Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Vicky Paschal Kamata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. VICKY P. KAMATA (K.n.y MHE. CONSTATINE J. KANYASU) aliuliza:- Mgodi wa GGM - Geita umepewa eneo la ukubwa wa kilometa za mraba 192 kwa ajili ya kuchimba dhahabu wakati wananchi wamenyang‘anywa maeneo yao. Je, ni lini maeneo waliyonyang‘anywa wananchi yatarudishwa kwa wananchi?

Supplementary Question 1

MHE. VICKY P. KAMATA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante pamoja na majibu mazuri sana ya Mheshimiwa Naibu Waziri nina maswali mawili ya nyongeza.
Kwa kuwa wananchi wa Nyamalembo, Nyamasagata, Semina na sehemu zote ambazo hawa wawekezaji wa GGM wamechukua maeneo yao ningependa kufahamu ni nini manufaa ya moja kwa moja wanayoyapata wananchi hao ambao waliruhusu maeneo yao yanatumiwa na GGM?
Swali la pili, kwa kuwa Serikali imekuwa ikiahidi mara kwa mara kuwapatia maeneo ya uhakika na ya kudumu wachimbaji wadogo na kwa kuwa mpaka sasa bado haijawapatia wachimbaji hawa. Je, Serikali inapanga nini kutatua tatizo hilo, ukizingatia hivi karibuni mwezi wa saba ile PML ya STAMICO ina expire ni kwa nini Serikali isitoe tamko hili sasa hivi hapa kwamba mara baada ya hii PML ku-expire basi lile eneo litapewa wachimbaji wadogo wadogo?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, manufaa ya wananchi wa Geita kulingana na mgodi huu ni kweli kabisa Watanzania wengi na wananchi wa Geita hasa wa maeneo yanayozunguka mgodi huu wamekuwa wakitarajia manufaa makubwa sana. Lakini hata hivyo mambo ambayo wananchi wa maeneo hayo wamenufaika ni kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, mgodi ulipoanza mwaka 1999 wananchi wanaozunguka mgodi huo walifanyiwa fidia. Wananchi ambao waliofanyiwa fidia ni pamoja na maeneo ya Nyamalembo, wananchi wa Nyamalembo wapatao 346 walilipwa fidia jumla ya shilingi bilioni sita nukta nane, lakini wananchi wa Katoma ambao wanafikia karibu 732 walilipwa shilingi bilioni 2.7 kama fidia na wananchi wengine wa Nyakabale, Nyamatagata ambao wanafikia 700 walilipwa shilingi bilioni 732 hayo ni manufaa ambayo wananchi hao waliyapata.
Lakini hata hivyo, pamoja na manufaa hayo mgodi wa GGM umeendelea kutoa ushuru kwa wananchi wanaozunguka maeneo hayo ambayo ni service levy. Hadi sasa mgodi huo umeshatoa takribani shilingi bilioni 4.7 kama service levy lakini manufaa mengine wanayoyapata wananchi hawa ni pamoja na ajira. Mgodi wa GGM hivi sasa unaajiri Watanzania wanaofikia 1568 kama nilivyozungumza kwenye jibu langu la msingi wakati wa bajeti yetu. Lakini kadhalika bado mgodi GGM wananchi wanaozunguka maeneo ya Geita, Nyamatagata, Katoma, Nyakabale, pia wamezungumzia kujengewa hospitali, vituo vya afya pamoja na shule za msingi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu swali lake la pili, kuhusu kuwapatia maeneo hasa ya Mgodi wa Bacliff ambao sasa hivi unamilikiwa na STAMICO pamoja na wabia wenzake. Niseme tu nitumie nafasi hii nimshukuru sana Mheshimiwa Mbunge Kamata ameendelea kupambana sana kwa wananchi wa Geita na mimi nimuombe aendelee kupambana. Lakini nimhakikishie tu sasa hivi Serikali inakamilisha mazungumzo kupitia STAMICO pamoja na wabia wake ili kuona sasa ni eneo gani kampuni yetu ya STAMICO pamoja na wabia wake kwenye Mgodi wa Bacliff maeneo yapi wanaachi kwa ajili ya wananchi wa Geita. Hata hivyo Serikali inaendelea kuwategea maeneo mengine mbadala karibu na mgodi huo. Maeneo ambayo Serikali itayatenga kama ambavyo tunasema kila siku pamoja na maeneo ya Mgusu pamoja na maeneo mengine machache sana ya kule Nyakabale pamoja na Nyamalembo.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pia tumeshatenga maeneo mengine kule Kasubuya, Mheshimiwa Mbunge Kamata unajua ulikwishakuja tukazungumza sana tumewatengea hekta 432; kule Kasubuya. Lakini kule Matabe tumewatengea hekta 568; kule Chato kule kwangu kule tumewatengea hekta 1258; lakini pia bado tunawatengea maeneo mengine hekta 232 maeneo ya Geita.
Kwa hiyo, nimuomba sana Mheshimiwa Vicky Kamata bado tuko na wewe naomba uje ukae tena tuendelee kukaa tupange kama ambavyo huwa tunapanga siku zote kwa niaba ya wananchi wa Geita, ahsante.

Name

Rwegasira Mukasa Oscar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Biharamulo Magharibi

Primary Question

MHE. VICKY P. KAMATA (K.n.y MHE. CONSTATINE J. KANYASU) aliuliza:- Mgodi wa GGM - Geita umepewa eneo la ukubwa wa kilometa za mraba 192 kwa ajili ya kuchimba dhahabu wakati wananchi wamenyang‘anywa maeneo yao. Je, ni lini maeneo waliyonyang‘anywa wananchi yatarudishwa kwa wananchi?

Supplementary Question 2

MHE. OSCAR R. MUKASA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri napenda kusikia pia kauli ya Serikali kuhusu pia wachimbaji wadogo wa Biharamulo wakiwemo wa Busiri, Kalukwete, Mavota, Kalenge na wale Nyanchimba Wilaya Chato kwa sababu nao wanapenda kusikia kauli ya kutengewa hekta kadhaa 500, 600 kama ilivyofanyika kwenye maeneo ya Geita.

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, kama ambavyo nimesema na nitumie nafasi hii nikushukuru sana rafiki yangu Mheshimiwa Mbunge wa Biharamulo kwa sababu ni jirani yangu, maeneo ya Biharamulo mwaka jana tumetenga hekta 1332 kwa Mheshimiwa Oscar, lakini Mheshimiwa Oscar bado tunakutengea eneo pale kwenye Mgodi wa Tulawaka, pale Mavota tunafanya mazungumzo. Tumeshakaa na wewe na Mbunge wa Bukombe tumeainisha mahektari kama hekta 2100 tuzitenge kwa ajili ya wananchi wako, lakini bado nikushukuru sana kwa sababu umependa pia nizungumzie kwangu kule Chato. Kule Chato Kampuni ya Wakawaka
imeachia eneo takribani ya hekta mbili ambako wananchi wako wa Biharamulo na wangu tutawagawia kwa utaratibu huo huo.

Name

Mboni Mohamed Mhita

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Handeni Vijijini

Primary Question

MHE. VICKY P. KAMATA (K.n.y MHE. CONSTATINE J. KANYASU) aliuliza:- Mgodi wa GGM - Geita umepewa eneo la ukubwa wa kilometa za mraba 192 kwa ajili ya kuchimba dhahabu wakati wananchi wamenyang‘anywa maeneo yao. Je, ni lini maeneo waliyonyang‘anywa wananchi yatarudishwa kwa wananchi?

Supplementary Question 3

MHE. MBONI M. MHITA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa fursa ya kuweza kuuliza swali la nyongeza kama ifuatavyo:-
Jimbo la Handeni Vijiji kwenye Kata ya Kang‘ata eneo la Magambazi, kuna mgogoro kati ya wananchi na mwekezaji lakini kwa sasa mgogoro huo unasubiri maamuzi kutoka kwenye Wizara ya Nishati na Madini. Lakini wakati huo huo mgogoro huo umeweza kusimamisha shughuli nyingi ambazo kwa namna moja ama nyingine zingeweza kunufaisha wananchi wa Kata ya Kang‘ata na eneo la Magambazi. Je, ni lini Wizara itatoa maamuzi juu ya utatuzi wa mgogoro huu ili shughuli ziweze kuendelea? Ahsante sana.

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli maeneo ya Handeni pamoja na maeneo mengi ya Kilindi kuna migogoro mingi sana kati ya wachimbaji wadogo, wananchi pamoja na wawekezaji kutoka nje. Lakini kwa jitihada ambazo tumechukua hasa kwa maeneo ya Handeni wiki iliyopita tulimtuma mkaguzi wa migodi kwenda kukagua migogoro iliyopo kati ya wananchi wa Magambazi pamoja na wawekezaji wanaochimba pale. Hivi sasa kampuni ambayo ilikuwa inachimba pale Kampuni ya Scanda ambayo pia ilifanya utafiti haijakamilisha kazi zake. Lakini nimhakikishie tu timu yetu ipo pale sasa na tukitoka hapa Mheshimiwa wa Handeni tukae tukubaliane tufuatilie timu imefikia hatua gani lakini tumeipa muda wa wiki mbili na wiki ijayo wataleta taarifa na taarifa hiyo tunahakikisha kwamba itatoa suluhisho na mgogoro wa wananchi wa Handeni pamoja na wachimbaji hao.

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Primary Question

MHE. VICKY P. KAMATA (K.n.y MHE. CONSTATINE J. KANYASU) aliuliza:- Mgodi wa GGM - Geita umepewa eneo la ukubwa wa kilometa za mraba 192 kwa ajili ya kuchimba dhahabu wakati wananchi wamenyang‘anywa maeneo yao. Je, ni lini maeneo waliyonyang‘anywa wananchi yatarudishwa kwa wananchi?

Supplementary Question 4

MHE. HUSSEIN M. BASHE: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru naomba kumuuliza swali fupi Mheshimiwa Waziri pamoja na jitihada alizozifanya katika Mgodi wa Resolute, Nzega. Je, sasa Serikali iko tayari leseni iliyokuwa chini ya MRI iweze kugawia kwa wachimbaji wadogo wa Mwaishina ambayo maarufu kwa namba saba original katika mji wa Nzega?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, eneo lililokuwa likimilikiwa na kampuni maarufu sana ya uchimbaji iliyoanza hapa nchini Resolute lilimilikiwa sasa na Serikali kupitia Chuo chetu cha Madini (MRI). Ni kweli kabisa lengo kubwa la mgodi kumilikisha kwa Serikali ili ku-plan kutoa fursa kwa wanafunzi wa Tanzania ambao wanasoma masomo kwa nadharia waweze sasa kupata eneo kwa kufanya kwa vitendo ndiyo maana tunawagawia eneo lile. Lakini nikubaliane na hoja ya Mheshimiwa Bashe tumeshazungumza naye, tumeshaweka mikakati ili tuone ni eneo gani ambalo Serikali kupitia MRI hawalihitaji ili waweze kugawia wananchi wa Nzega lakini hata hivyo tumechukua hatua mbadala zaidi ya hapo. Mheshimiwa Bashe nikuhakikishie Kampuni ya Zari Exploration imeachia kilometa nyingine kumi karibu na eneo hilo ambao wananchi wako wa Nzega tutawagawia kwa utaratibu wa Serikali.