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge kama nilivyotoa maelezo katika jibu la swali la msingi kwamba tuna dhamira ya kuhakikisha kwamba vijiji vyote vinapata mawasiliano. Kwa hiyo, naomba kuchukua fursa hii kumhakikishia kwamba tutafuatilia kuhakikisha katika Jimbo lake na hizo kata alizozitaja, mawasiliano ya simu yanapatikana kupitia Mic, Airtel, Tigo, Vodacom, Viettel pamoja na wengine ambao wanakuja karibuni tutakapotoa tenda ya masafa ya mawasiliano.

Name

Josephine Johnson Genzabuke

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH aliuliza:- Katika karne hii ya sayansi na teknolojia, mawasiliano ya simu za mkononi ni muhimu sana katika kurahisisha na kuharakisha huduma mbalimbali kwa watumiaji wakiwemo wavuvi, wakulima, wafanyabiashara, wafanyakazi, wasanii na kadhalika:- Je, ni lini Serikali itaboresha ujenzi wa minara ya huduma ya mawasiliano ya simu katika Vijiji vya Mkoa wa Lindi?

Supplementary Question 4

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi. Kwa kuwa Mkoa wa Kigoma ni kati ya mikoa ambayo iko pembezoni na viko vijiji ambavyo vimepakana na nchi jirani ya Burundi na vijiji hivyo havina mawasiliano. Je, Serikali iko tayari kushawishi makampuni kupeleka minara katika Vijiji vya Kitanga (Kasulu), Kilelema (Buhigwe) na Nyagwijima (Kibondo)?

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, tupo tayari na kwa kweli ndicho tunachokifanya siku zote hizi. Mheshimiwa Mbunge anafahamu kwamba katika suala la mawasiliano mipakani ni priority namba moja.