Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 35 Good Governance Ofisi ya Rais TAMISEMI. 284 2016-06-02

Name

Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. ALLY K. MOHAMED (K.n.y. MHE. AIDA J. KHENANI) aliuliza:-
Kumekuwa na hali ya ukiukwaji wa haki za binadamu unaofanywa na
mgambo na askari polisi wanapotekeleza maagizo ya Serikali dhidi ya wafanyabiashara wadogo wadogo hususan mama lishe, bodaboda pamoja na machinga. Je, Serikali inatoa tamko gani juu ya hali hiyo?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais,
TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Aida Joseph Khenani, Mbunge
wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, mgambo wanafanya kazi kwa mujibu wa sheria
ya polisi wasaidizi ya mwaka 1969 kwa kuzingatia sheria hiyo, Halmashauri
zimeruhusiwa kuajiri askari ngambo kwa ajili ya kusaidia usimamizi wa Sheria
Ndogondogo za Halmashauri za Majiji, Manispaa, Miji na Wilaya.
Mheshimiwa Naibu Spika, askari mgambo anayefanya kazi katika
Halmashauri anawajibika kuzingatia sheria za nchi pamoja na sheria ndogo
ndogo zilizotungwa na Halmashauri. Jukumu lao kubwa ni kulinda mali za
umma, kulinda usalama wa wananchi pamoja na kutekeleza maelekezo
yatakayotolewa na Halmashauri kwa wakati wowote.
Mheshimiwa Naibu Spika, mgambo hawaruhusiwi kwa mujibu wa sheria
kuchukua au kuharibu mali za wananchi. Kufanya hivyo ni ukiukwaji wa sheria
za Serikali, na Serikali haitasita kuchuakua hatua kwa vitendo hivyo. Aidha,
naomba kutumia fursa hii kuzikumbusha Halmashauri zote kutenga maeneo
maalum kwa ajili ya wafanyabiashara wadogo ili biashara hizo zifanyike katika
maeneo yaliyotengwa rasmi na kuacha kufanya shughuli hizo katika hifadhi za
barabara na maeneo mengine yasiyoruhusiwa.