Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 49 Energy and Minerals Wizara ya Madini 435 2022-06-22

Name

Ndaisaba George Ruhoro

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngara

Primary Question

MHE. NDAISABA G. RUHORO aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha wananchi wa Jimbo la Ngara wananufaika na uchimbaji wa madini ya Nickel?

Name

Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Madini, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Ndaisaba George Ruhoro, Mbunge wa Jimbo la Ngara, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, uchimbaji wa madini ya Nickel katika eneo la Kabanga unafanywa na Kampuni ya Tembo Nickel Corporation Limited iliyopewa leseni mnamo tarehe 25 Oktoba, 2021. Mradi huo unatarajiwa kuchangia ushuru wa huduma kwa Halmashauri ya Wilaya ya Ngara kiasi cha dola za Marekani milioni 65, sawa na takribani shilingi bilioni 151 kwa kipindi cha uhai wa mgodi huo. Aidha, mradi huo unatarajia kutoa ajira za moja kwa moja 978 kwa Watanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hadi kufikia Aprili, 2022 mradi ulikuwa umetumia jumla ya dola za Marekani milioni 1.5 katika ununuzi wa bidhaa na huduma ndani ya nchi. Kati ya hizo, Dola 125,673 zilitumika kufanya ununuzi katika Wilaya ya Ngara. Hivyo, nitoe rai kwa wananchi wa Wilaya ya Ngara na Taifa kwa ujumla kuchangamkia fursa zilizopo katika mradi huo. Aidha, kupitia Sheria ya Wajibu wa Makampuni kwa Jamii (Cooperate Social Responsibility - CSR), mradi huo ulichangia takribani Shilingi milioni 39 kwa mwaka 2021 na unatarajiwa kuchangia jumla kiasi cha shilingi milioni 207.8 mwaka huu 2022, ahsante sana.