Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Josephine Tabitha Chagulla

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPHINE T. CHAGULA aliuliza:- Wilaya ya Nyang’hwale ni moja kati ya Wilaya mpya zilizoanzishwa hivi karibuni ili kuharakisha utoaji wa huduma kwa wananchi. Je, Serikali ina mpango gani wa haraka wa kuwezesha kujenga ofisi na nyumba za watumishi katika Makao Makuu ya Wilaya eneo la Karumwa?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPHINE T. CHAGULA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Pamoja na majibu mazuri sana ya Mheshimiwa Naibu Waziri, naomba nimuulize swali la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, tatizo la ukosefu wa nyumba za kuishi watumishi katika Halmashauri ya Wilaya ya Nyang’hwale ni kubwa sana; watumishi hawa hulazimika kutembea umbali wa kilometa 50 mpaka 80, lakini wengine wanaishi Mkoani kabisa Geita ambako ni umbali wa kilometa 100. (Makofi)
Je, Serikali haioni kuna haja sasa ya kuharakisha majengo haya ili watumishi hawa waweze kuishi karibu na ofisi zao?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, tumekisikia kilio hiki, ndiyo maana mwaka huu tumetenga bajeti ya shilingi milioni 850.
Nawapongeza kwa sababu mshauri ameshaanza zile kazi za awali; ramani imeshapatikana na bajeti iliyolipwa pale kwa shilingi milioni 177, pesa iliyobakia inaonekana mkandarasi aliyepatikana hawezi kuanza kufanya kazi. Ndiyo maana tumesema kwamba mwaka huu tumetenga shilingi milioni 850, lengo letu kubwa ni kwamba tukichanganya na zile za mwanzo sasa, mkandarasi aweze kuingia site na hii kazi iende kwa haraka.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimwahidi Mheshimiwa Mbunge kwamba katika mchakato huu wa bajeti tutaharakisha fedha hizi ziende mapema ili mradi ujenzi uweze kuanza kwa wakati ili kuondoa kero kwa watumishi hawa ambao wanasafiri katika umbali mrefu.

Name

Amina Nassoro Makilagi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPHINE T. CHAGULA aliuliza:- Wilaya ya Nyang’hwale ni moja kati ya Wilaya mpya zilizoanzishwa hivi karibuni ili kuharakisha utoaji wa huduma kwa wananchi. Je, Serikali ina mpango gani wa haraka wa kuwezesha kujenga ofisi na nyumba za watumishi katika Makao Makuu ya Wilaya eneo la Karumwa?

Supplementary Question 2

MHE. AMINA N. MAKILAGI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Tatizo la nyumba na ofisi katika Halmashauri mpya ya Wilaya ya Nyang’hwale ni sambamba na matatizo katika Halmashauri nyingi zilizoanzishwa hapa nchini ambazo ni mpya. Sasa napenda kujua, je, Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha inatenga fedha za kutosha kwa ajili ya kujenga ofisi mpya na nyumba mpya katika Halmashauri zote nchini zilizoanzishwa ikiwemo na Halmashuri ya Butiama ambako ndiko alikotoka Baba wa Taifa?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa mama yangu na wamama wa Tanzania, Mheshimiwa Mama Amina Makilagi kama ifuatavyo:- (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali hili ni lazima nilijibu taratibu sana kwanza. Kweli hoja aliyoitoa Mheshimiwa Mama Makilagi ni ya msingi sana, ndiyo maana siku tulipokuwa tukihitimisha bajeti yetu ya TAMISEMI nilisema kwamba Halmashauri zile mpya lazima tuhakikishe tunaweka miundombinu na ni lazima nyumba zijengwe. Ndiyo maana katika kipaumbele chetu sisi cha TAMISEMI katika bajeti yetu ya mwaka huu, tuliziorodhesha zile Halmashauri ambazo ujenzi unaanza, lakini Halmashauri nyingine mpya hata ujenzi haujaanza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sababu swali hili ni kubwa na zito na limetolewa na Mbunge mzito, niseme yafuatayo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, katika kuliona hili tunaweka kipaumbele; kuna Halmashuri mpya zipatazo 20 tumezitengea kila moja shilingi bilioni 2,140,000,000 kila Halmashuri moja! Halmashauri hizo ni Buchosa, Bunda TC, Chalinze DC, Handeni TC, Ifakara TC, Itigi DC, Kasulu TC, Kibiti DC, Kondoa TC, Madaba DC, Mafinga TC, Malinyi DC, Mbinga TC, Mbulu TC, Mpimwa TC, Nanyamba TC, Newala TC, Nzega TC, Songwe DC na Tunduma TC. Hizi kila moja tumezitengea shilingi bilioni 2,140,000,000.
Mheshimiwa Naibu Spika, sambamba na hilo, kuna Halmashauri zipatazo 44 tumezitengea kati ya shilingi milioni 500 na shilingi milioni 850. Hii maana yake ni nini? Wajumbe mbalimbali inawezekana wakasimama hapa kutaka kujua juu ya hoja hiyo.
Nakala hii iko hapa, mtu anaweza akafanya reference katika Halmashauri yoyote ambapo mwaka huu tumeweka kipaumbele, lazima Ofisi ya Rais, TAMISEMI ihakikishe inajenga miundombinu katika maeneo hayo, ili mradi wafanyakazi waweze kupata huduma bora na waweze kupata mazingira rafiki ya kufanyia kazi.

Name

Hussein Nassor Amar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyang'hwale

Primary Question

MHE. JOSEPHINE T. CHAGULA aliuliza:- Wilaya ya Nyang’hwale ni moja kati ya Wilaya mpya zilizoanzishwa hivi karibuni ili kuharakisha utoaji wa huduma kwa wananchi. Je, Serikali ina mpango gani wa haraka wa kuwezesha kujenga ofisi na nyumba za watumishi katika Makao Makuu ya Wilaya eneo la Karumwa?

Supplementary Question 3

MHE. HUSSEIN N. AMAR: Hussein Nassor Amar, Mbunge wa Jimbo la Nyang’hwale.
Mheshimiwa Naibu Spika, nampongeza Naibu Waziri wa TAMISEMI kwa majibu yake mazuri ya kwamba tumetengewa shilingi milioni 850 katika Halmashauri ya Nyang’hwale. Namuomba Mheshimiwa Waziri kwamba kwa kuwa kuna pesa ambayo imetengwa, shilingi milioni 80 kwa ajili ya kulipa fidia kwa wananchi wenye eneo lile. Naomba amuagize Mkurugenzi zoezi hilo la kuwalipa wananchi lifanyike haraka ili ujenzi huo uanze kujengwa mara moja. Ahsante.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, anayezungumza hapa ni Mbunge wa Jimbo hilo, maana yake yeye anayajua ya huko yalivyo na hizo pesa wameshatenga tayari. Hizo pesa kama zipo sasa, nadhani tusifanye ajizi. Namuomba Mkurugenzi haraka sana, kama vigezo vyote vimetimia, hakuna sababu kuwacheleweshea ulipaji wa fidia. Tunachotaka ni kwamba fidia ilipwe, ujenzi uendelee.
Mheshimiwa Naibu spika, kwa hiyo, moja kwa moja Mheshimiwa Mbunge ni kwamba tunamwelekeza Mkurugenzi wa Nyang’hwale ahakikishe kwamba kama kuna hiyo fedha imetengwa na ipo, watu walipwe fedha zao ili mradi hii kazi hii isiendelee kuchelewa tena kwa sababu ina maslahi mapana kwa wananchi wa Nyang’hwale.