Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Maria Ndilla Kangoye

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARIA N. KANGOYE aliuliza:- Sekta ya Utalii ni Sekta inayotegemewa kuliingiza Taifa mapato kwa sababu ya vivutio vingi tulivyojaliwa Tanzania:- (a) Je, Serikali ina mkakati gani wa kutekeleza ahadi iliyopo kwenye Ilani ya Uchaguzi ya Mwaka 2016 - 2020 katika kuongeza bajeti ya Wizara ya Maliasili na Utalii? (b) Je, ni nini mkakati wa Serikali kukiimarisha Chuo cha Utalii ili kutoa mafunzo ya Hoteli na Utalii katika ngazi ya Stashahada ili kuongeza ubora wa Watumishi wa huduma za ukarimu na utalii? (c) Je, Serikali ina mkakati gani wa kuweka mazingira bora ya kuwezesha vijana kuanzisha makampuni ya kutembeza watalii katika maeneo mbalimbali ya utalii?

Supplementary Question 1

MHE. MARIA N. KANGOYE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Pamoja na majibu mazuri kutoka kwa Mheshimiwa Naibu Waziri, naomba niulize maswali yangu mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza Vyuo vya Utalii katika Mikoa mingine ya Tanzania hasa katika ngazi ya shahada? (Makofi)
Swali la pili, kwa kuwa Mkoa wa Mwanza una makumbusho mbalimbali ya kihistoria yakiwemo ya Kageye na makumbusho ya kabila la Kisukuma yaliyopo Bujola Wilayani Magu, ambayo yamekuwa yakipoteza umaarufu wake kadri miaka inavyoongezeka. Je, Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha kwamba umaarufu huu wa makumbusho haya unaongezeka ili kuiwezesha Wilaya ya Magu kupata kipato kupitia utalii hasa tukizingatia kwamba Wilaya hii imekuwa na mapato madogo kiasi kwamba, imekuwa haikidhi haja ya utoaji wa asilimia kumi ya mapato yake kwa ajili ya vijana na wanawake?

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu swali lake la kwanza la kuongeza vyuo vya utalii na hasa katika ngazi ya shahada, napenda kutoa maelezo ambayo ndani yake kuna majibu kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la kwanza, Serikali itaelekeza nguvu zake zaidi kwa sasa katika kuimarisha vyuo vilivyopo, vile ambavyo nimevitaja katika campus tatu, mbili zikiwa Dar es Salaam na moja ikiwa pale Arusha.
Mheshimiwa Naibu Spika, wakati tunazingatia kuongeza vyuo zaidi, tutazingatia pia ukweli kwamba kitaalam na hasa unapozungumzia kuongeza mafunzo hayo katika ngazi ya shahada ili wahitimu wenye ngazi ya Shahada waweze kufanya kazi sawasawa na yenye tija, unahitaji zaidi kuwa na wataalam katika ngazi ya kati.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, tutaelekeza nguvu zetu zaidi kwa wataalam wa ngazi ya kati sambamba na kuangalia uwiano kati ya wale wahitimu wanaohitimu katika vyuo vya kati ili tuweze kuboresha zaidi utendaji wa wale ambao watakuwa wamehitimu katika ngazi ya shahada hapo baadaye, lakini kwa sasa hivi tuelekeze nguvu nyingi zaidi katika kuzalisha wataalam katika ngazi ya kati.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu suala la makumbusho yaliyoko katika Mkoa wa Mwanza na umaarufu wake unaoendelea kupungua, namwomba Mheshimiwa Mbunge arejee majibu ya maswali yaliyotangulia hapo awali. Hata hivyo, nitarudia pia kwa ufupi kwamba, hivi sasa mpango wa Serikali kupitia Wizara ya Wizara ya Maliasili na Utalii ni kwenda katika kila Halmashauri ya Wilaya nchini na kuorodhesha aina zote za vivutio vya utalii ikiwemo makumbusho mbalimbali ili tuweze kupanga vizuri zaidi namna ya kuweza kuvitunza vile vilivyopo katika hali iliyopo, kuviboresha na kuweza kuvifanya viweze kuchangia vizuri katika uchumi wa Taifa kwa kadri ambavyo tutaweza kuvitangaza zaidi.

Name

Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Primary Question

MHE. MARIA N. KANGOYE aliuliza:- Sekta ya Utalii ni Sekta inayotegemewa kuliingiza Taifa mapato kwa sababu ya vivutio vingi tulivyojaliwa Tanzania:- (a) Je, Serikali ina mkakati gani wa kutekeleza ahadi iliyopo kwenye Ilani ya Uchaguzi ya Mwaka 2016 - 2020 katika kuongeza bajeti ya Wizara ya Maliasili na Utalii? (b) Je, ni nini mkakati wa Serikali kukiimarisha Chuo cha Utalii ili kutoa mafunzo ya Hoteli na Utalii katika ngazi ya Stashahada ili kuongeza ubora wa Watumishi wa huduma za ukarimu na utalii? (c) Je, Serikali ina mkakati gani wa kuweka mazingira bora ya kuwezesha vijana kuanzisha makampuni ya kutembeza watalii katika maeneo mbalimbali ya utalii?

Supplementary Question 2

MHE. SHABANI O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kuniona. Kwa kuwa Wilaya ya Lushoto ni Wilaya yenye vivutio vingi vya kitalii na vijana wa Lushoto wanafanya kazi ile kwa mazoea. Je, ni lini Serikali itafungua Chuo cha Kitalii ili kuwajengea uwezo vijana wa Lushoto ili wasifanye kazi ile kwa mazoea?

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nawapongeza vijana wa Lushoto kwa moyo wao wa kujitokeza kupenda kufanya kazi katika eneo hili, kwa sababu kupitia kwao, tutaweza kufanya ajira kwa vijana ikawa imepata mchango mkubwa sana kupitia Sekta ya Utalii na kupitia kwao tunaweza kuchangia vizuri zaidi uchumi wa Taifa.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu kufanya kazi kwa mazoea na mahitaji ya kupata mafunzo, kwanza nipate takwimu kwa sababu kwa sasa hivi Mheshimiwa Mbunge ametoa maombi ambayo ni ya jumla, nimtake sasa tuweze kushirikiana, nione kwamba kwenye eneo la Lushoto lile kuna vijana wangapi ambao wamejitokeza kupendelea kuingia katika fani hii. Kwa sababu ninachoamini ni kwamba vyuo tulivyonavyo bado havijaelemewa.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mujibu wa taarifa zilizopo mpaka sasa hivi, vyuo tulivyonavyo bado vina uhitaji wa wanafunzi; lakini kama itajitokeza kwamba vyuo vinalemewa na kuna uhitaji wa kuongeza vyuo vingine, au kuboresha mazingira ya vyuo vilivyopo ili viweze kupokea wanafunzi zaidi, basi Serikali itaweza kuchukua hatua muafaka ili kila mmoja mwenye nia na kiu ya kujiunga kwenye mafunzo yatakayompelekea kuwa na taaluma muhimu ya kushiriki vizuri zaidi kwenye Sekta hii ya Utalii aweze kufanya hivyo bila mashaka yoyote.

Name

Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Primary Question

MHE. MARIA N. KANGOYE aliuliza:- Sekta ya Utalii ni Sekta inayotegemewa kuliingiza Taifa mapato kwa sababu ya vivutio vingi tulivyojaliwa Tanzania:- (a) Je, Serikali ina mkakati gani wa kutekeleza ahadi iliyopo kwenye Ilani ya Uchaguzi ya Mwaka 2016 - 2020 katika kuongeza bajeti ya Wizara ya Maliasili na Utalii? (b) Je, ni nini mkakati wa Serikali kukiimarisha Chuo cha Utalii ili kutoa mafunzo ya Hoteli na Utalii katika ngazi ya Stashahada ili kuongeza ubora wa Watumishi wa huduma za ukarimu na utalii? (c) Je, Serikali ina mkakati gani wa kuweka mazingira bora ya kuwezesha vijana kuanzisha makampuni ya kutembeza watalii katika maeneo mbalimbali ya utalii?

Supplementary Question 3

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kuniona. Kwa kuwa nchi yetu kiutalii na kitakwimu tunaambiwa ni nchi ya pili kwa kuwa na vivutio baada ya Brazil na ili kunufaika zaidi na utalii ambao tunaambiwa pia kitakwimu ndiyo sekta zinazoongoza kwa kuingiza fedha za Kigeni.
Mheshimiwa Naibu Spika, ili kusudi kuiwezesha Bodi ya Utalii Tanzania kufanya promotion na advertisement kwa kiwango cha kuridhisha na hivyo kuongeza idadi ya watalii; je, Serikali iko tayari sasa kuunda chombo maalum ambacho kitasimamia ile Tourism Development Levy kusudi kuiwezesha TTB kufanya promotion na advertisement kwa kiwango kikubwa ili kuvutia watalii wa kutosha na hivyo kuongeza mapato ya Serikali?

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli na nafikiri hapa anatukumbusha tu; kama ambavyo nimesema mara nyingi, nchi yetu ina vivutio vingi vya utalii; na ni ya pili baada tu ya Brazil. Kuhusu suala la Tourism Development Levy (TDL) namna ambavyo inaweza kuchangia zaidi na inavyoweza kusaidia zaidi Bodi ya Utalii, (Tanzania Tourism Board) kufanya majukumu yake vizuri zaidi na wazo la kuanzishwa kwa chombo kingine tena cha kuweza kusimamia TDL, napenda kujibu kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sasa hivi, suala la (Tourism Develeopment Levy - TDL) kama lilivyo, halina matatizo yanayohitaji kuanzishwa kwa chombo kingine kusimamia. Tunahitaji kuboresha vizuri zaidi usimamizi kupitia vyombo vilivyopo chini ya Serikali hivi sasa, lakini ni kweli kwamba tunakwenda sasa kujipanga vizuri zaidi ili mapato yanayopatikana kutokana na Tourism Develepment Levy yaweze kusaidia zaidi Bodi ya Utalii kutimiza majukumu yake ambayo kwa kiwango kikubwa ni kutangaza utalii ndani na nje ya mipaka ya nchi hii kwa ajili ya kuboresha mapato ya Taifa kupitia Sekta ya Utalii.