Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Josephine Johnson Genzabuke

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza:- Je, lini Halmashauri ya Mji wa Kasulu itaondokana na matumizi ya maji machafu kutokana na ukosefu wa chujio?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, nashukuru kwa majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri.

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri lakini nina maswali mawili ya nyongeza; kwanza nishukuru Serikali kwa kuweka Mji wa Kasulu kati ya miji 28 itakayonufaika na mpango wa maji.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza kwa wakati huu ambapo kuna mlipuko wa kipindupindu je, Serikali ina mpango upi wa dharura wa kuweza kuwasaidia wananchi wa Kasulu ili kuondokana na tatizo la maji machafu?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili katika Halmashauri ya Kasulu DC zipo kata ambazo tayari zimeshachimba visima lakini maji hayajasambazwa kutokana na ukosefu wa miundombinu ya mabomba. Kata hizo ni Kata ya Kasangezi, Lusesa, Hurugongo na Shunguliba. Ni lini Serikali itamaliza matatizo hayo katika kata hizo nilizozitaja? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Genzabuke kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza tupokee pongezi zako na tumshukuru Mheshimiwa Rais ambaye ameweza kupigania huu mradi wa miji 28 sasa tayari unatekelezwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusiana na mlipuko wa kipindupindu Mheshimiwa Genzabuke sisi kama Wizara tuko imara sana kuona kwamba kama chujio halipo lakini tunatibu maji kwa kutumia chlorine hatutoi maji bila kuyatibu. Kwa hiyo, huenda maji yakawa na tope kidogo lakini yametibiwa na chlorine. Kwa hiyo, vidudu vinakuwa vinauliwa na tunawasihi wananchi kuhakikisha wanachemsha maji, wanakula vyakula vya moto ili tuweze kupunguza maambukizi ya kipindupindu.

Mheshimiwa Naibu Spika, visima tayari, bado kusambaza, tayari Serikali tumeanza kufikia visima vyote vilivyochimbwa na vina maji ya kutosha kuona tunaleta usambazaji. Vilevile kama kisima kina maji kidogo tunaweka japo vichotea maji viwili, vitatu katika lile eneo ili wananchi waweze kufikiwa. Hivyo nikupongeze dada yangu Mheshimiwa Josephine kwa ufatliaji huo na niseme kwamba tutakuja kuhakikisha visima vyote vilivyochimbwa vinaweza kuleta tija ya wananchi kupata maji safi na salama bombani.

Name

Esther Lukago Midimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza:- Je, lini Halmashauri ya Mji wa Kasulu itaondokana na matumizi ya maji machafu kutokana na ukosefu wa chujio?

Supplementary Question 2

MHE. ESTHER L. MIDIMU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali la nyongeza. Je, Mradi wa Maji wa Malampaka Male utaanza lini?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer


NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante naomba kujibu swali la nyongeza la Esther, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Mradi wa Malampaka upo kwenye hatua za mwisho kabisa na kuona kwamba tunaanza kuutekeleza.

Name

Mwanaisha Ng'anzi Ulenge

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza:- Je, lini Halmashauri ya Mji wa Kasulu itaondokana na matumizi ya maji machafu kutokana na ukosefu wa chujio?

Supplementary Question 3

MHE. ENG. MWANAISHA N. ULENGE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, kwanza nimpongeze Naibu Waziri kwa ziara yake nzuri aliyoifanya katika Wilaya ya Lushoto na sasa maji yanatiririka pale kwenye Kata ya Kwai. Naomba kuuliza ule mradi mkubwa ambao uta-cover kata 13 za Wilaya ya Lushoto ni lini utaanza?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ulenge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nipende kukushukuru kwa pongezi zako lakini kwa kazi kubwa na wewe unayoshiriki kuifanya katika Jimbo la Lushoto katika majimbo yale matatu ushiriki wako niliweza kuukuta na hongera sana pia.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mradi huu wa kata 15 ambao umeutaja tayari Serikali tunaendelea na hatua za mwisho kabisa ili tuweze kuja kuuanza mara moja na utekelezaji utaendelea mwaka ujao wa fedha.