Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 3 Water and Irrigation Wizara ya Maji 43 2024-02-01

Name

Josephine Johnson Genzabuke

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza:-

Je, lini Halmashauri ya Mji wa Kasulu itaondokana na matumizi ya maji machafu kutokana na ukosefu wa chujio?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji naomba kujibu swali la Mheshimiwa Josephine Johnson Gezabuke, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kuna ukosefu wa miundombinu ya kusafisha na kutibu maji katika Halmashauri ya Mji wa Kasulu. Ili kutatua changamoto Serikali imekamilisha ukarabati wa chujio la maji la Kabanga ambalo limeanza kufanya kazi. Chujio hilo lina uwezo wa kuchuja maji jumla ya lita 1,000,000 kwa siku. Aidha, ujenzi wa machujio ya maji kutoka vyanzo vya Mto Chai na Miseno umeanza na unatarajiwa kukamilika ifikapo mwezi Aprili, 2024. Machujio haya yatakuwa na uwezo wa kuchuja maji jumla ya lita 3,000,000 kwa siku. Kwa sasa utekelezaji wake umefikia asilimia 15.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia mradi wa maji wa miji 28 imeanza ujenzi wa chujio la maji kutoka chanzo cha maji cha Mto Ruchunji. Kwa sasa mradi huo utekelezaji wake umefikia asilimia 5 na unatarajiwa kukamilika ifikapo mwezi Aprili, 2025 ambapo chujio hilo litakuwa na uwezo wa kuchuja maji jumla ya lita 15,000,000 kwa siku.