Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 36 Energy and Minerals Wizara ya Madini 296 2016-06-03

Name

Dr. Haji Hussein Mponda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Malinyi

Primary Question

MHE. OMARY T. MGUMBA (K.n.y. MHE. DKT. HADJI H. MPONDA) aliuliza:-
Serikali kupitia Wizara ya Nishati na Madini iliahidi kupeleka huduma za umeme katika Hospitali ya Lugala ambayo ni hospitali pekee na tegemezi katika Wilaya nzima ya Malinyi. Katika kutekeleza agizo hili, Oktoba, 2014, TANESCO Mkoa wa Morogoro ilitengewa fedha kwa kuanza ujenzi huo wa 33KV, HT line ya kilometa 3.5 na kuunganisha umeme katika hospitali hiyo na Kijiji cha Lugala lakini hadi leo agizo hilo halijatekelezwa:-
(a) Je, sababu gani zilifanya mradi huo usitekelezeke licha ya kutengewa fedha?
(b) Je, ni lini hospitali hiyo muhimu kwa wakazi wa Wilaya ya Malinyi itapatiwa huduma ya umeme?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati na Madini, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Hadji Hussein Mponda, Mbunge wa Malinyi, lenye sehemu (a) na (b), kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, mradi wa kupeleka umeme katika Hospitali ya Lugala, Wilayani Malinyi haukuweza kutekelezwa kwa sababu fedha iliyotarajiwa kutengwa kutoka kwenye bajeti ya TANESCO ya mwaka 2014/2015 haikutengwa kutokana na ufinyu wa bajeti ya TANESCO. Hata hivyo, Hospitali hiyo pamoja na Kijiji cha Lugala vitapatiwa umeme mwaka huu kupitia bajeti ya TANESCO. Kazi hii itajumuisha sasa ujenzi wa njia ya umeme wa msongo wa kilovoti 33 yenye urefu wa kilometa tatu, ujenzi wa njia ya umeme msongo wa kilovoti 0.4 yenye urefu wa kilometa tano pamoja na ufungaji wa transfoma mbili za kVA 100 na kVA 200.
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na utekelezaji huo, kazi nyingine itakayofanyika ni kuwaunganishia umeme wateja wapatao 116 katika maeneo hayo. Kazi hii inatarajiwa kuanza mwishoni mwa mwezi Juni, 2016 na itakamilika mwezi Julai, 2016 kwa gharama ya shilingi milioni 329.27.