Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

George Malima Lubeleje

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpwapwa

Primary Question

MHE. GEORGE M. LUBELEJE aliuliza:- Serikali ilikwishaanza kujenga vituo vya afya katika vijiji vya Mima na Mbori na ujenzi huo umesimama kutokana na ukosefu wa fedha. Je, Serikali ina mpango gani wa kukamilisha ujenzi wa vituo hivyo ili wananchi wa maeneo hayo wapate huduma za afya?

Supplementary Question 1

MHE. GEORGE M. LUBELEJE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi niweze kuuliza maswali mawili ya nyongeza pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza, pamoja na kutenga shilingi milioni 15 kwa ajili ya ukamilishaji wa Kituo cha Mima na shilingi milioni 35 kwa ajili ya kukamilisha Kituo cha Afya cha Mbori, je, Mheshimiwa Waziri haoni fedha hizi zilizotengwa ni kidogo kiasi kwamba vituo hivi vitachukua zaidi ya miaka mitano kukamilika?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa kuna majengo ya zahanati ya Kijiji cha Igoji Kaskazini na Igoji Kusini Salaze yamekamilika na kinachohitajika sasa ni huduma za dawa.
Je, yuko tayari sasa majengo haya yakaanza kutumika kwa ajili ya huduma za dawa?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa George Lubeleje, kama nilivyosema wiki iliyopita kwamba yeye ni greda za zamani lakini makali yale yale. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli Kituo cha Mima kimetengewa shilingi milioni 15 na Mbori shilingi milioni 35, Mbunge anasema fedha hizi hazitoshi. Hata hivyo, katika mchakato wa bajeti tulikuwa tunapokea mapendekezo mbalimbali ambapo wahandisi wetu walifanya analysis ya kila jengo linahitaji kiasi gani ili liweze kukamilika. Kama fedha hizi hazitoshi basi tutaangalia nini cha kufanya.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini katika jibu langu la swali la msingi la wiki iliyopita nilisema, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, Wizara ya Afya na Kamati ya Bunge tulifanya zoezi moja ambalo tunaendelea kulifanya mpaka hivi sasa na tumeshapeleka maelekezo mbalimbali kwa Wakurugenzi wetu wa Halmashauri, wabainishe miradi yote ambayo haijakamilika halafu tuifanyie analysis tuone ni jinsi gani tutafanya ili mradi miradi hiyo yote iweze kukamilika. Kwa sababu ukiachia kwa Mheshimiwa Lubeleje sambamba na hilo kuna maeneo mbalimbali miradi mingi sana iliyojengwa miaka ya nyuma bado haijakamilika. Kwa hiyo, ndiyo maana Ofisi yetu ikaamua ni vyema tubainishe miradi yote na tuifanyie tathmini ya kina ili tujue tunahitaji pesa kiasi gani ili iweze kukamilika.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimuahidi Mheshimiwa Lubeleje kwamba lengo letu ni kukamilisha maeneo haya nikijua wazi kwamba Halmashauri ya Mpwapwa na Jimbo lake la Mpwapwa na Kibakwe ambapo kijiografia ni eneo kubwa sana, wananchi wake lazima wapatiwe huduma. Kwa hiyo, tuna kila sababu kama Ofisi ya Rais, TAMISEMI kuhakikisha huduma za wananchi hasa huduma za afya zinapatikana.
Mheshimiwa Naibu Spika, suala la kwamba vituo vya afya vimekamilika lakini kuna tatizo kubwa la ukosefu wa dawa na vifaa tiba, naomba nimuahidi Mheshimiwa Mbunge, kama nilivyofanya siku chache zilizopita kutembelea Jimbo lake na kubaini huduma na changamoto mbalimbali, tutajitahidi kadiri iwezekanavyo vituo hivi viweze kufanya kazi ili wananchi wapate huduma.

Name

Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Primary Question

MHE. GEORGE M. LUBELEJE aliuliza:- Serikali ilikwishaanza kujenga vituo vya afya katika vijiji vya Mima na Mbori na ujenzi huo umesimama kutokana na ukosefu wa fedha. Je, Serikali ina mpango gani wa kukamilisha ujenzi wa vituo hivyo ili wananchi wa maeneo hayo wapate huduma za afya?

Supplementary Question 2

MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, Kituo cha Afya cha Karema ni kituo ambacho kimekamilishwa ujenzi na Serikali lakini tatizo kituo hicho hakina umeme ili kiweze kufanya kazi. Je, ni lini Serikali itatoa fedha za kukamilisha kituo hicho ili kiweze kuwahudumia wananchi wa Tarafa ya Karema?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kakoso, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kabisa Jimbo la Mpanda hadi sasa linapata umeme kwa kutumia mafuta kitu ambacho ni gharama kubwa sana. Hata hivyo, tumeshakaa na Mheshimiwa Kakoso, tumeainisha vijiji vyote vya Mpanda na Katavi, vijiji vyote vya eneo lake pamoja na hospitali na maeneo mengine yatapata umeme kuanzia Julai, 2016.

Name

Catherine Valentine Magige

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GEORGE M. LUBELEJE aliuliza:- Serikali ilikwishaanza kujenga vituo vya afya katika vijiji vya Mima na Mbori na ujenzi huo umesimama kutokana na ukosefu wa fedha. Je, Serikali ina mpango gani wa kukamilisha ujenzi wa vituo hivyo ili wananchi wa maeneo hayo wapate huduma za afya?

Supplementary Question 3

MHE. CATHERINE V. MAGIGE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Kwa kuwa hospitali inayotegemewa na wananchi wa Loliondo, Mkoani Arusha ni Hospitali ya Misheni ya Waso ingawa hospitali hii ina changamoto nyingi sana; na kwa kuwa hatuna Hospitali ya Wilaya ya Ngorongoro, Serikali haioni sasa ni wakati muafaka wa kujenga Hospitali ya Wilaya ili wakazi wa maeneo yale wapate huduma ya matibabu ipasavyo maana wakazi wengi wa maeneo yale ni wafugaji?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nichukue ombi hili kutoka kwa Mheshimiwa Catherine Magige kwamba Ngorongoro ijengwe Hospitali ya Wilaya na nikitambua kwamba katika maeneo haya kuna changamoto kubwa sana. Juzi juzi nilikuwa na Mbunge wa eneo hilo akishirikiana na wananchi wake na Madiwani ambapo walikuja ofisini kwangu kuelezea changamoto zinazowakabili wananchi wa maeneo hayo.
Kwa hiyo, jambo kubwa kama nilivyosema katika miradi kama hii, naomba Mheshimiwa Mbunge kwa sababu yeye ni wa mkoa mzima ashirikiane na Mbunge wa Jimbo na najua ni mpambanaji mkubwa sana katika sekta ya afya, wafanye mchakato mpana wa kuliibua vizuri jambo hili ili badala ya kutumia Hospitali ya DDH ambayo ni ya Misheni tuhakikishe wananchi tunawapatia Hospitali yao ya Wilaya ili mradi na wao waweze kunufaika na huduma ya afya katika nchi yao.

Name

Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Primary Question

MHE. GEORGE M. LUBELEJE aliuliza:- Serikali ilikwishaanza kujenga vituo vya afya katika vijiji vya Mima na Mbori na ujenzi huo umesimama kutokana na ukosefu wa fedha. Je, Serikali ina mpango gani wa kukamilisha ujenzi wa vituo hivyo ili wananchi wa maeneo hayo wapate huduma za afya?

Supplementary Question 4

MHE. SHABANI O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kuniona. Kwa kuwa Wilaya ya Lushoto ina majimbo matatu na Hospitali ya Wilaya ni moja. Je, ni lini sasa Serikali itapanua hospitali ile hasa wodi ya akinamama wajawazito?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nikiri kwamba si chini ya wiki tatu au nne Mheshimiwa Shekilindi na Mheshimiwa Shangazi walikuja ofisini kwangu. Lengo la kuja ofisini kwangu ilikuwa ni ajenda ya barabara halikadhalika huduma ya afya katika maeneo yao. Licha ya ajenda ya kuhakikisha tunapanua hospitali ile lakini miongoni mwa ajenda walizokujanazo ni kuimarisha vile vituo vyao vya afya viweze kufanya kazi vizuri. Kwa hiyo, kama nilivyomuahidi Mheshimiwa Shekilindi alivyokuja ofisini, jukumu letu kubwa ni kubainisha na aliniambia nipite route tofauti nione jiografia ya eneo lake, nikija naomba anipitishe niione vizuri lakini tupange mikakati ya pamoja kuwasaidia wananchi wetu.

WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri wa TAMISEMI, napenda kuongeza majibu kwenye swali la Mheshimiwa Shekilindi, Mbunge wa Lushoto kwamba katika sera ya afya sasa hivi tunataka kuondoka kwenye Hospitali ya Wilaya twende kwenye Hospitali za Halmashauri.
Kwa hiyo, nataka kuwahakikishia Waheshimiwa Wabunge wote ambao Wilaya zao zina Halmashauri zaidi ya mbili, tatu, sasa hivi kisera tunapendekeza kila Halmashauri iwe na hospitali yake badala ya kuwa na Hospitali ya Wilaya. Kwa kufanya hivi tunaamini tutaweza kutatua mlundikano wa wagonjwa katika hospitali mbalimbali za Wilaya.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, tutatoa maelekezo rasmi ya kisera katika Halmashauri mbalimbali.