Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ally Mohamed Keissy

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. ALLY K. MOHAMED (K.n.y. MHE. AIDA J. KHENANI) aliuliza:- Kumekuwa na hali ya ukiukwaji wa haki za binadamu unaofanywa na mgambo na askari polisi wanapotekeleza maagizo ya Serikali dhidi ya wafanyabiashara wadogo wadogo hususan mama lishe, bodaboda pamoja na machinga. Je, Serikali inatoa tamko gani juu ya hali hiyo?

Supplementary Question 1

MHE. ALLY K. MOHAMED: Mheshimiwa Naibu Spika, Asante sana. Pamoja
na jibu zuri la Naibu Waziri. Sasa lini Serikali itatoa kero kwa hizi kodi ndogo
ndogo za akina mama hasa wakinamama wauza vitumbua, wauza mchicha,
wauza dagaa, wauza nyanya ili kutoa kero kwa wananchi wetu wasiendelee
kudhulumiwa na kuteswa na hawa wakusanya kodi na hawa Wanamgambo,
imekuwa kero na Serikali kila mara ilitangaza hapa kwamba kodi ndogondogo
hizi ni kero lini Serikali itatangaza Halmashauri zote ziache mara moja kutoza
akina mama kwenye masoko madogo madogo?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, tukifanya rejea wakati wa kampeni ya uchaguzi ya mwaka 2015. Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akijinadi kwa wananchi ni suala zima la mchakato wa kuondoa hizi kero ndogo ndogo. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli Mheshimiwa Keissy, nimefanya ziara katika maeneo mbalimbali hata pale maeneo ya Ilala pale katika soko letu la Ilala, soko la Feri, Sokola Pugu Kajungeni na maeneo mbalimbali, soko la Mwanjelwa kule Mbeya. Hizi ni miongoni kwa concern lakini siyo hivyo utakuta mtu wa kawaida analipishwa risiti isiyokuwa sawasawa ndio maana tumezielekeza Halmashauri zote. Sambamba na hilo tukaona sasa lazima tubainishe ipi ni kero ambayo itaweza sasa ikashughulikiwa vizuri.
Mheshimiwa Naibu Spika, ndio maana sasa kwa mujibu wa utaratibu wetu tumeandaa sheria sasa inakuja hapa Bungeni, ambayo sheria ile itaainisha sasa sheria ambayo marekebisho ya Sheria ya Mambo ya Tozo na Ushuru Sura ya namba 290 itakuja hapa na sisi Wabunge wote tutashiriki, na nina imani kwamba Mungu akijalia huenda Mkutano ujao wa Bunge inawezekana sheria hiyo itaweza kufika mara baada ya wadau wakishashiriki vya kutosha.
Mheshimiwa Naibu Spika, tunaziagiza Halmashauri zote kwamba yale mambo ambayo unaona kwamba hili ni kero, kwa sababu hili suala Mameya wote, Wenyeviti wa Halmashauri wanajua kwamba sehemu hizo wamepewa kura na wananchi wao. Jambo ambalo naona kwamba jambo hili halina tija kwa wananchi wetu wa kawaida, naomba tulifanyie kazi, lakini jambo ambalo mmeona mmeliweka kwa mujibu wa sheria basi mlisamize kwa utaratibu bora, siyo kwenda kutoa kapu la mama anauza vitunguu barabarani au anauza nyanya barabarani hilo jambo litakuwa siyo sawasawa.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nazielekeza Halmashauri zote hasa Mameya na Wenyeviti wa Halmashauri waweze kukaa pamoja na Kamati zao za Fedha, wabainishe ipi ni kero kwa sasa kabla sheria hii haijakuja hapa Bungeni ili mradi kuweza kuondoa kero kuwafurahisha wananchi waishi katika maisha ya utaratibu wa kujenga uchumi wa nchi yao.

Name

Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Primary Question

MHE. ALLY K. MOHAMED (K.n.y. MHE. AIDA J. KHENANI) aliuliza:- Kumekuwa na hali ya ukiukwaji wa haki za binadamu unaofanywa na mgambo na askari polisi wanapotekeleza maagizo ya Serikali dhidi ya wafanyabiashara wadogo wadogo hususan mama lishe, bodaboda pamoja na machinga. Je, Serikali inatoa tamko gani juu ya hali hiyo?

Supplementary Question 2

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kupata nafasi hii, kwa kuwa Halmashauri ya Mji wa Mafinga na maeneo mengi ya mijini kumekuwa na kero kubwa kama hii ambayo imeelezwa kwenye swali la msingi iikiwa ni pamoja na timua timua ya wafanyabiashara ndogo ndogo. Sasa kwa kuwa Halmashauri ya Mji wa Mafinga ni Halmashauri mpya bado haijakuwa na uwezo wa kutenga maeneo kwa maana ya kwamba kifedha, kwa ajili ya wafanyabiashara ndogo ndogo. Je, Serikali iko tayari kutusaidia sisi kama Halmashauri mpya japo kusudi kutuwezesha kutenga maeneo hayo na hivyo wafanyabiashara kuwapunguzia bugudha bugudha wamama wauza vitumbua, wauza matunda, vijana wachoma mahindi na wote wanaofanya shughuli za namna hiyo? Ahsante.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, si muda mrefu nilifika pale Mafinga nilifika Jimboni kwake Mheshimiwa na nilienda mpaka katika kituo kile cha watoto walemavu pale, lakini kwa maelekezo ya Mheshimiwa Mbunge mwenyewe. Ni kweli Halmashauri ile ni mpya, naomba niseme sisi tutakupa ushirikiano mkubwa kama Serikali kama Ofisi ya Rais, TAMISEMI. Lakini suala zima la utengaji wa eneo naomba niwasihi Waheshimiwa Wabunge jambo hili linaanza kwetu sisi wenyewe, kwa sababu sisi ndio tunajua wapi eneo la wazi lipo nini kifanyike.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini vile vile atuelekezi watu waende wakapange biashara katika maeneo ya barabara, hilo jambo halikubaliki. Kwa hiyo, naomba nikusihi Mheshimiwa Mbunge ninyi pale kama Baraza la Madiwani naomba anzeni, kwa sababu mnanza kufanya mambo mazuri zaidi. Na sisi Ofisi ya Rais – TAMISEMI tutashauri vizuri nini kifanyike ili mradi wananchi wa Mafinga pale wapate huduma bora hasa ya suala zima ya ujasiriamali kufanya biashara katika maeneo yao.

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze Naibu Waziri kwa majibu mazuri sana, hata hivyo kwa namna kero ya askari hawa mgambo walioajiriwa na mamlaka zetu za Serikali za Mitaa na hasa za Mijini ni kero kubwa na inaleta usumbufu mkubwa na miongoni mwa mambo ambayo husababisha na pengine kupelekea hata Serikali kuchukiwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, sekta yetu binafsi nchini haijarasimishwa sana na kwa hivyo wananchi wetu wanahangaika kufanya shughuli mbalimbali ili wapate kipato na kwa hakika ndio wanaojenga uchumi wa nchi yetu. Lazima tuwe na staha katika kushughulika nao, maana hata hivyo hatujaweza kuwatengea maeneo ya kufanyia shughuli zao rasmi lakini hatuna mfumo rasmi sana wa mitaji na kwa hivyo kitendo cha askari mgambo kuvuruga biashara zao, kukamata na kutaifisha mali zao kitendo hiki hakikubaliki na Serikali kabisa. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nichukue nafasi hii kuziomba mamlaka zote na hasa za Mijini zinazounda majeshi haya kwa maana ya mgambo chini ya Sheria ile ya Jeshi la Akiba linalosaidiana na Polisi, kuhakikisha kwamba kila operation wanayoifanya basi inakuwa na makubaliano maalum katika mamlaka husika kwanza. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, na baada ya pale operation yeyote inayofanyika, lazima isimamiwe vizuri, haiwezekani mgambo wa Jiji wakawa wanakamata pikipiki, wanakamata bodaboda, wanakamata yaani ni vurugu tupu. Kwa hiyo, hili jambo halikubaliki nafahamu na nafikiri iko haja tukafanya mapitio ya Jeshi la Mgambo ambalo linaundwa kwenye hizi Mamlaka za Mijini na kuona kama kuna haja ya kuja na mwongozo na utaratibu mpya pamoja na kwamba tunafahamu kwamba iko sheria hili jambo hili liweze kukomeshwa kwa sababu wanaleta mateso na vilio vingi katika familia ambazo zinataifishiwa mali zao.

Name

Venance Methusalah Mwamoto

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. ALLY K. MOHAMED (K.n.y. MHE. AIDA J. KHENANI) aliuliza:- Kumekuwa na hali ya ukiukwaji wa haki za binadamu unaofanywa na mgambo na askari polisi wanapotekeleza maagizo ya Serikali dhidi ya wafanyabiashara wadogo wadogo hususan mama lishe, bodaboda pamoja na machinga. Je, Serikali inatoa tamko gani juu ya hali hiyo?

Supplementary Question 3

MHE. VENANCE M. MWAMOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri ningependa niulize swali langu moja.
Kwa kuwa fedha ambazo zinatolewa kwa hawa akina mama lishe na kufanya biashara ni fedha za Serikali ambao walio wengi zinatoka TASAF, ni fedha za kuondo umasikini. Na kwa kuwa sasa Watendaji wengi sana wa Vijiji hawajaajiriwa kwa hiyo wanafanya zile kazi kama kukomoa. Je, sasa Serikali inasemaje kuhusu hilo?

Name

George Boniface Simbachawene

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibakwe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba maeneo mengi vijijini Watendaji wa Vijiji na hata wa Kata, hawajaajiriwa kwa ajira rasmi na Halmashauri husika, na hii inapelekea utekelezaji wa shughuli za maendeleo ikiwa ni pamoja na uwajibikaji kuwa katika kiwango cha chini kwa sababu mtu anaona mimi sijaajiriwa kwa hiyo nikifanya lolote lile ni sawa tu.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini tumekubaliana na tulipitisha hapa utaratibu kuanzia mwaka jana, tumeruhusu kwamba kada fulani za chini zinaweza zikatolewa ajira hizo na mamlaka husika kutegemeana tu bajeti zao walizozitenga. Nitoe rai kwa Halmashauri zote nchini kuhakikisha kwamba zinatoa ajira za Watendaji wa Vijiji ambao kwa sifa na kwa utaratibu tulioweka wanaruhusiwa kuzitoa wao ili waweze kuwa wamekamilisha idadi ya vijiji na watendaji wote wakamilike wale walioajiriwa na Serikali itakuwa tayari kupokea isipokuwa tu wazingatie sifa zao.
Mheshimiwa Naibu Spika, tunavyo vyuo ambavyo vinatoa watu waliosomea masuala ya mamlaka ya Serikali za Mitaa na mifumo ya Serikali za Mitaa Tanzania, Chuo cha Hombolo ambacho kina wataalam wazuri sana tunacho Chuo cha Mipango, Dodoma ambacho nao wamefundishwa masuala haya ya mipango vijijini ni vizuri watu wanaoajiriwa wakawa wanatoka kwenye vyuo hivi.