Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Soud Mohammed Jumah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Donge

Primary Question

MHE. SOUD MOHAMMED JUMAH aliuliza:- Je, kuna mkakati gani wa kupunguza athari hasi zitakazojitokeza kutokana na kuondolewa kwa buffer zone katika hifadhi na mapori?

Supplementary Question 1

MHE. SOUD MOHAMMED JUMAH: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa kuondoshwa kwa maeneo ya kinga (buffer zone) kunasogeza zaidi wananchi karibu na hifadhi na kuwahatarisha na wanyama wakali na waharibifu: Je, Serikali haioni haja ya kuja na mikakati zaidi ya kutoa elimu ili kuwasaidia wananchi hawa kuwaepusha na hiyo hatari? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili. Kwa kuwa buffer zone kitaalam inalenga kuwatenga wananchi na maeneo ya hifadhi na hivyo, kupunguza vitendo vya uharibifu na vitendo vya uvamizi.

Je, Serikali ina utaratibu gani wa kuhakikisha kwamba, utaratibu huu wa kuondoa buffer zone katika maeneo ya hifadhi haujirudii? Ahsante. (Makofi)

Name

Dunstan Luka Kitandula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkinga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mohammed Soud Jumah, Mbunge wa Donge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema kwenye jibu langu la msingi, Wizara inajielekeza sana kwenye kutoa elimu. Sambamba na hiyo, kwenye maeneo ya namna hii vilevile tuna mikakati ya kuwahamasisha wananchi kufuga nyuki kwenye maeneo hayo. Vilevile, kuendesha utalii wa kiutamaduni, kupanda au kutunza misitu ili waweze kuja na mfumo wa biashara ya uvunaji wa Hewa ya Ukaa. Tunaamini wananchi wakijielekeza kwenye maeneo haya, basi huo muingiliano utapungua athari zake.

Mheshimiwa Spika, katika swali la pili, ni kweli kwamba maeneo haya ya buffer zone yanalenga kuwatenga wananchi na maeneo ya hifadhi ili kuwaondolea athari ya madhara ya uvamizi na hivi. Pamoja na kutoa elimu, Wizara inajielekeza kwenye kusimamia sheria, kanuni na taratibu za uhifadhi na kutoa elimu kwa viongozi na wananchi. Imani yetu ni kwamba, elimu hii ikiwaingia wananchi na wakazingatia maelekezo haya, basi migogoro hii itaondoka. (Makofi)

Name

Christopher Olonyokie Ole-Sendeka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Simanjiro

Primary Question

MHE. SOUD MOHAMMED JUMAH aliuliza:- Je, kuna mkakati gani wa kupunguza athari hasi zitakazojitokeza kutokana na kuondolewa kwa buffer zone katika hifadhi na mapori?

Supplementary Question 2

MHE. CHRISTOPHER O. OLE-SENDEKA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa wanyama hao walioko katika maeneo yetu ya uhifadhi, mara baada tu ya kuvuka kwenye buffer zine wanaingia kwenye ardhi za vijiji.

Je, Wizara au Serikali haioni kwamba kuna haja sasa ya Wizara kukaa na vijiji vinavyozunguka maeno ya hifadhi ili kwa pamoja waweze kuweka utaratibu rafiki wa namna ya kusimamia wanyama pori nje ya hifadhi za Taifa na kupunguza athari zinazoweza kujitokeza katika maeneo hayo? (Makofi)

Name

Dunstan Luka Kitandula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkinga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ole-Sendeka kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Wizara imekuwa ikifanya jambo hili ambalo Mheshimiwa Ole-Sendeka amelishauri. Sambamba na hilo, tumekuwa tukishirikiana vilevile na Wizara ya Ardhi katika kufanya mipango ya matumizi bora ya ardhi. Tunaamini kwa kufanya hivyo tutaepuka changamoto tunazokabiliana nazo.