Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 7 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 94 2023-11-07

Name

Ally Anyigulile Jumbe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyela

Primary Question

MHE. ALLY A. J. MLAGHILA aliuliza: -

Je, lini Serikali itahakikisha mfumo wa uuzaji wa zao la Kakao unaomnufaisha mkulima badala ya wafanyabiashara wachache?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwa niaba ya Waziri wa Kilimo, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ally Anyigulile Jumbe Mlaghila, Mbunge wa Jimbo la Kyela, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, zao la kakao huuzwa kupitia mfumo wa Stakabadhi Ghalani chini ya utaratibu wa minada inayoratibiwa na vyama vya ushirika. Mfumo huo ulianza kutumika mwaka wa fedha 2018/2019 ambapo bei ya kakao imeendelea kuimarika kulingana na mahitaji ya soko. Wastani wa bei ya kakao kwa kilo kuanzia msimu wa 2018/2019 ilikuwa shilingi 4,611; 2019/2020 ilikuwa shilingi 5,034, mwaka wa fedha 2020/2021 ilikuwa shilingi 4,818, mwaka wa fedha 2021/2022 ilikuwa shilingi 4,711 na hadi kufikia tarehe 23 Oktoba msimu wa mwaka wa fedha 2023/2024 wastani wa bei ya kakao kwa kilo ni shilingi 8,079.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inaendelea kuimarisha mifumo ya uuzaji wa mazao nchini ili kuongeza ushindani na kumnufaisha mkulima.