Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 36 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 302 2016-06-03

Name

Hamida Mohamedi Abdallah

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Lindi Mjini

Primary Question

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH aliuliza:-
Katika karne hii ya sayansi na teknolojia, mawasiliano ya simu za mkononi ni muhimu sana katika kurahisisha na kuharakisha huduma mbalimbali kwa watumiaji wakiwemo wavuvi, wakulima, wafanyabiashara, wafanyakazi, wasanii na kadhalika:-
Je, ni lini Serikali itaboresha ujenzi wa minara ya huduma ya mawasiliano ya simu katika Vijiji vya Mkoa wa Lindi?

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Hamida Mohamed Abdallah, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nakubaliana na Mheshimiwa Mbunge kuwa mawasiliano ya simu za mikononi ni muhimu katika kurahisisha na kuharakisha maendeleo na ndiyo maana Serikali imeweka sera madhubuti za kuhakikisha wananchi katika maeneo yote ya nchi wanapata huduma hiyo. Kwa kutambua hilo, Serikali ilianzisha Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) ili kutekeleza sera hiyo kwa kupeleka huduma za mawasiliano katika maeneo yote ya nchi yenye uhitaji wa huduma husika.
Mheshimiwa Naibu Spika, hadi sasa Serikali kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote imetenga jumla ya dola za Marekani 2,186,061 kwa ajili ya kupeleka mawasiliano katika jumla ya kata 25 za Mkoa wa Lindi zilizokuwa ama na huduma duni au kutokuwa na huduma kabisa za mawasiliano ya simu za mikononi. Kati ya Kata hizo, Kata ya Kiegi Wilaya ya Nachingwea imeshapata mawasiliano ya simu za mkononi kupita kampuni ya TTCL wakati kata nyingine ziko katika hatua mbalimbali za ujenzi wa miundombinu ya mawasiliano.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa wote itaendelea kuyaainisha maeneo mengine ya Mkoa wa Lindi na Tanzania kwa ujumla wa kadri ya uhitaji na upatikanaji wa fedha katika kufanikisha malengo ya uanzishwaji wa Mfuko ambayo ni pamoja na kuhakikisha kuwa kila mwananchi wa Tanzania bila kujali mahali alipo anapata huduma za mawasiliano ili kurahisisha na kuhakikisha upatikanaji wa huduma mbalimbali za kimaendeleo.