Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Juma Othman Hija

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tumbatu

Primary Question

MHE. JUMA OTHMAN HIJA aliuliza:- Je, ni kwa kiasi gani lengo la Benki Kuu la kutoa mikopo kwa sekta binafsi limefikiwa?

Supplementary Question 1

MHE. JUMA OTHMAN HIJA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nina swali moja la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, miongoni mwa changamoto zinazoikabili mtaji wa sekta binafsi ni viwango vya riba katika benki zetu. Je, Serikali ina mpango gani kudhibiti viwango hivi vya riba? (Makofi)

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Juma Othman Hija, Mbunge wa Tumbatu, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Benki Kuu ya Tanzania ilishatoa trilioni moja kwa benki ili kutoa mikopo hasa ya kilimo kwa riba nafuu, isiyozidi asilimia 10 na zipo Benki zetu kama vile CRDB, NMB katika dirisha la kilimo wapo na single digit. Nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali imezingatia na itaendelea kuangalia viwango vya riba kulingana na hali ya uchumi nchini, ahsante.

Name

Asha Abdullah Juma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JUMA OTHMAN HIJA aliuliza:- Je, ni kwa kiasi gani lengo la Benki Kuu la kutoa mikopo kwa sekta binafsi limefikiwa?

Supplementary Question 2

MHE. ASHA ABDULLAH JUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi. Kwa kuwa Benki Kuu ya Tanzania ndio custodian wa waendesha biashara za benki nchini Tanzania.

Je, ni lini Serikali kupitia Benki Kuu ya Tanzania itachukua hatua ya kuwafidia waliokuwa wateja wa SBNE pamoja na wafanyakazi kuwalipa haki zao kama vile inavyofanya SMZ - Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, imewalipa wateja wa Master Life waliopata kadhia kama hiyo? Sasa Serikali hii yetu ya Tanzanzania itafanya nini na kwa nini haiwapi taarifa wananchi kuhusu kadhia hiyo? (Makofi)

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Asha Mshua, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imechukua hatua mbalimbali kutoa fidia kwa wale waathirika wa benki kama zilivyotokea wakati huo na bado Serikali ipo inafanya upembuzi, fedha itakapojitosheleza na kujiridhisha Serikali itatoa fidia kwa wananchi wake. (Makofi)

Name

Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JUMA OTHMAN HIJA aliuliza:- Je, ni kwa kiasi gani lengo la Benki Kuu la kutoa mikopo kwa sekta binafsi limefikiwa?

Supplementary Question 3

MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali dogo la nyongeza. Tunatambua kwamba kuna mwongozo ambao umetolewa na Wizara ya fedha ku-regulate riba kwenye microfinace hapa nchini, lakini mwongozo huo haufuatwi na hizo taasisi za kutoa fedha wakati mwingine zinachukua hadi kadi za ATM za watumishi wanaokwenda kukopa pale, Serikali inasema nini juu ya hili ili miongozo hiyo iweze kufuatwa?

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali siku zote inafuata miongozo na taratibu ambazo zimewekwa, kama zipo changamoto ambazo ameziona acha tuzichukue twende tukajadili, tuangalie, tukijiridhisha basi tutazifanyia kazi. (Makofi)