Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 39 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 324 2016-06-09

Name

Josephine Tabitha Chagulla

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPHINE T. CHAGULA aliuliza:-
Wilaya ya Nyang’hwale ni moja kati ya Wilaya mpya zilizoanzishwa hivi karibuni ili kuharakisha utoaji wa huduma kwa wananchi.
Je, Serikali ina mpango gani wa haraka wa kuwezesha kujenga ofisi na nyumba za watumishi katika Makao Makuu ya Wilaya eneo la Karumwa?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Josephine Tabitha Chagula, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa fedha 2014/2015 Halmashauri mpya ya Nyang’hwale ilipokea shilingi milioni 450 kwa ajili ya kuanza ujenzi wa ofisi katka Makao Makuu ya Wilaya iliyoko Karumwa. Kati ya fedha hizo, shilingi milioni 177.7 zimetumika kumlipa Mtaalam Mshauri ambaye ni BJ Amili Limited kwa ajili ya kuandaa michoro, upembuzi yakinifu na usanifu wa eneo lote zinalojengwa ofisi. Kiasi kilichobaki kinajumuishwa katika fedha zilizoombwa mwaka 2016/2017 kwa ajili ya kuendeleza ujenzi.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika bajeti ya mwaka 2016/2017 Halmashauri hiyo imetengewa shilingi milioni 850 kwa ajili ya kuendela na ujenzi majengo ya Makao Makuu ya Halmashauri katika eneo la Karumwa. Azma ya Serikali ni kuhakikisha ofisi na nyumba za watumishi zinajenwa katika Wilaya na Mikoa mipya kwa awamu ili kuboresha mazingira ya kufanyia kazi.