Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Nicodemas Henry Maganga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbogwe

Primary Question

MHE. NICODEMAS H. MAGANGA aliuliza:- Je, Serikali inachukua hatua gani kwa Watumishi wanaohusika kutumia vibaya fedha za miradi ya Serikali?

Supplementary Question 1

MHE. NICODEMAS H. MAGANGA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Kwanza nimesikia majibu ya Naibu Waziri, niseme kwamba sijaridhishwa. Nataka kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, pamoja na kwamba watumishi elfu mbili na kitu wame…..

SPIKA: Mheshimiwa Maganga subiri kidogo. Hujaridhishwa kwa maana ya kwamba jibu la Mheshimiwa Waziri halijajibu swali lako…

MHE. NICODEMAS H. MAGANGA: Mheshimiwa Spika, ndio maana nataka niulize maswali mawili…

SPIKA: Maana kazi yangu ni kusimamia kanuni hapa mbele ili kama unaona swali lako halijajibiwa kikamilifu, huwezi kuuliza maswali ya msingi, maana yake jibu halipo.

MHE. NICODEMAS H. MAGANGA: Mheshimiwa Spika, hapana, nipe nafasi niulize maswali mawili, labda nitapata majibu. (Kicheko)

SPIKA: Sasa inabidi uwe umeridhika na hayo majibu ndiyo uulize, kwamba haya majibu yaliyoko hapa, lakini bado una maswali ya nyongeza. Kwa hiyo, endelea Mheshimiwa, nimeelewa kwamba umeridhika na majibu sasa unataka kuuliza maswali yako ya msingi. (Makofi)

MHE. NICODEMAS H. MAGANGA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kumwuliza Mheshimiwa Naibu Waziri kwamba pamoja na watumishi elfu mbili na kitu hao waliobainika, nataka kujua, wangapi ambao wamefungwa kwa ajili ya makosa ya kutuhujumu wananchi pamoja na Mheshimiwa Rais anatafuta pesa anapeleka kwenye miradi ya maendeleo? Nawe ni shahidi, umesema kwamba watu elfu mbili na kitu walibainika; wangapi walioko magerezani mpaka sasa?

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili. Serikali ya Awamu ya Tano ilitangaza kwamba itatengeneza Magereza ya Mafisadi ambao wanabainika ili wasiende moja kwa moja Mahakamani, wakae kwenye lockup za Mahakama ya mafisadi? Je, hamuoni sasa ni wakati muafaka?

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Spika, swali la kwanza lililoulizwa na Mheshimiwa Mbunge la kutaka kujua wangapi wapo magerezani; naomba nisiwe muongo mbele ya Bunge lako naomba nijiridhishe juu ya idadi kamili ili niweze kuja kumwambia Mheshimiwa Mbunge na Bunge lako.

Mheshimiwa Spika, swali la pili juu ya utekelezaji wa magereza maalum kwa ajili ya hawa wanaohujumu uchumi wetu, nadhani jambo hili linategemea zaidi upatikanaji wa fedha ili kuweza kutekeleza azma hiyo ya viongozi wetu kama ambavyo iliahidiwa na Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kuwa atatekeleza yale yote ya walitangulia kabla yake na ya kwake yeye ni kuandaa Tanzania anayoitaka, ahsante sana.

Name

Josephine Johnson Genzabuke

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NICODEMAS H. MAGANGA aliuliza:- Je, Serikali inachukua hatua gani kwa Watumishi wanaohusika kutumia vibaya fedha za miradi ya Serikali?

Supplementary Question 2

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Spika, ahsante. Tunafahamu kwamba Baraza la Madiwani ni mamlaka ya nidhamu kwa watumishi ngazi ya halmashauri. Je, Mkurugenzi ana mamlaka ya kutengua maamuzi ya Baraza la Madiwani pale wanapobaini kwamba watumishi wamefanya makosa?

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa Sheria ya Serikali za Mitaa, maamuzi ya Baraza la Madiwani hayapingwi na mtu yeyote na maamuzi hayo ni maamuzi yaliyokamilika ikiwa yamefuata taratibu na kama kuna mtu yeyote ambaye hatoridhika na maamuzi hayo, basi taratibu za kisheria zimewekwa wazi ili kuweza kutengua maamuzi hayo na siyo Mkurugenzi kujipa mamlaka juu ya maamuzi yanayofanya na Baraza la Madiwani. (Makofi)

SPIKA: Mheshimiwa Amina. Mheshimiwa Waziri wa Nchi.

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Spika, ni mpongeze Naibu Waziri kwa majibu mazuri lakini niongezee kwenye jibu alilolitoa kwa Mheshimiwa Genzabuke. Kamati ya Halmashauri inapojigeuza kuwa Kamati ya Nidhamu, Katibu wake ni Mkurugenzi na Wajumbe ni wale Madiwani. Sasa haiwezekani Katibu na ile Kamati wamefanya maamuzi halafu Katibu akaenda akageuza. Kama kulikuwa kuna mabadiliko hayo basi angepaswa kurudi tena kwenye Kamati ile ile ili aweze kugeuza. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, tutajaribu kulichukua kwa kushirikiana na TAMISEMI, tulifuatilie tuone kilichotokea hasa ni kitu gani, ahsante sana. (Makofi)