Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 49 Finance and Planning Wizara ya Fedha na Mipango 437 2022-06-22

Name

Juma Othman Hija

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tumbatu

Primary Question

MHE. JUMA OTHMAN HIJA aliuliza:-

Je, ni kwa kiasi gani lengo la Benki Kuu la kutoa mikopo kwa sekta binafsi limefikiwa?

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Juma Othman Hija, Mbunge wa Tumbatu kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Sera ya Fedha ya Mwaka 2021/2022, imeainisha shabaha ya ukuaji wa mikopo kwa sekta binafsi wa asilimia 10.6 ili kuwezesha upatikanaji wa mikopo kwa gharama nafuu na kuongeza ukwasi katika uchumi. Kutokana na utekelezaji wa sera hiyo, kiwango cha ukuaji wa mikopo kwa sekta binafsi kimeendelea kuongezeka kufikia wastani wa asilimia 8.4 katika kipindi cha Julai, 2021 hadi Aprili, 2022, ikilinganishwa na wastani wa asilimia 4.3 katika kipindi cha Julai, 2020 hadi Aprili, 2021.

Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, kuanzia mwezi Desemba, 2021, ukuaji wa mikopo kwa sekta binafsi ulikuwa zaidi ya asilimia 10 ambapo mwezi Aprili, 2022, ukuaji huu ulifikia asilimia 13.4. Kutokana na mwenendo huu ni matarajio yetu kuwa, lengo la ukuaji wa mikopo kwa sekta binafsi la asilimia 10.6 kwa mwaka 2021/2022 litafikiwa na hivyo kuchangia uwekezaji, uzalishaji na kuongeza ajira nchini, ahsante.