Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mwantum Dau Haji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MWANTUMU DAU HAJI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani kupunguza msongamano wa malori barabarani?

Supplementary Question 1

MHE. MWANTUMU DAU HAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwanza kabisa nimshukuru Waziri kwa majibu yake mazuri aliyoyatoa sasa hivi.

Je, Serikali inasema nini katika kufuatilia utendaji katika mizani ili kupunguza msongamano wa malori barabarani?

Swali la pili, nini mkakati wa muda mrefu wa upanuzi wa barabara kiwango cha njia, hasa barabara kuu ziingiazo nchini? Ahsante.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema kwenye jibu langu la msingi, kwamba moja ya maeneo ambayo yameonekana yanakuwa na msongamano mkubwa ni kwenye mizani. Utaratibu ambao sasa tumeanza kuufanya, kwanza ni kubadilisha mizani ile ambayo ilikuwa siyo ya kieletroniki ambayo inatakiwa gari lisimame ndiyo lipime. Sasa tunatumia mizani ambayo tunasema weigh in motion yaani gari linakuwa linatembea huku linapima, kwa hiyo litumia muda mfupi sana, ikiwa ni pamoja na kuweka mizani pande zote mbili. Kwa hiyo, kwa kufanya hivyo kwenye mizani hiyo kumepunguza sana changamoto ya msongamano.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu mpango wa kuzipanua barabara kwenye mipaka yetu ama njia zinazoingia nchini, ziko barabara hasa kwenye vituo vyetu vya forodha vikubwa kama Tunduma, ambako sasa hivi tunafikiria namna ya kuongeza njia kutoka njia mbili kwenda njia nne ili kupunguza msongamano katika maeneo hayo. Ndiyo maana katika mradi wa sasa ambao unakwenda kwa mfano mpaka wa Tunduma, barabara inayojengwa ni ya njia nne. Ahsante.

Name

Deodatus Philip Mwanyika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Primary Question

MHE. MWANTUMU DAU HAJI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani kupunguza msongamano wa malori barabarani?

Supplementary Question 2

MHE. DEODATUS P. MWANYIKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.

Je, ni lini barabara ya mchepuo katika Mji wa Njombe kutoka Kibena kwenda mpaka maeneo ya Kobe itaanza kujengwa kuondoa adha ya malori?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Sasa hivi kilichofanyika katika Mji wa Njombe ambao Mji unakua kwa kasi sana, wameshafanya usanifu wa awali kabisa (reconnaissance survey) ili kuona namna wapi barabara ya mchepuko itapita katika Mji wa Njombe. Kwa hiyo mipango hiyo ipo kinachofatia sasa hivi ni kutafuta fedha kukamilisha huo usanifu. Ahsante.

Name

Shally Josepha Raymond

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MWANTUMU DAU HAJI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani kupunguza msongamano wa malori barabarani?

Supplementary Question 3

MHE. SHALLY J. RAYMOND: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kuniona. Niipongeze Serikali kwa kutenganisha Wizara ya Ujenzi na Wizara ya Uchukuzi.

Kwa kuwa, vyombo vya usafiri barabarani vimeongezeka, ukianzia baiskeli, bajaji, bodaboda, magari madogo mpaka malori lakini barabara hizo zimebakia ni zile zile mbili. Nikifatilia majibu ya msingi ya Mheshimiwa Waziri amezitaja zote kwamba zitapanuliwa lakini mimi nauliza kabisa, ni lini haswa Barabara ya kutoka Dar es Salaam mpaka Arusha - Namanga na inayokwenda mpaka Cape Town itapanuliwa ili basi ianzie hapo tuende ile ya Dar - Mbeya, Dar - Lindi, Dar – Mwanza, Dodoma - Arusha?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunakiri kwamba barabara nyingi ambazo tulijenga zamani, zilijengwa kulingana na mahitaji ya wakati huo na lazima tukiri kwamba tunapoona magari mengi yameongezeka maana yake uchumi wetu, umezidi kukua na ndiyo maana tunaona magari makubwa na malori makubwa. Kwa hiyo, sasa hivi tunachofanya hizi barabara zote tunapotakiwa kuzipanua ni kwamba ni lazima tufanye usanifu upya, halafu tuzijenge kwa kiwango cha sasa. Kwa hiyo Serikali imeliona hilo ikiwa ni pamoja na barabara hiyo ya kutoka Chalinze kwenda Mombo hadi Moshi. Kwa hiyo, tayari zimeainishwa, kinachotegemewa sasa ni kutafuta fedha ili kuanza kuzitengeneza hizo barabara mpya kwa kiwango cha sasa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ndiyo maana hata sasa barabara tunazozijenga upana wake ni tofauti kabisa na upana wa barabara zile zilizojengwa zamani ikiwepo barabara aliyoitaja Mheshimiwa Mbunge., Ahsante sana.

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Primary Question

MHE. MWANTUMU DAU HAJI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani kupunguza msongamano wa malori barabarani?

Supplementary Question 4

MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushuru kwa kunipa nafasi.

Kwa kuwa, msongamano uliopo Mji wa Tunduma ni mkubwa sana na katika hali ya kawaida upanuzi wake utakuwa gharama kubwa sana, bahati nzuri Mheshimiwa Naibu Waziri alipita akaona uwezekano wa kujenga barabara kiwango cha lami kuanzia Laela kwenda kuunganisha ile barabara kwenda Kasesha.
Je, nini mpango wa Serikali katika kuondoa msongamano huo?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza tu niwakumbushe Waheshimiwa Wabunge kwamba pamoja na mchango wa barabara kuleta msongamano Tunduma lakini kuna mambo mengine ambayo ni ya kiforodha ambayo yanasababisha msongamano katika Mji wa Tunduma ikiwa ni pamoja na wenzetu wa upande wa pili ambao hawaendani na kasi ya kwetu. Sisi tunafanya masaa 24 wao wanafanya masaa 12.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na hilo kumjibu Mheshimiwa Mbunge, ni kwamba tunafikiria kama Serikali kwanza kutengeneza bypass kutoka Mpemba kwenda kuunganisha na barabara inayokwenda Sumbawanga ili magari ambayo yanaenda njia ya Sumbawanga yasilazimike kupita Tunduma, hilo la kwanza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili ni kweli nimepita kwenye barabara aliyoisema ambayo kama tutaijenga kwa kiwango cha lami itasaidia sana magari mengi kwenda Bandari ya Kasanga ikiwa ni pamoja na mpaka wa Kasesya. Kwa hiyo, hiyo mipango ipo kinachosubiriwa tu ni Serikali itakapopata fedha kuijenga hiyo Barabara. Ahsante.

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MWANTUMU DAU HAJI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani kupunguza msongamano wa malori barabarani?

Supplementary Question 5

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiwa unatoka Kibaha unaenda Dar es Salaam kwenye njia nane, kuna Maliasili Idara ya Misitu wanakagua malighafi za misitu kwenye hiyo njia nane barabarani kabisa, kitu ambacho kinasababisha msongamano na ajali.

Ni kwa nini Serikali isiweke mchepuko kama wanavyofanya kwenye mizani waweze kuwajengea wakifika pale wanachepuka, wanakaguliwa, wanaingia kwenye highway wanaendelea, kuliko kukaguliwa kwenye high way?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba nilichukue suala hilo kwa ajili ya kulifanyia study na kuona uwezekano wa hicho alichokisema Mheshimiwa Esther Matiko Mbunge. Ahsante.(Makofi)

Name

Eric James Shigongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buchosa

Primary Question

MHE. MWANTUMU DAU HAJI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani kupunguza msongamano wa malori barabarani?

Supplementary Question 6

MHE. ERIC J. SHIGONGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kuniona.

Hivi karibuni tulisaini mkataba wa Barabara ya Sengerema - Nyehunge kwa kiwango cha lami na Mheshimiwa Naibu Waziri alikuwepo lakini imekuwa kimya. Je, tunaweza kufahamu tatizo hasa ni nini mpaka muda huu kazi hiyo haijaanza?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba nikubaliane na Mheshimiwa Mbunge Eric Shigongo, kwamba tulisaini mkataba lakini maendeleo ni madogo sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba tu nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba, tayari Mkandarasi huyo ameshaitwa na Wizara na Mheshimiwa Waziri kujua changamoto yake ni nini ili tuone taratibu za kuchukua za kimkataba kama itaonekana kwamba huyo Mkandarasi ana changamoto ili taratibu za kimkataba ziweze kuchukuliwa, ili tuone kwamba hii kazi nzuri anayoifanya Daktari Samia isikwamishwe na huyu Mkandarasi. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tumeshaliona na hatua tayari tumeshaanza kuchukua. Ahsante.