Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ally Anyigulile Jumbe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyela

Primary Question

MHE. ALLY A. J. MLAGHILA aliuliza: - Je, lini Serikali itahakikisha mfumo wa uuzaji wa zao la Kakao unaomnufaisha mkulima badala ya wafanyabiashara wachache?

Supplementary Question 1

MHE. ALLY A. J. MLAGHILA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwa kuwa Serikali ndiyo wanaondesha mfumo huu kupitia vyama vya ushirika, na hapo awali kabla ya kuanza mfumo huu bei ya kakao ilikuwa ni shilingi 7,000 kwa kilo tukiuza kwenye kampuni za botanical; na sasa hivi mfumo huu umeingia wizi mkubwa sana ambao unaendelea mpaka sasa. Kwa sasa zao hili halimnufaishi mkulima wa Kyela mpaka Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa comrade Homera amekiri wazi kwamba mfumo huu unawanufaisha watu wachache na hela haionyeshi kwamba inaingia kwa wakulima.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mfumo huu una matatizo sana, nina maswali mawili ya nyongeza. Kwa nini Serikali inaendelea kung’ang’ania mfumo huu ambao haumnufaishi mkulima?

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, tarehe 7 mwezi wa nane, mwaka 2022 Mheshimiwa Waziri wa Viwanda na Biashara alikiri wazi kwamba mfumo huu utaondoka kwenye zao hili. Je, ni lini sasa Waziri ataenda kuwaambia wananchi wa Kyela kwamba sasa mfumo ambao utamnufaisha mkulima ni huu ambao na wao watakuwa wameujadili naye? (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Jambo la kwanza namuondoa hofu Mheshimiwa Mbunge, na ndiyo maana mnaona katika matumizi ya huu mfumo tunavozungumza sasa bei ya zao la kakao kwa kilo imefika shilingi 8,000 kwa hiyo unaona kuna maendeleo makubwa. Bahati nzuri katika mfumo huu mkulima analipwa ndani ya masaa 48 baada ya mnada kuwa umekamilika; kwa hiyo utaona kuna manufaa mengi kwenye huu mfumo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi kama Wizara ya Kilimo kwa sababu tunaendelea kupitia hii mifumo na kuangalia kama kuna changamoto basi tunapokea sehemu ya maoni ambayo Mheshimiwa Mbunge ameyatoa na tutayapitia tuone kama kuna mahali kuna changamoto ili tuweze kuirekebisha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu kueleza kwamba, ni lini mfumo huu utaondoka nafikiri baada ya mapitio ya changamoto tujue kama kweli kuna changamoto lakini jukumu letu sisi ni kuboresha na kuhakikisha mfumo huu unawasaidia wakulima nchini, ahsante.

Name

Joseph Zacharius Kamonga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ludewa

Primary Question

MHE. ALLY A. J. MLAGHILA aliuliza: - Je, lini Serikali itahakikisha mfumo wa uuzaji wa zao la Kakao unaomnufaisha mkulima badala ya wafanyabiashara wachache?

Supplementary Question 2

MHE. JOSEPH Z. KAMONGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa kunipa nafasi. Kwa kuwa Mheshimiwa Waziri alishatoa taarifa kwa Umma kwamba Serikali ya Awamu ya Sita imeshatoa fedha zote kwa ajili ya kuwalipa wakulima wa zao la mahindi kule Ludewa. Je, nini maelekezo ya Serikali kwa watu wa NFRA kuwahisha malipo hayo ili wazazi waweze kupeleka watoto vyuo na kununua mbolea? Ahsante.

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Bahati nzuri Mheshimiwa Mbunge ameeleza kwamba tuko katika hatua za mwisho kumalizia malipo kwa watu ambao wapo katika awamu ya mwisho. Kwa maelezo ambayo Mheshimiwa Waziri wa Kilimo alikuwa amenipatia, ni kwamba baada ya kumaliza huu mchakato, Serikali itarudi kwa ajili ya kuendelea kununua mazao kwa wakulima.

Mheshimiwa Mwenyekiti, maelekezo ni kwamba, kwa sababu fedha hizi ziko katika Taasisi za Kibenki, wanamalizia tu huu mchakato na naamini kabla ya mwisho wa mwezi huu wakulima wote nchini watakuwa wameshalipwa. Ahsante.

Name

Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ALLY A. J. MLAGHILA aliuliza: - Je, lini Serikali itahakikisha mfumo wa uuzaji wa zao la Kakao unaomnufaisha mkulima badala ya wafanyabiashara wachache?

Supplementary Question 3

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Licha ya mkakati wa Serikali kuruhusu minada ya kahawa, Mkoani Kagera, bado changamoto ya bei inabaki kuwa chini ukilinganisha za majirani zetu wa Uganda, hivyo kupelekea watu kutamani kuvusha kahawa. Je, ni nini mkakati wa Serikali kuhakikisha bei ya kahawa Mkoani Kagera haitofautiani sana na Uganda ili watu waweze kupata faida ya kahawa zao?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Swali la namna hii nilijibu nafikiri ndani ya siku mbili au tatu zilizopita, tukaainisha moja ya mchakato wa Serikali wa kuongeza thamani katika zao la kahawa ambao utachangia ongezeko la bei kwa sababu asilimia kubwa ya kahawa ambayo tunauza sisi ni kahawa ghafi ambayo inapelekea bei kuwa chini. Nimthibitishie kwamba mkakati wetu juu ya uwekezaji katika zao la kahawa uko palepale na tutawasaidia wakulima katika maeneo yote nchini wanayolima ikiwemo katika Mkoa wa Kagera. Kwa hiyo nimwondoe shaka Mbunge katika hili, hii kazi tunaiweza na tutaifanya. Ahsante.