Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Primary Question

MHE. JAPHET N. HASUNGA aliuliza:- Kuwepo kwa Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya nchini kumekuwa kukileta migongano katika utekelezaji wa sera na shughuli mbalimbali za maendeleo nchini:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuupitia upya mfumo wa ugatuaji wa madaraka (D by D) ili kuweza kuuboresha na kupunguza migongano mbalimbali ya kiutendaji?

Supplementary Question 1

MHE. JAPHET N. HASUNGA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, lakini naomba niulize maswali madogo ya nyongeza. Kwa kuwa mfumo wa ugatuaji wa madaraka ulikuwa na lengo la kuwapa madaraka wananchi kuweza kuwa na maamuzi yao na kutekeleza masuala yao yanayohusiana kufuatana na mazingira yaliyopo; na kwa kuwa Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya wamekuwa ni sehemu ya utekelezaji wa majukumu hayo katika maeneo husika: Je, Serikali haioni haja ya kuupitia upya huu mfumo ili Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya ndio wabaki badala ya kuwa na Wenyeviti wa Halmashauri za Miji, Halmashauri za Wilaya pamoja na Wenyeviti wa Halmashauri za Majiji ambao kidogo wamekuwa wakiongeza gharama kwenye Serikali?
Mheshimiwa Naibu Spika, la pili; kwa kuwa Ofisi za Wakuu wa Wilaya sasa hivi zimekuwa zikikabiliwa na upungufu mkubwa sana wa mapato na kwa sababu Serikali kuu imekuwa haina fedha za kutosha kuweza kuzipatia hizo Wilaya. Je, Serikali haioni haja kwamba Wakuu wa Wilaya sasa iwe ni sehemu ya kutegemea mapato yanayotokana na hizo Halmashauri ili waweze kuendesha majukumu yao na kusimamia sera vizuri katika maeneo husika?
Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, nimeelezea pale awali maeneo haya mawili; nafasi za Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya kwa mujibu wa Katiba, Ibara ya 61 na ile ya Serikali za Mitaa Ibara ya 145 na 146.
Mheshimiwa Naibu Spika, wazo la Mheshimiwa Mbunge ni kwamba ikiwezekana basi hizi nafasi nyingine zitolewe. Kutokana na Katiba hiyo sasa zimekwenda kutungwa sheria. Kuna Sura namba 287 na 288, ambapo 287 inaelekeza katika Halmashauri, kuonyesha structure, jinsi gani kama Mwenyekiti wa Halmashauri, Diwani na kiongozi wa ngazi ya Kijiji anayechaguliwa ndiyo maana ya ile dhana kubwa ya D by D kushusha madaraka kwa wananchi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tukisema uondoe hilo, maana yake umetoa dhana ya D by D. Kwa hiyo, maana yake ni Katiba sasa imetupeleka katika utengenezaji wa sheria ambapo leo hii kijiji kinahakikisha kina Mwenyekiti wake wa Kijiji na Mwenyekiti wake wa Vitongoji, wanafanya maamuzi katika maeneo haya.
Mheshimiwa Naibu Spika, hawa Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya, jukumu lao kubwa ni kusimamia utaratibu na kanuni kuhakikisha kwamba unaendelea kama ilivyo. Kwa hiyo, kitendo cha kuondoa kimojawapo, maana yake, kwanza utakuwa umevunja Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, lakini Sheria za Bunge ambazo zimewekwa humu kwa mujibu wa sheria itakuwa inaonekana hatuko sawasawa. Naamini kwamba mfumo tuliokuwa nao hivi sasa uko sawasawa. Kama kutakuwa na mawazo mengine, basi tutaendelea kuboresha kwa kadri siku zinavyoendelea.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika suala hili la Wakuu wa Wilaya kwamba hawana mapato na mapato yao ikiwezekana yanayotoka kwenye Halmashauri ndiyo yangeweza kuwasaidia kufanya kazi zao.
Mheshimiwa Naibu Spika, lengo kubwa ni kwamba, tunajua Wakuu wa Wilaya na Wakuu wa Mikoa wakati mwingine wanakuwa na changamoto kubwa sana kwenye OC. Jukumu letu kubwa sisi kama Ofisi ya Rais ni kuhakikisha tunaziwezesha ofisi hizi. Kitendo cha mfano, hata hatukipendi sana, saa nyingine kitendo cha Mkuu wa Wilaya kwenda kuomba kwa Mkurugenzi kupewa pesa ya mafuta, mwisho wa siku anashindwa hata kuisimamia Halmashauri husika. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, hili ni jukumu la Serikali Kuu na sisi tutajitahidi, ndiyo maana tunasema kwamba tufanye collection ya mapato. Serikali Kuu inavyopata fedha za kutosha zitasaidia ku-facilitate kazi zake kwa Wakuu wa Wilaya na Wakuu wa Mikoa ziweze kufanya kazi vizuri.

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAMISEMI: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Naibu Waziri wa TAMISEMI, Mheshimiwa Jafo, nataka niongezee majibu hayo katika swali lililoulizwa na Mheshimiwa Japhet Ngailonga Hasunga, Mbunge wa Vwava kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, amesema yeye angependekeza kwamba hawa Wenyeviti wa Halmashauri waondoke na badala yake, kazi zile kwa sababu zinafanywa kwa pamoja katika dhana ya ugatuaji wa madaraka kwenye Halmashauri, basi Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya hawa wachukue nafasi ile. Nataka tu niseme kwamba kusema ukweli hapa itakuwa imekiuka dhana ya checks and balances kwa sababu Wenyeviti ni Wawakilishi wa wananchi na wao ndiyo political figures kwenye maeneo yale, kwa maana ya uwakilishi wa wananchi per se.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hawa Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya ni Wawakilishi wa Serikali Kuu. Kazi yao, pamoja na kazi nyingine ni kuziangalia hizi Halmashauri kama zinafuata sera, sheria za nchi, kanuni, taratibu na maagizo mbalimbali ya Serikali Kuu, pale chini. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa wanamwangalia nani? Wanamwangalia huyu Mwakilishi wa wananchi ambaye yuko pale na wataalam wake hawa kuanzia Mkurugenzi na wataalam wengine kama wanafanya vizuri. Ndiyo maana tunasema, hakuna mwingiliano kwa sababu mwingiliano ni pale ambapo Mkuu wa Mkoa au Mkuu wa Wilaya anaingilia jambo ambalo linakwenda vizuri. Huo ni mwingiliano; lakini anapofanya intervention ya jambo linalokwenda vibaya ili sheria izingatiwe, hii inaruhusiwa kwa sababu ndiyo kazi yake iliyomweka pale. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nataka niongezee majibu haya na niwahakikishie kwamba mfumo wetu sisi Watanzania wa ugatuaji wa madaraka ni mfumo mzuri ambao nchi nyingi za Kiafrika zinakuja kujifunza hapa kwa sababu ni mfumo uliokaa vizuri na unasababisha amani na utulivu katika nchi.
Mheshimiwa Naibu Spika, nadhani tuendelee nao huu hadi hapo baadaye ingawa tunakubali kwamba huwa kuna reforms zimekuwa zikifanyika kuanzia mwaka 1982, mwaka 1992, mwaka 1998, lakini ipo haja ya kuendelea kuboresha lakini siyo katika eneo hili la checks and balances. Tutaharibu system nzima ilivyokaa.

Name

Juma Selemani Nkamia

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chemba

Primary Question

MHE. JAPHET N. HASUNGA aliuliza:- Kuwepo kwa Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya nchini kumekuwa kukileta migongano katika utekelezaji wa sera na shughuli mbalimbali za maendeleo nchini:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuupitia upya mfumo wa ugatuaji wa madaraka (D by D) ili kuweza kuuboresha na kupunguza migongano mbalimbali ya kiutendaji?

Supplementary Question 2

MHE. JUMA S. NKAMIA: Mheshimiwa Naibu Spika, naitwa Nkamia, ahsante. Najua umenikosea kwa sababu leo niko tofauti kidogo.
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu ya Mheshimiwa Waziri na Naibu Waziri nina swali moja tu la nyongeza. Wala sina tatizo lolote na Wakuu wa Wilaya, lakini kama Serikali Kuu inashindwa kumhudumia Mkuu wa Wilaya, anakwenda kuomba Halmashauri ambayo inaongozwa na Mkurugenzi, hiyo checks and balances inatoka wapi? Haoni kwamba Wakuu wengi wa Wilaya watakuwa ni ombaomba sasa kwa sababu OC wanazopata ni kidogo na matokeo yake wanaishi kwa kutegemea fadhila za Wakurugenzi?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba kumekuwa kuna maelezo kwa baadhi ya maeneo kwamba Wakuu wa Wilaya wanawaomba mafuta Wakurugenzi.
Mheshimiwa Naibu Spika, sisi formally yaani kupata taarifa rasmi kwa maana ya kwamba hilo linatokea na kwamba limekubalika, kweli jambo hilo halipo. Kwa hiyo, kama linatokea pengine ni kwa kesi fulani fulani tu, lakini kusema ukweli kwanza hatulikubali na haliruhusiwi kwa mujibu wa sheria. Pia kama linafanyika, linakiuka sheria. Kwa hiyo, niseme tu, siwezi kuridhia udhaifu huu mpaka tufanye utafiti tujue kweli hili jambo linatokea? Kama linatokea, nini tufanye kwa kuzingatia hili linalosemwa na Mheshimiwa Mbunge?
Mheshimiwa Naibu Spika, nadhani jambo hili siyo maeneo yote tuka-generalise kwamba sehemu zote inatokea, siyo kweli. Pia kama linatokea, linakiuka taratibu, kanuni na sheria za mgawanyo wa madaraka na majukumu na the principle of checks and balances.

Name

Oliver Daniel Semuguruka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JAPHET N. HASUNGA aliuliza:- Kuwepo kwa Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya nchini kumekuwa kukileta migongano katika utekelezaji wa sera na shughuli mbalimbali za maendeleo nchini:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuupitia upya mfumo wa ugatuaji wa madaraka (D by D) ili kuweza kuuboresha na kupunguza migongano mbalimbali ya kiutendaji?

Supplementary Question 3

MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipatia nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa zana ya D by D inaonekana bado haieleweki hata kwa sisi Wabunge; je, Serikali ina mpango gani wa kutoa elimu kwa makundi mbalimbali ikiwemo sisi Wabunge na Madiwani?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli hii dhana imekuwa ni dhana ngeni, japo imeanza muda mrefu; lakini hata ukifanya rejea, wakati mijadala yetu katika bajeti mbalimbali za sekta unaona kwamba hata Waheshimiwa Wabunge, ile concept nzima ya D by D bado haijakaa vizuri. Leo hii tulivyokuwa tukijadili katika Wizara ya Elimu, tulivyokuwa tukijadili katika Wizara ya Afya, ukiangalia michango ya Wajumbe wengi sana dhana ya D by D haijakaa vizuri. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, ndiyo maana hata katika kikao chetu tulivyokuwa tukifanya na Wizara ya Afya, Wataalam na sisi Viongozi Wakuu tulivyokuwa tukibadilishana mawazo tukasema ni vyema sasa dhana hii kwanza ikiwezekana iingie hata kwa watu walioajiriwa wa Serikali, wajue falsafa halisi ya dhana ya D by D. Maana yake katika Mpango huu imetupa changamoto pana.
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa tutaangalia jinsi gani tutafanya ili mradi hata Wabunge na Waheshimiwa Madiwani wote kwa pamoja na Watumishi wote wa Serikali wajue nini concept ya D by D? Nini maana ya dhana ya kurudisha madaraka kwa wananchi?
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, hoja yake ni ya msingi, nadhani tutaifanyia kazi kama Ofisi ya Rais, TAMISEMI.

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba uelewa siyo mzuri sana kwenye dhana hii ya ugatuaji wa madaraka, nami napendekeza tu kwa sababu dhana hii ina maudhui makubwa sana katika msingi wa utawala wa nchi yetu. Inapokuwa haieleweki, inasababisha hata mijadala wakati mwingine kutoka nje ya context na pengine siyo kawaida kuonekana pengine mjadala huo anayetoa kwenye context ni mtu ambaye ana nafasi kubwa na kwamba jambo hili lipo kikatiba sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa napendekeza na pengine naomba kwa kupitia swali hili tuone utaratibu kwa sisi Serikali na Bunge; namna ya kufanya kwanza semina hata kwa Wabunge wote kabisa kwenye jambo hili. Mfanye semina na ikibidi kile Chuo chetu cha Uongozi ndiyo kije kituwezeshe katika jambo hili na kama tuna Wataalam ndani ya Serikali tunaweza tukatoa Watalaam, lakini kama kuna wataalam ndani ya Bunge, tutoe. Kwa sababu jambo hili kwa mimi ambaye ni mwanataaluma wa eneo hilo, napata nalo shida sana. Kusema ukweli context imepotea kabisa kwa sababu watu wanatafuta hata kwa upungufu fulani wanafikiri solution ni ku-centralize tena badala ya ku-decentralize. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nadhani tuone namna bora ya kuweza kufanya semina kubwa nzuri ya watu kupata uelewa juu ya jambo hili.

Name

Mary Pius Chatanda

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Korogwe Mjini

Primary Question

MHE. JAPHET N. HASUNGA aliuliza:- Kuwepo kwa Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya nchini kumekuwa kukileta migongano katika utekelezaji wa sera na shughuli mbalimbali za maendeleo nchini:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuupitia upya mfumo wa ugatuaji wa madaraka (D by D) ili kuweza kuuboresha na kupunguza migongano mbalimbali ya kiutendaji?

Supplementary Question 4

MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kuniona. Kwa kuwa Wakuu wa Wilaya ndiyo Watendaji Wakuu ambao wanakutana na wananchi kwa karibu zaidi. Je, Waziri anaweza sasa kufanya mabadiliko badala ya kupeleka OC kwa RAS wakapeleka moja kwa moja kwa DAS ili kusudi waweze kufanya kazi zao vizuri zaidi?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba jambo hili tumeliona na pengine liko dhahiri sana. Kwa sababu kule kuna Mkuu wa Utawala katika Ofisi ya Mkuu wa Wilaya. Pia kuna Mkuu wa Utawala katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa ambaye ndiye RAS na huku anaitwa DAS ambao kazi yao na majukumu tofauti ni maeneo tu. Kwa hiyo, sidhani kama kuna ubaya. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nilisema wakati wa majumuisho yangu siku ya bajeti yangu kwamba tunaangalia namna ya kuhakikisha kwamba OC hizi kwenye Wilaya zinapelekwa moja kwa moja, nasi tumekubaliana. Katika utekelezaji wa bajeti ya mwaka 2016/2017, OC hizi kwenye Wilaya zitapelekwa moja kwa moja kwenye Ofisi za Ma-DAS ili na wenyewe waweze ku-manage pale kama wanavyoafanya Mkoani. Kusema ukweli tunalichukua wazo hili, ni zuri nasi tulishawekea mkakati wake, tutalitekeleza, ni jambo zuri sana.