Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 10 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 146 2023-11-10

Name

Soud Mohammed Jumah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Donge

Primary Question

MHE. SOUD MOHAMMED JUMAH aliuliza:-

Je, kuna mkakati gani wa kupunguza athari hasi zitakazojitokeza kutokana na kuondolewa kwa buffer zone katika hifadhi na mapori?

Name

Dunstan Luka Kitandula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkinga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Soud Mohammed Jumah, Mbunge wa Donge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, maeneo ya kinga za hifadhi za wanyamapori husaidia wanyamapori kupata mahitaji yao ikiwemo malisho na hivyo kupunguza migongano baina ya binadamu na wanyamapori.

Mheshimiwa Spika, katika kupunguza athari za kutokuwa na maeneo ya kinga, Wizara kupitia taasisi zake za uhifadhi (TANAPA, TAWA na NCAA) inatoa elimu kwa wananchi kuhusu kutokuanzisha shughuli za kibinadamu kama vile kilimo na makazi kwenye maeneo ya karibu na hifadhi ili kuepuka madhara yanayoweza kusababishwa na wanyamapori.

Vilevile kuwaelimisha kuanzisha shughuli rafiki kama vile ufugaji nyuki kwenye maeneo hayo. Sambamba na hatua hiyo, jitihada za kudhibiti wanyamapori wakali na waharibifu zinafanyika ili kulinda wananchi na mali zao.