Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 7 Works and Transport Wizara ya Ujenzi 97 2023-11-07

Name

Mwantum Dau Haji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MWANTUMU DAU HAJI aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani kupunguza msongamano wa malori barabarani?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mwantumu Dau Haji, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, mipango ya Serikali na jitihada za kupunguza msongamano wa magari ikiwemo malori barabarani ni pamoja na kujenga Madaraja na Barabara za juu kwenye majiji makubwa nchini, kufanya upanuzi wa barabara kutoka njia mbili kwenda njia nne hadi nane kwa maeneo yenye msongamano mkubwa, ujenzi wa maegesho ya malori, ufungaji wa mifumo ya kielektroniki ya kupima uzito wa malori yakiwa kwenye mwendo (Weigh in Motion System – WIMS) katika vituo vya mizani na barabara za michepuo katika miji na majiji mbalimbali, ahsante.