Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Omary Tebweta Mgumba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini Mashariki

Primary Question

MHE. OMARY T. MGUMBA (K.n.y. MHE. DKT. HADJI H. MPONDA) aliuliza:- Serikali kupitia Wizara ya Nishati na Madini iliahidi kupeleka huduma za umeme katika Hospitali ya Lugala ambayo ni hospitali pekee na tegemezi katika Wilaya nzima ya Malinyi. Katika kutekeleza agizo hili, Oktoba, 2014, TANESCO Mkoa wa Morogoro ilitengewa fedha kwa kuanza ujenzi huo wa 33KV, HT line ya kilometa 3.5 na kuunganisha umeme katika hospitali hiyo na Kijiji cha Lugala lakini hadi leo agizo hilo halijatekelezwa:- (a) Je, sababu gani zilifanya mradi huo usitekelezeke licha ya kutengewa fedha? (b) Je, ni lini hospitali hiyo muhimu kwa wakazi wa Wilaya ya Malinyi itapatiwa huduma ya umeme?

Supplementary Question 1

MHE. OMARY T. MGUMBA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri, naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza. La kwanza, je, Serikali ina mpango gani kupeleka umeme kwenye huduma zingine za jamii kama vile zahanati, Vituo vya Polisi na Ofisi za Serikali ya Kijiji katika Kijiji hicho cha Lugala?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa sababu matatizo yaliyopo Malinyi yanafanana kabisa na matatizo yaliyoko katika Jimbo la Morogoro Kusini Mashariki, je, Serikali ina mpango gani kupeleka umeme katika Vijiji vya Luholole, Misala, Mmalazi, Kivuma, Ludewa na Amini kule kwenye Kata ya Kinole?
Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana.

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, mpango wa Serikali wa kupeleka umeme kwenye maeneo aliyoyataja hasa ya huduma za jamii uko pale pale. Kama nilivyosema mara nyingi kazi kubwa ya mradi wa REA awamu ya tatu, inakusudia kupeleka umeme kwa vipaumbele vya zahanati, shule za sekondari na shule za msingi lakini pamoja na taasisi nyingine za Serikali ikiwa ni pamoja na Magereza. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba maeneo yote ya vituo vya afya, zahanati, shule pamoja na taasisi nyingine yatapelekewa umeme wa uhakiki. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la pili kuhusiana na vijiji alivyovitaja, kama nilivyosema REA awamu ya tatu itapeleka umeme kwenye vijiji vyote ikiwa ni pamoja na vijiji vya Mheshimiwa Mbunge Omary kama alivyovitaja bila kubakiza kijiji chochote.

Name

Dr. Faustine Engelbert Ndugulile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigamboni

Primary Question

MHE. OMARY T. MGUMBA (K.n.y. MHE. DKT. HADJI H. MPONDA) aliuliza:- Serikali kupitia Wizara ya Nishati na Madini iliahidi kupeleka huduma za umeme katika Hospitali ya Lugala ambayo ni hospitali pekee na tegemezi katika Wilaya nzima ya Malinyi. Katika kutekeleza agizo hili, Oktoba, 2014, TANESCO Mkoa wa Morogoro ilitengewa fedha kwa kuanza ujenzi huo wa 33KV, HT line ya kilometa 3.5 na kuunganisha umeme katika hospitali hiyo na Kijiji cha Lugala lakini hadi leo agizo hilo halijatekelezwa:- (a) Je, sababu gani zilifanya mradi huo usitekelezeke licha ya kutengewa fedha? (b) Je, ni lini hospitali hiyo muhimu kwa wakazi wa Wilaya ya Malinyi itapatiwa huduma ya umeme?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. FAUSTINE E. NDUGULILE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipatia fursa ya kuuliza swali la nyongeza. Mji wa Kigamboni au Wilaya mpya ya Kigamboni inakua kwa kasi sana. Umeme kwa wakazi wa Kigamboni unatoka katika Wilaya ya Ilala na ku-supply baadhi ya maeneo ya Wilaya ya Ilala, Temeke, Mbagala yote, Mkuranga yote na Kigamboni yote. Je ni lini sasa Serikali itajenga kituo cha umeme katika Wilaya mpya ya Kigamboni ili kuendana na mahitaji ya sasa?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, Mji wa Kigamboni ni mpya na kwa sasa unatumia umeme kutoka Ilala na umbali uliopo ni zaidi ya kilometa 50. Kwa nguvu iliyopo kwa sasa hivi, uwezo wa kupeleka umeme kwa Kigamboni hautoshi. Mpango wa Serikali utakapokuwa unasambaza umeme kwenye REA awamu ya tatu, utajenga pia kituo cha kupozea umeme kwenye Wilaya ya Kigamboni ili kuhakikishia upatikanaji wa umeme kwa wananchi wa Kigamboni.

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Primary Question

MHE. OMARY T. MGUMBA (K.n.y. MHE. DKT. HADJI H. MPONDA) aliuliza:- Serikali kupitia Wizara ya Nishati na Madini iliahidi kupeleka huduma za umeme katika Hospitali ya Lugala ambayo ni hospitali pekee na tegemezi katika Wilaya nzima ya Malinyi. Katika kutekeleza agizo hili, Oktoba, 2014, TANESCO Mkoa wa Morogoro ilitengewa fedha kwa kuanza ujenzi huo wa 33KV, HT line ya kilometa 3.5 na kuunganisha umeme katika hospitali hiyo na Kijiji cha Lugala lakini hadi leo agizo hilo halijatekelezwa:- (a) Je, sababu gani zilifanya mradi huo usitekelezeke licha ya kutengewa fedha? (b) Je, ni lini hospitali hiyo muhimu kwa wakazi wa Wilaya ya Malinyi itapatiwa huduma ya umeme?

Supplementary Question 3

MHE. JUMAA H. AWESO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Kwa kuwa umeme ni kichocheo muhimu katika shughuli za kiuchumi. Je, ni lini Serikali itapeleka umeme katika Vijiji vya Langoni, Kikokwe pamoja na Kigulusimba Misufini ili kuhakikisha kwamba wananchi wa Pangani wanaenda kushiriki katika shughuli mbalimbali za kiuchumi na kujiletea maendeleo?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa hata sasa hivi bado Serikali inapeleka umeme kwenye vijiji vingi chini ya mradi wa REA awamu ya pili. Hata hivyo, kuna vijiji vingi havijapata umeme. Jimbo la Mheshimiwa la Pangani tunalifahamu, ni vijiji vichache sana vimepata umeme. Nimeshazungumza naye na nikamwambia alete orodha yake ya vijiji ambavyo havijapata umeme na ameshaniletea. Kwa hiyo, napenda kumwambia Mheshimiwa Mbunge wa Pangani vijiji vyake vyote alivyovitaja vitapata umeme kwenye REA awamu ya tatu.

Name

Mendard Lutengano Kigola

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Primary Question

MHE. OMARY T. MGUMBA (K.n.y. MHE. DKT. HADJI H. MPONDA) aliuliza:- Serikali kupitia Wizara ya Nishati na Madini iliahidi kupeleka huduma za umeme katika Hospitali ya Lugala ambayo ni hospitali pekee na tegemezi katika Wilaya nzima ya Malinyi. Katika kutekeleza agizo hili, Oktoba, 2014, TANESCO Mkoa wa Morogoro ilitengewa fedha kwa kuanza ujenzi huo wa 33KV, HT line ya kilometa 3.5 na kuunganisha umeme katika hospitali hiyo na Kijiji cha Lugala lakini hadi leo agizo hilo halijatekelezwa:- (a) Je, sababu gani zilifanya mradi huo usitekelezeke licha ya kutengewa fedha? (b) Je, ni lini hospitali hiyo muhimu kwa wakazi wa Wilaya ya Malinyi itapatiwa huduma ya umeme?

Supplementary Question 4

MHE. MENDRAD L. KIGOLA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza. Suala la umeme vijijini pamoja na ahadi nzuri za Serikali na kwenye bajeti hii ya 2016/2017, Serikali imeahidi vizuri sana na tunasema vijiji vyote vitapewa umeme. Kwenye shule za sekondari, shule za misingi, zahanati na sehemu nyingine za hospitali. Tunaomba Serikali itoe commitment kwamba katika mwaka huu wa fedha tuta-specialize hasa kwenye vituo vya afya na zahanati ili tusi-generalise kwamba tutapeleka kila sehemu?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, kama ambavyo tumekuwa tukieleza, labda niwaombe Waheshimiwa Wabunge watupe ushirikiano kuhusu jambo hili. Wananchi na Waheshimiwa Wabunge wengi wamekuwa wakiomba sana kupelekewa umeme kwenye vijiji vyao badala ya huduma za afya na taasisi nyingine. Namshukuru sana Mheshimiwa Kigola lakini niseme tu mpango wa Serikali wa awamu ya tatu ya REA, unazingatia sana vipaumbele vya kuwapelekea umeme taasisi za jamii pamoja na kwamba tunawapelekea pia kwenye matumizi ya nyumbani. Kwa hiyo, mpango wetu unatekelezwa hivyo. Nimwombe Mheshimiwa Mbunge ikibidi anilitee taasisi zake za umma kabla hatujatoka kwenye Bunge hili ili nimhakikishie kwamba tutaanza na hizo kabla ya kuwapelekea umeme kwenye nyumba zao.