Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Nashon William Bidyanguze

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigoma Kusini

Primary Question

MHE. NASHON W. BIDYANGUZE aliuliza:- Je, lini Serikali itakamilisha ahadi ya shilingi milioni 10 za ujenzi wa Kituo cha Afya cha Kazuramimba?

Supplementary Question 1

MHE. NASHON W. BIDYANGUZE: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niulize swali langu la nyongeza, kwamba kwa kuwa Kituo cha Afya cha Kazuramimba ni kata ya kimkakati. Sasa ni lini Serikali itapeleka fedha kwa ajili ya kujenga majengo mengine? Ahsante.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana na naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Bidyanguze, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, nimwakikishie kwamba Serikali hii ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan tayari imeshaainisha maeneo yote ya kata za kimkakati kwa ajili ya ujenzi wa vituo vya afya kwa awamu na mpaka sasa imeshajenga vituo vyake 466 vyenye thamani ya shilingi bilioni 718 na Kituo cha Afya cha Kazuramimba ni miongoni mwa vituo hivyo ambavyo vitatengewa fedha kwa ajili ya majengo mengine, ahsante.

Name

Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Primary Question

MHE. NASHON W. BIDYANGUZE aliuliza:- Je, lini Serikali itakamilisha ahadi ya shilingi milioni 10 za ujenzi wa Kituo cha Afya cha Kazuramimba?

Supplementary Question 2

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi pamoja na jitihada hizo nzuri za Serikali lakini vituo vingi vya afya ikiwemo cha Bumilainga na Ifingo bado havijakuwa na miundombinu ya kutosha ikiwemo kuwepo wodi ya akinamama na wodi ya wanaume.

Je, Serikali iko tayari kwenda awamu ya pili kwa kuanza kujenga facilities hizo muhimu?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana na naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Cosato Chumi, Mbunge wa Jimbo la Mafinga, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, nimwakikishie tu kwamba Serikali iko tayari kuendelea na ujenzi wa majengo ya wodi za wanawake na wanaume katika Kituo cha Afya cha Ifingo na kituo hicho alichokitaja pia katika vituo vyote ambavyo vimejengwa awamu ya kwanza vyote vitakwenda awamu ya pili kwa ajili ya kukamilisha miundombinu, ahsante.