Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 3 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 39 2024-02-01

Name

Twaha Ally Mpembenwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibiti

Primary Question

MHE. TWAHA A. MPEMBENWE aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaanza ukarabati wa shule chakavu za msingi Jimbo la Kibiti?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Twaha Ally Mpembenwe, Mbunge wa Jimbo la Kibiti, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imeanza ukarabati wa shule chakavu ambapo katika mwaka wa fedha 2022/2023, Serikali ilipeleka shilingi milioni 100 kwa ajili ya ukarabati wa Shule ya Msingi Kiasi. Aidha, katika Mwaka wa Fedha 2023/24, Serikali imepeleka shilingi milioni 180 kwa ajili ya kukarabati shule chakavu za msingi katika Jimbo la Kibiti ambapo jumla ya shule nne zitakarabatiwa ambazo ni Pongwe (maradasa matatu yalikarabatiwa), Mchinga (madarasa mawili), Saninga (madarasa mawili) na Misimbo (madarasa mawili).