Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Raphael Masunga Chegeni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busega

Primary Question

MHE. DKT. RAPHAEL M. CHEGENI (K.n.y. MHE. SUSANNE P. MASELLE) aliuliza:- Mwaka 2007 Serikali ilipima viwanja vya Luchelele Wilayani Nyamagana, Mwanza na iliendelea na mpango huo ambapo mwaka 2012 ilifanya tathmini na uhakiki kwa ajili ya kulipa fidia lakini hadi leo wananchi hao hawajawahi kulipwa fidia zao. Je, Serikali inatoa kauli gani kwa wananchi hao wa Luchelele kuhusu hatma yao hasa ikizingatiwa kuwa Waziri wa Ardhi alitoa ahadi mwaka 2015 kuwa atalitatua tatizo hili ndani ya mwezi mmoja?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. RAPHAEL M. CHEGENI: Mheshimiwa Naibu Spika ahsante sana. Napenda nishukuru kwa majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri. Kwa kuwa muuliza swali ametoka Bungeni humu na ameliacha swali hili, mimi naomba niulize kama ifuatavyo:- (Makofi)
Mheshimiwa Waziri, kwa kuwa wananchi wa Luchelele wamekuwa kwa muda mrefu sana wakiahidiwa kuhusu suala la fidia; na pale Luchelele kulikuwa na mpango mpaka kujenga kiwanja cha golf ambacho mpaka leo hii imekuwa ni hadithi; na hii mara kwa mara tunaambiwa kuna fidia italipwa, imechukua muda mrefu. Sasa Serikali imefikia wapi kwa suala la fidia ili kweli wananchi wa Luchelele walipwe fidia yao na Serikali iendelee na mpango wake wa Luchelele kama ilivyopangilia?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa Wilaya ya Nyamagana inapanuka kuelekea sehemu za Luchelele na kwa kuwa mipango mingi kule inafanyika. Je, Serikali kupitia Wizara yako, ina mkakati gani kuhakikisha kwamba ile Luchelele na St. Augustine yote inaendelezwa kwa mpango na masharti ya Mpango Mji wa Jiji la Mwanza?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, katika majibu yangu ya awali nilisema kwamba wananchi hawa watalipwa fidia na taarifa zilizopo kama nilivyosema ni kwamba kuna mkopo kutoka CRDB. Status ya mkopo huo ni nini na tumefikia wapi mpaka sasa? Ni kwamba walipoleta ile request, katika ile shilingi bilioni sita, CRDB walikuwa wameweka commitment yao kuwakopesha shilingi bilioni 5.5. Kwa hiyo, ilivyokuja ile request TAMISEMI, ikaonekana kwamba deni linalodaiwa ni tofauti na mkopo watakaoweza kupata.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, ikatakiwa clarification, ni jinsi gani pesa nyingine itaweza kupatikana hapo? Wakaandikiwa tena barua, Mkurugenzi wa Nyamagana ambayo ni barua ya tarehe 5 Mei, 2016 kumwambia kwamba alete mchanganuo huo sasa, ile tofauti ya shilingi bilioni 2.5 ambayo inatakiwa ku-top up na ile ambayo inatoka CRDB, kuona italipwa vipi na utaratibu wake utakuwaje?
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, wakaleta hiyo feedback tena katika Ofisi ya TAMISEMI lakini hawakuambatanisha ule muhtasari wa vikao vilivyokubaliana hilo. Kwa hiyo, ofisi yetu imepeleka hiyo barua tena. Lengo ni kuleta zile attachments za makubaliano ya kikao ili mradi ofisi ya Rais, TAMISEMI iendelee na process ya kuhakikisha jambo hili linakamilika.
Mheshimiwa Naibu Spika, suala la pili kuhusu mikakati ya kuendeleza Wilaya ya Nyamagana; kama nilivyosema watu wa Nyamagana mpango wao mkubwa ni kuhakikisha maeneo hayo yanapimwa. Tunajua wazi kwamba Jiji la Mwanza ni kubwa sana, ndiyo maana katika suala zima la uendelezaji wake, tunaelekeza hizi Halmashauri na Manispaa zetu ziweze kuweka utaratibu mzuri wa mipango miji.
Mheshimiwa Naibu Spika, nawashukuru sana watu wa Jiji la Mwanza, kwa sasabu kwa utashi wao mzuri na mawasiliano mazuri wamesababisha Jiji la Mwanza libadilike. Kwa kushirikiana na LAPF wametengeneza center nzuri sana ya kibiashara. Ni imani yangu kubwa sana kwamba mpango ule walioufanya LAPF na mikakati yao ya upimaji katika eneo la Nyamagana kuelekea maeneo haya ya Luchelele itaendelea. Lengo kubwa ni kulibadilisha Jiji la Mwanza liendelee kuwa bora, katika suala zima la kuendeleza Kanda ya Ziwa ya nchi yetu.

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza namshukuru Naibu Waziri kwa majibu mazuri, lakini nilitaka kuongezea tu katika majibu yake.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika suala zima la uendelezaji wa Mji wa Mwanza kama ambavyo Mheshimiwa Mbunge ameuliza, Jiji la Mwanza pamoja na Majiji mengine kama 14 yako kwenye utaratibu wa kupanga Miji yao kwa maana ya kuwa na master plan; na Jiji la Mwanza ni mojawapo na master plan yake inaandaliwa na wameshirikishwa vizuri. Kwa hiyo, hata hawa ambao wako Luchelele wamekuwa considered katika ile master plan ambayo iko katika process ambayo inaandaliwa. Baada ya muda mfupi nadhani kwenye mwezi Juni hii itakuwa imekamilika na watakuwa katika utaratibu mzuri.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia katika suala la fidia siyo Luchelele peke yake, ni maeneo mengi labda kwa kutumia fursa hii pia niseme Wizara imejipanga katika kuhakikisha tunawakumbusha wale wote ambao Mashirika na Taasisi mbalimbali ambazo zinadaiwa wakimewo wenzetu wa Airport Dar es Salaam na maeneo mengine na hata yale yaliyochukuliwa na Jeshi. Tunawaandikia ili kuwakumbusha zile fidia waweze kuzilipa kwa sababu zimekuwa za muda mrefu na kadri zinavyokaa ndivyo jinsi gharama ya Serikali inavyokuwa kubwa hasa katika kupitia katika Mashirika yenyewe.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, tutalizingatia na tutaendelea kulifuatilia na watu wa Mwanza, Luchelele na maeneo mengine watafidiwa.

Name

Stanslaus Shing'oma Mabula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyamagana

Primary Question

MHE. DKT. RAPHAEL M. CHEGENI (K.n.y. MHE. SUSANNE P. MASELLE) aliuliza:- Mwaka 2007 Serikali ilipima viwanja vya Luchelele Wilayani Nyamagana, Mwanza na iliendelea na mpango huo ambapo mwaka 2012 ilifanya tathmini na uhakiki kwa ajili ya kulipa fidia lakini hadi leo wananchi hao hawajawahi kulipwa fidia zao. Je, Serikali inatoa kauli gani kwa wananchi hao wa Luchelele kuhusu hatma yao hasa ikizingatiwa kuwa Waziri wa Ardhi alitoa ahadi mwaka 2015 kuwa atalitatua tatizo hili ndani ya mwezi mmoja?

Supplementary Question 2

MHE. STANSLAUS S. MABULA: Mheshimwa Naibu Spika, hoja yangu bado iko pale pale kwamba pamoja na majibu mazuri ya Serikali na utaratibu mzima ambao Jiji la Mwanza unao sasa wa master plan ya miaka 20 ijayo lakini kama tunavyofahamu, pamoja na master plan bado kuna suala la fidia. Luchelele sasa ni takriban miaka kumi tangu wamethaminishwa na fidia wanaambiwa kila leo.
Mheshimiwa Naibu Spika, imefika hatua sehemu wananchi wanachoka. Sasa ukopaji wa fedha hizi umeanza muda mrefu; ulianzia TIB ukashindikana; umehamia CRDB; lakini ili fedha ziweze kupatikana CRDB ni lazima kibali cha Serikali kutoka TAMISEMI kipatikane. Sasa lazima tuliweke vizuri, ni lini Serikali itakuwa tayari kutoa kibali cha fedha ili Halmashauri ipate fedha iende kulipa fidia na mipango inayotarajiwa hata ya master plan ifikie kwenye wakati wake na ikubalike vizuri na wananchi? Nakushukuru sana.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, hapa ninayo barua ya tarehe 5 Mei, 2016. Barua hii inataka ufafanuzi kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Jiji la Nyamagana. Lengo kubwa ni kwamba akisha-meet haya maelezo ambayo yameandikwa humu, tofauti yake ni nini? CRDB kama nilivyosema awali, walikuwa na uwezo wa kutoa mkopo wa shilingi bilioni 5.5. Kulikuwa na tofauti pale kidogo ambapo kulikuwa na maelezo ambayo yalitaka ufafanuzi zaidi.
Mheshimiwa Naibu Spika, Ofisi ya TAMISEMI tarehe 5 Mei ikaandika barua kwa ajili ya hayo maelezo, ambapo kwa mujibu wa barua hii, yenye kumbukumbu Na. CE.214/237/01/31 imani yangu kwamba Mkurugenzi wa Jiji la Mwanza ataweza ku-meet hivi vigezo vya barua hiyo. Halafu mwisho wa siku ni kwamba Waziri mwenye dhamana ataipitia ile document. Lengo ni kwamba wananchi wa eneo hili ambao wanadai fidia, fidia yao iweze kufika.
Mheshimiwa Naibu Spika, najua ni kweli jambo hili la muda mrefu, lakini naamini kwamba vigezo hivi vikipita na vikifika kwa Mheshimiwa Waziri mwenye dhamana, basi atalitolea maamuzi sahihi.

Name

Mwanne Ismail Mchemba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Primary Question

MHE. DKT. RAPHAEL M. CHEGENI (K.n.y. MHE. SUSANNE P. MASELLE) aliuliza:- Mwaka 2007 Serikali ilipima viwanja vya Luchelele Wilayani Nyamagana, Mwanza na iliendelea na mpango huo ambapo mwaka 2012 ilifanya tathmini na uhakiki kwa ajili ya kulipa fidia lakini hadi leo wananchi hao hawajawahi kulipwa fidia zao. Je, Serikali inatoa kauli gani kwa wananchi hao wa Luchelele kuhusu hatma yao hasa ikizingatiwa kuwa Waziri wa Ardhi alitoa ahadi mwaka 2015 kuwa atalitatua tatizo hili ndani ya mwezi mmoja?

Supplementary Question 3

MHE. MWANNE I. MCHEMBA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi name niulize swali dogo la nyongeza.
Kwa kuwa tatizo la Mwanza linafanana na tatizo la Tabora Manispaa, Kata ya Malolo na mpaka sasa hawajalipwa fidia ya aina yoyote na wakati huo huo Mheshimiwa Waziri wa Ardhi aliwahi kufika na kutoa agizo. Je, Serikali inasemaje kuhusu kulipa fidia ya hawa wakazi wa Kata ya Malolo?

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kama nilivyosema katika majibu ya awali ambayo nilikuwa naongezea kwa Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais (TAMISEMI), nimesema Wizara imejipanga katika kupitia; kwa sababu tumekusanya madai haya au migororo na fidia anazozisema mengi yako katika ile orodha tuliyoichukua. Kwa hiyo, tutakachofanya sisi ni kukumbusha taasisi zinazohusika na fidia hiyo ili waweze kulipa, kwa sababu ni nyingi kweli zimekaa muda mrefu.
Mheshimiwa Naibu Spika, hakuna namna nyingine ya kufanya kwa sababu Serikali haiwezi kulipa fidia ambayo inadaiwa taasisi au maeneo mengine tofauti. Kwa hiyo, tutakachofanya sisi ni kupeleka kumbukumbu za kuwakumbusha wahusika na pale ambapo Serikali inahusika yenyewe basi itajipanga namna ya kuweza kuilipa.