Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ndaisaba George Ruhoro

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngara

Primary Question

MHE. NDAISABA G. RUHORO aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha wananchi wa Jimbo la Ngara wananufaika na uchimbaji wa madini ya Nickel?

Supplementary Question 1

MHE. NDAISABA G. RUHORO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana na nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali, lakini nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; kwa kuwa ilitokea katika historia ya Nchi yetu Tanzania ikatawaliwa na wakoloni na kwa kuwa wakoloni hawa walifanya tafiti mbalimbali za madini hapa nchini, sambamba na kuchimba madini hayo.

Je, ni lini Wizara ya Madini itawaomba wakoloni hawa waje kufunga mashimo waliyoyaacha kwa maana ya kufanya mining closure?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; naomba kujua kama Wizara ya Madini wanazo tafiti zilizoachwa na wakoloni ili waweze kuziweka wazi kwa Watanzania ili waweze kuwekeza kwenye madini. Ahsante.

Name

Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili madogo ya nyongeza ya Mheshimiwa Ndaisaba George Ruhoro, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa swali lake la kwanza, kuhusu wakoloni ambao walifanya tafiti, wakachimba madini na wakaacha mashimo na yeye kutaka kujua mpango wa haya mashimo kuja kufungwa, nipende kumjulisha Mheshimiwa Mbunge kwamba, wakoloni wa Kijerumani ambao walifanya utafiti mkubwa wa madini ya makaa ya mawe na hata dhahabu katika maeneo mbalimbali ya nchi yetu ikiwepo kule Ngara na maeneo ya Sekenke Singida waliondoka kabla hawajayamaliza madini katika machimbo hayo, hivyo hawakuhangaika kuyafunga na mashimo haya yamekuwa msaada kwetu katika kuendeleza tafiti.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika maeneo mengine leseni zimeshatolewa na mashimo haya yamekuwa yakitoa mwongozo wa kubaini madini yaliyopo ili tuendelee kuyavuna na hivyo basi kwa ajili ya jibu la swali lake hilo pia kwa kipengele cha hayo mashimo, wale waliopewa leseni sasa kulingana na Sheria yetu ya Madini, Sura ya 125 ndio wamepewa wajibu wa kuandaa closure plan, mpango wa ufungaji wa mgodi kulingana na Sheria ya Mazingira ya mwaka 2004 ambao unamtaka mwenye mgodi aweke utaratibu wa jinsi atakavyorejesha ile ardhi katika hali yake salama baada ya mradi kumaliza uhai wake. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa upande wa swali lake la pili, hizo takwimu za tafiti zilizofanywa na wakoloni tutazipataje. Kwa bahati nzuri wajerumani walivyofanya tafiti za madini katika nchi hii kuanzia mwaka 1925, waliacha takwimu za kutosha, data zipo katika archives zetu katika taasisi yetu ya GST hapa hapa Dodoma.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa kuibua hilo swali ili nitumie fursa hii kutoa rai kwa Watanzania wanaopenda kufanya biashara za madini kwamba tunazo data za tangu enzi za ukoloni mwaka 1925, waje wazifuatilie kule, maktaba ipo na wanaweza wakapata taarifa za kijiolojia za kuwaongoza katika kwenda kuendeleza kwenye uchimbaji wa madini husika katika maeneo yaliyofanyiwa utafiti. Ahsante sana.

Name

Deodatus Philip Mwanyika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Primary Question

MHE. NDAISABA G. RUHORO aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha wananchi wa Jimbo la Ngara wananufaika na uchimbaji wa madini ya Nickel?

Supplementary Question 2

MHE. DEODATUS P. MWANYIKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali dogo la nyongeza. Je, ni lini Serikali sasa itawaangalia wachimbaji wadogo wa Mkoa wa Njombe ambao walishaomba leseni za kuchimba makaa ya mawe kule Ludewa na Wizara imeshawaahidi na wakaunda vikundi, lini watawapa leseni?

Name

Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Deodatus Mwanyika, Mbunge wa Njombe Mjini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kuna wachimbaji wengi nchini ambao wameomba leseni za uchimbaji na bado hawajapata na hasa wa jimbo lake ambapo kuna maeneo ya machimbo ya makaa ya mawe ambayo yapo katika eneo linalomilikiwa na Taasisi nyingine ya umma ya NDC. Kwa sababu ya utaratibu kwamba yale maeneo yana wamiliki wengine sisi tukitoa leseni ni lazima wale waliopewa leseni wakaombe mwenye surface right kuingia katika uchimbaji na mchakato wa kuwasaidia wachimbaji wadogo ili wapate maeneo ya kuchimba ni moja ya dhamana tuliyopewa sisi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hivyo, nimwahidi tu Mbunge kwamba baada ya Bunge hili mwezi Julai, mimi binafsi nitafika katika maeneo hayo yenye wachimbaji ambao wamepata leseni au wanaomba leseni hawajapata, tujue changamoto zinazowakabili ili tuzitatue na waweze kupata maeneo maana ni dhamira yetu kwamba wachimbaji wadogo wapewe maeneo ya kuchimba ili wapate tija kutokana na rasilimali madini yaliyopo katika nchi yetu. (Makofi)