Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 3 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 41 2024-02-01

Name

Nashon William Bidyanguze

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigoma Kusini

Primary Question

MHE. NASHON W. BIDYANGUZE aliuliza:-

Je, lini Serikali itakamilisha ahadi ya shilingi milioni 10 za ujenzi wa Kituo cha Afya cha Kazuramimba?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Nashon William Bidyanguze, Mbunge wa Jimbo la Kigoma Kusini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imeendelea kutenga fedha kwa awamu kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu katika Kituo cha Afya Kazuramimba. Katika mwaka wa fedha 2022/2023, Serikali kupitia mapato ya ndani ya halmashauri ilitenga shilingi millioni 158 na kuendeleza ujenzi wa Jengo la wagonjwa wa nje (OPD) ambalo ujenzi wake upo katika hatua za ukamilishaji.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali itaendelea kutenga fedha kupitia vyanzo mbalimbali na kuhakikisha inajenga na kukamilisha vituo vya afya kwenye maeneo ya kimkakati kote Nchini kikiwemo kituo cha Afya Kazuramimba, ahsante.