Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 3 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 40 2024-02-01

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA aliuliza: -

Je, lini Serikali itaingia ubia na Wakala wa Nyumba Tanzania (TBA) kuwajengea nyumba walimu nchini na kisha kuwakata mishahara yao?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Zuberi Mohamedi Kuchauka, Mbunge wa Jimbo la Liwale, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatambua mahitaji ya nyumba kwa ajili ya walimu ambapo kuanzia mwaka wa fedha 2021 hadi 2023 zimejengwa nyumba 562 zenye uwezo wa kuchukua familia 1,124 kwa thamani ya shilingi 56,325,000,000.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa pendekezo la Mheshimiwa Mbunge ni la msingi na linahusisha ujenzi wa nyumba ambazo itabidi Walimu wazilipie kupitia mishahara yao, Serikali itakaa kwanza na walimu ili kulijadili na endapo wataafiki wazo hilo litawasilishwa kwa Wakala wa Nyumba Tanzania (TBA) kwa ajili ya makubaliano.