Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA aliuliza: - Je, lini Serikali itaingia ubia na Wakala wa Nyumba Tanzania (TBA) kuwajengea nyumba walimu nchini na kisha kuwakata mishahara yao?

Supplementary Question 1

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nishukuru kwa majibu, lakini lengo la swali langu lilikuwa ni Serikali kuingia ubia na TBA, kwanza halmashauri watenge maeneo ya makazi, waingie mkataba na TBA, wajenge nyumba za gharama nafuu, ambazo walimu watagawiwa kwa mkataba ambao wataingia nayo. Kwa maana ya kwamba zile nyumba ambazo watamiliki wao hata kama ukistaafu itakuwa nyumba za kuanzia maisha sio nyumba za shule ambazo zinamilikiwa na halmashauri.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu je, Serikali haioni namna bora ya kuwasaidia walimu hasa wale wastaafu wanapotangatanga baada ya kukosa makazi na umri wao wa kuishi nao unapungua kwa sababu ya stress za kukosa makazi. Je, Serikali haioni umuhimu wa kuwajengea nyumba walimu hawa?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, nikijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kuchauka, kwanza nikiri tunapokea mawazo na maoni ya Mheshimiwa Kuchauka aliyoyatoa na kama nilivyosema kwenye majibu yangu ya msingi ya kwamba itabidi tukae na walimu wenyewe kwa sababu jambo lenyewe ni la hiari la wao kuweza kuchangia au kukatwa katika mishahara yao kulipia nyumba zile ambazo zitakuwa zimejengwa kwa ajili yao.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kukubaliana nao ndipo basi Serikali itakaa ubia na TBA, National Housing, Watumishi Housing, taasisi nyingi nyingine na Serikali kwa ajili ya kuona ni namna gani nyumba hizi zinaweza zikajengwa kwa ajili ya kuweza kuwauzia walimu.