Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Agnes Elias Hokororo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AGNES E. HOKORORO aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kukamilisha muundo wa Wakala wa Elimu na Mafunzo ya Uvuvi?

Supplementary Question 1

MHE. AGNES E. HOKORORO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali naomba kuuliza maswali mawili madogo ya nyongeza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, baadhi ya vyuo katika taasisi hizo kama vile Mtwara–Mikindani, Kibirizi–Kigoma, Gabimori–Rorya mameneja wake wamekaimu kwa kipindi kirefu sana kuanzia miaka saba mpaka kumi na moja;

i. Je, Serikali haioni inafifisha malengo ama maelekezo ya Chama cha Mapinduzi katika vyuo hivyo kutoa mafunzo kwa sababu havina mameneja wa kudumu?

ii. Je, Serikali itakapokamilisha mchakato huo wa kujaza hizo nafasi kwa muundo uliokamilika tangu Novemba 2022, iko tayari kuwalipa mameneja hao wanaokaimu akiwemo meneja wa Mtwara-Mikindani aliyokaimu kwa miaka 11 kwa nafasi hiyo? (Makofi)

Name

Alexander Pastory Mnyeti

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Misungwi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kwanza nampongeza sana dada yangu Agnes kwa jinsi ambavyo amekuwa akifuatilia sana chuo hiki na kwa kweli kama Wizara tunatumia nafasi hii kumpongeza sana kwa jinsi ambavyo anafuatilia habari hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza, ni kweli kwamba kuna makaimu katika vyuo vingi vinavyohusiana na masuala ya uvuvi. Napenda kutumia nafasi hii kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba makaimu hao sasa watakwenda kuthibitishwa, wale wenye vigezo. Jambo hili liko kwenye upekuzi na upekuzi upo katika hatua za mwisho namhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba linakwenda kufanikiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili alilosema kuhusu mameneja waliokaimu kwa muda mrefu taratibu za kiutumishi zinafahamika. Kama watakuwa na sifa za kulipwa basi watalipwa, Serikali iko tayari kuwalipa na kama watakuwa hawana sifa za kulipwa basi hawatalipwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.