Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Twaha Ally Mpembenwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibiti

Primary Question

MHE. TWAHA A. MPEMBENWE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ukarabati wa shule chakavu za msingi Jimbo la Kibiti?

Supplementary Question 1


MHE. TWAHA A. MPEMBENWE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Naipongeza Serikali kwa majibu mazuri. Pamoja na hayo, nina maswali mawili madogo ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza, je, Serikali ina mpango gani sasa wa kuweza kujenga shule mpya katika Jimbo la Kibiti?

Mheshimiwa Naibu Spika, la pili, naomba kuuliza: Serikali ina mpango gani wa dharura wa kuweza kukarabati Shule ya Msingi ya Mchukwi pamoja na Shule ya Msingi ya Nyanjati iliyopo katika Kata ya Mahenge?

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana.

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, nikijibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Twaha Mpembenwe, hili la kwanza la mpango wa Serikali kujenga shule mpya katika Wilaya ya Kibiti, nimtaarifu tu Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali hii ya Awamu ya Sita ya Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, kupitia Mradi wa Boost, imejenga shule mbili mpya katika Jimbo lake la Kibiti. Jumla ya shilingi milioni 821 zilipelekwa katika Halmashauri ya Kibiti kujenga shule hizo ambazo ipo ya Itonga Kata ya Bungu na vilevile kuna shule inaitwa Mpembenwe ambayo imejengwa, ilipelekewa shilingi milioni 306 kwa ajili ya ujenzi wa shule hiyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, nakwenda kwenye swali la pili sasa. Mheshimiwa Twaha Mpembenwe amekuwa akiifuatilia sana juu ya ujenzi wa shule hizi za Mchukwa na nyingineyo ambayo imetajwa. Namtoa mashaka, Serikali hii itatafuta fedha na kuweza kupeleka kwa ajili ya ukarabati wa maeneo haya ambayo ameyataja.

Mheshimiwa Naibu Spika, vile vile, kule Kibiti kuna shule mpya ya Sekondari ambayo sasa fedha imepelekwa kwa jitihada zake Mheshimiwa Mbunge na Mheshimiwa Rais wetu Dkt. Samia Suluhu Hassan, alitoa fedha kwa ajili ya kujenga shule katika Kata ya Kibiti.

Name

Nicholaus George Ngassa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igunga

Primary Question

MHE. TWAHA A. MPEMBENWE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ukarabati wa shule chakavu za msingi Jimbo la Kibiti?

Supplementary Question 2

MHE. NICHOLAUS G. NGASSA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana. Kwenye Jimbo la Igunga, kuna changamoto kubwa sana kwenye Shule ya Msingi Butamisuzi Kata ya Mbutu na Mwajinjama. Tunaishukuru Serikali, Shule ya Msingi ya Buta wametupatia fedha kuboresha madarasa chakavu. Imebaki changamoto kwenye Shule ya Msingi Mwajinjama iliyopo Kata ya Mtungulu: Je, ni lini Serikali mtapeleka fedha kwa ajili ya kutusaidia kuboresha madarasa?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, nikijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ngassa, kwa sasa kuna tathmini ambayo ilikuwa inafanyika na Ofisi ya Rais, TAMISEMI kupitia kwa Maafisa Elimu wetu wa Msingi katika Halmashauri zote hapa nchini ili kuweza kupata taarifa sahihi ya idadi ya madarasa yanayohitajika ili fedha iweze kutafutwa na kupelekwa. Vilevile kule kwa Mheshimiwa Ngassa, itafanyika hivyo.

Name

Festo Richard Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makete

Primary Question

MHE. TWAHA A. MPEMBENWE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ukarabati wa shule chakavu za msingi Jimbo la Kibiti?

Supplementary Question 3

MHE. FESTO R. SANGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kutokana na uchakavu wa majengo kwenye shule za msingi kule Makete, Waratibu Kata Elimu leo wamekuja kutoka Makete wako hapa wanataka kujua ni lini Serikali itapeleka fedha za kukarabati Shule ya Msingi Lupalilo, Shule ya Msingi Ikungula, Shule ya Msingi Iwawa na Shule ya Msingi Kijombo? Waratibu wangu wa Elimu Kata wako hapa leo, wanataka waondoke na majibu ya Serikali. Ni lini fedha zitatoka? (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, fedha itapelekwa na Serikali katika Shule za Msingi Lupalilo, Ikungula na maeneo mengine ambayo ameyataja Mheshimiwa Sanga hapa kadri ya upatikanaji wa fedha hizo. Kama nilivyomjibu Mheshimiwa Ngassa, kwa hiyo na tathmini inayofanyika hivi sasa na baada ya tathmini hiyo kukamilika, Serikali itatafuta fedha hizo na kuweza kupeleka huko.

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TWAHA A. MPEMBENWE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ukarabati wa shule chakavu za msingi Jimbo la Kibiti?

Supplementary Question 4

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Naibu Spika, kuna shule za msingi ambazo ni kongwe zimejengwa miaka ya 1960 na 1970 ambazo hazifai kabisa kukarabatiwa bali inabidi Serikali iende na mkakati wa kuzijenga upya. Mathalan Shule ya Msingi Nyabilongo, Kikomori na Kiongera zilizopo Kata ya Susuni, Jimbo la Tarime Vijijini. Ni shule ambazo ni hatarishi hata kwa wanafunzi wanaposoma katika maeneo hayo.
Mheshimiwa Naibu Spika, nataka kujua ni nini mkakati wa Serikali kuhakikisha kwamba inapeleka fedha kwa uharaka ili hizi shule kongwe ziweze kujengwa na kuweza kunusuru maisha ya wanafunzi wale? (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, nikijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Matiko, kwanza niliarifu Bunge lako Tukufu kwamba katika kipindi hiki cha uongozi wa Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, ndiyo kipindi ambacho Serikali hii ya Awamu ya Sita imewekeza zaidi ya shilingi bilioni 230 katika ujenzi wa shule mpya na ukarabati wa madarasa kwenye Elimu Msingi kuliko wakati mwingine wowote ule. Hivyo basi, nimtoe mashaka Mheshimiwa Matiko, shule hizi alizozitaja tutaziweka katika mpango na kuona ni namna gani fedha inazifikia kwa ajili ya ukarabati wa madarasa na ujenzi wa majengo mapya katika shule hizi. (Makofi)

Name

Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Primary Question

MHE. TWAHA A. MPEMBENWE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ukarabati wa shule chakavu za msingi Jimbo la Kibiti?

Supplementary Question 5

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Tunaipongeza Serikali kwa jitihada kubwa ya ukarabati na ujenzi wa shule mpya hapa nchini. Je, Serikali ina mpango gani sasa wa kujenga nyumba za walimu ambazo hazifai kabisa katika hizo shule kongwe nchini? (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, nikimjibu Mheshimiwa Issaay, kutoka mwaka 2021 hadi 2023, Serikali hii imejenga zaidi ya nyumba 562 za walimu kote nchini ambapo imetumika zaidi ya shilingi bilioni 56,325,000,000/= kwa ajili ya ujenzi wa nyumba hizi za walimu.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimtoe mashaka Mheshimiwa Mbunge, Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya ujenzi wa nyumba zaidi za walimu kama ambavyo umeona jitihada hizi zinafanyika kwa sasa.