Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jackson Gedion Kiswaga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalenga

Primary Question

MHE. JACKSON G. KISWAGA aliuliza: - Je, lini Serikali itapeleka huduma ya mawasiliano ya simu Kata ya Masaka – Kalenga?

Supplementary Question 1

MHE. JACKSON G. KISWAGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naishukuru sana Serikali kwa kuwahakikishia wananchi wa Masaka kwamba sasa unapeleka mawasiliano. Pamoja na majibu mazuri, nina swali moja la nyongeza. Kwa kuwa Jimbo la Kalenga lilipewa minara kumi: Je, hizo Kata nyingine za Kihanga pamoja na Ulanda nazo zitajengwa kwa pamoja? Ahsante sana.

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Jackson, Mbunge wa Kalenga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama ambavyo nimetoa ufafanuzi, miradi yote ambayo imeshaainishwa katika Mradi wa Tanzania ya Kidigitali upo katika hatua ambazo nimemaliza kuzielezea na tuwe na subira Waheshimiwa Wabunge. Naamini kabisa kwamba, hatua zote ambazo ni za ndani zikishakamilika, sasa tukishahamia site na niwahakikishie Waheshimiwa Wabunge kusimamisha ile passive structure haimalizi hata wiki tatu na ukija kuhakikisha kwamba unafunga zile active equipment haimalizi hata wiki moja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, tukishamaliza process za ndani hizi, tukahamia site nina uhakika ndani ya mwezi mmoja au miwili minara hiyo itakuwa inakamilika katika kila eneo ambalo tutakuwa tunapeleka huduma ya mawasiliano, ahsante.

Name

Elibariki Emmanuel Kingu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Magharibi

Primary Question

MHE. JACKSON G. KISWAGA aliuliza: - Je, lini Serikali itapeleka huduma ya mawasiliano ya simu Kata ya Masaka – Kalenga?

Supplementary Question 2

MHE. ELIBARIKI I. KINGU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kuniona. Nilikuwa nataka niulize swali la nyongeza. Ni lini Serikali itakwenda kutatua changamoto ya upatikanaji wa mawasiliano kwa wananchi wa Kata ya Igombwe pamoja na Ihanja ambapo kuna minara inasuasua sana ikizingatiwa kwamba Kata ya Igombwe ndiyo Kata inayochangia kwa kiwango kikubwa pato la Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Elibariki Kingu, Mbunge kuhusiana na changamoto ya Kata ya Igombwe pamoja na Ihanja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu minara tayari imejengwa, ipo. Changamoto ni kwamba Mheshimiwa Mbunge, amesema inasuasua. Tutawaelekeza TCRA kwa sababu kwa mujibu wa sheria, wao wana dhamana ya kuhakikisha kwamba watoa huduma wote wanazingatia quality of service. Kwa hiyo, tutahakikisha tunawatuma watalamu wetu wakajiridhishe, tatizo liko wapi? Kama mnara umezidiwa, basi tujue kwamba tunaongeza nguvu na kama mnara una changamoto ya kiufundi, basi wachukue hatua kuhakikisha kwamba wananchi wa Igombwe na Ihanja ambao ni wananchi wa Mheshimiwa Kingu na Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan wanapata huduma ya mawasiliano. (Makofi)

Name

Dr. Pius Stephen Chaya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Mashariki

Primary Question

MHE. JACKSON G. KISWAGA aliuliza: - Je, lini Serikali itapeleka huduma ya mawasiliano ya simu Kata ya Masaka – Kalenga?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa hii nafasi. Kwa kuwa Naibu Waziri amesema upembuzi yakinifu wa ujenzi wa minara umeshafanyika na katika Kata ya Iseke tayari walishafika: Je, ni lini sasa ujenzi wa mnara wa mawasiliano utaanza katika Kata ya Iseke? Ahsante.

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Dkt. Chaya, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Kata ya Iseke kama ambavyo nimejibu katika majibu mengine ni kwamba, vifaa vikishaingia nchini na hatua za kiufundi na za kiutaratibu na za kisheria zikishakamilika, tutahakikisha kwamba Kata ya Iseke tunaanza ujenzi mara moja na kuhakikisha kwamba Wananchi wa maeneo hayo wanaendelea kufurahia matunda ya nchi yao, ahsante sana.

Name

Stella Simon Fiyao

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JACKSON G. KISWAGA aliuliza: - Je, lini Serikali itapeleka huduma ya mawasiliano ya simu Kata ya Masaka – Kalenga?

Supplementary Question 4

MHE. STELLA S. FIYAO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Kata ya Mlowo ni Kata ambayo iko katikati ya Mji ndani ya Wilaya Mbozi, lakini kuna baadhi ya maeneo kumekuwa na changamoto kubwa ya mawaliano ikiwepo eneo la Saganoti na maeneo mengine ya Forest. Serikali ina mkakati gani wa kurekebisha mawasiliano katika maeneo haya? (Makofi)

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Stella, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti ni dhamira ya Serikali ya Chama Cha Mapinduzi kupitia utekelekezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi kuhakikisha Watanzania wote wanapata huduma ya mawasiliano. Kwa sababu hiyo, mkakati wa Serikali ni kuhakikisha kwamba tunajiridhisha kila sehemu ambayo ina changamoto ya mawasiliano, basi tunafika na kuchukua hatua stahiki ili Watanzania wote waweze kupata.

Mheshimiwa Mwenyekiti, namwomba Mheshimiwa Stella, baada ya Bunge hili tuweze kuwasiliana ili tuweze kuchukua taarifa kamili kuhusiana na maeneo husika ili sasa tutume watalamu wetu wakajiridhishe ni nini kikafanyike katika eneo hilo ili kuhakikisha kwamba tunatatua changamoto ya mawasiliano, ahsante.

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JACKSON G. KISWAGA aliuliza: - Je, lini Serikali itapeleka huduma ya mawasiliano ya simu Kata ya Masaka – Kalenga?

Supplementary Question 5

MHE. DKT. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi niulize swali dogo la nyongeza. Je, ni lini Serikali itapeleka mawasiliano katika Kata ya Masisiwe katika Wilaya ya Kilolo? Kwa sababu wananchi wamekuwa wakipata mateso makubwa sana, hawana mawasiliano kwa muda mrefu sana.

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Ritta Kabati, Mbunge wa Iringa kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyeki, hii Kata ya Masisiwe Mheshimiwa Mbunge alishaiongea zaidi ya mara tatu mwaka 2022. Baada ya kuongea, tukaiingiza kwenye utekelezaji wa mradi wa Tanzania ya Kidigitali na sasa tunasubiri katika hatua mbalimbali za utekelezaji zikishakamilika Kata ya Masisiwe itapata mawasiliano, ahsante sana.

Name

Jonas William Mbunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Mjini

Primary Question

MHE. JACKSON G. KISWAGA aliuliza: - Je, lini Serikali itapeleka huduma ya mawasiliano ya simu Kata ya Masaka – Kalenga?

Supplementary Question 6

MHE. JONAS W. MBUNDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kata ya Kikolo katika Jimbo la Mbinga Mjini ina changamoto kubwa sana ya mawasiliano: Ni lini Serikali itapeleka huduma hiyo?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunda, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nilipokee na nilichukue kama changamoto ambayo tutaenda kuifanyia kazi, ahsante.