Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 7 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Waziri wa Mifugo na Uvuvi 92 2023-11-07

Name

Agnes Elias Hokororo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AGNES E. HOKORORO aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kukamilisha muundo wa Wakala wa Elimu na Mafunzo ya Uvuvi?

Name

Alexander Pastory Mnyeti

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Misungwi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI alijibuĀ¬: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mifugo na Uvuvi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Agness Elias Hokororo, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, muundo (organization Structure) wa Wakala ya Elimu na Mafunzo ya Uvuvi yaani Fisheries Education and Training Agency - FETA uliokuwa ukitumika ulipitishwa tarehe 1 Oktoba, 2018. Muundo huo ulikuwa unaendana na matakwa ya Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi yaani National Council for Technical and Vocational Education and Training - NACTVET, ambalo ndio linaratibu vyuo vya ufundi stadi ikiwemo FETA.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kutokana na changamoto ya vyuo vinavyoratibiwa na NACTVET kuwa na miundo isiyofanana, NACTVET walihuisha miundo ya vyuo wanavyo viratibu ili kuongeza tija katika utoaji elimu na pia kupunguza gharama za uendeshaji. Hivyo, kufuatia uhuishaji huo wa NACTVET, muundo mpya wa FETA uliidhinishwa Novemba, 2022 na kwa sasa Serikali inaendelea na taratibu za kujaza nafasi za uongozi katika muundo huo mpya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.