Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 39 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 325 2016-06-09

Name

Susanne Peter Maselle

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. RAPHAEL M. CHEGENI (K.n.y. MHE. SUSANNE P. MASELLE) aliuliza:-
Mwaka 2007 Serikali ilipima viwanja vya Luchelele Wilayani Nyamagana, Mwanza na iliendelea na mpango huo ambapo mwaka 2012 ilifanya tathmini na uhakiki kwa ajili ya kulipa fidia lakini hadi leo wananchi hao hawajawahi kulipwa fidia zao.
Je, Serikali inatoa kauli gani kwa wananchi hao wa Luchelele kuhusu hatma yao hasa ikizingatiwa kuwa Waziri wa Ardhi alitoa ahadi mwaka 2015 kuwa atalitatua tatizo hili ndani ya mwezi mmoja?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Susanne Peter Maselle, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, eneo la Luchelele lilipimwa mwaka 2008 likiwa na ukubwa wa hekta 873.38 ambapo viwanja vilivyopimwa ni 3,583. Katika zoezi hilo wapo wananchi waliokuwa ni wamiliki wa asili wa eneo hilo wapatao 683 ambao kwa makubaliano maalum yaliyofanyika tarehe 27/01/2013 chini ya Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana, wamemilikishwa viwanja badala ya fidia.
Mheshimiwa Naibu Spika, wananchi wanaodai fidia katika eneo la Luchelele ni wale ambao walikutwa katika maeneo yao lakini baada ya upimaji, maeneo hayo ni kwa ajili ya Taasisi au barabara na idadi yao ni 671. Wananachi hao wanadai fidia ya shilingi bilioni sita. Kauli ya Serikali ni kwamba wananchi hao watalipwa fidia na tayari Halmashauri imeomba mkopo kutoka Benki ya CRDB ambao wamekubali kutoa mkopo huo ili wananchi hao waweze kulipwa fidia