Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Daimu Iddi Mpakate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kusini

Primary Question

MHE. DAIMU I. MPAKATE aliuliza:- Katika Wilaya ya Tunduru iko miradi mingi ya REA ambayo kampuni mbili zimepewa kazi hiyo lakini wakandarasi wanasuasua kukamilisha miradi hiyo na muda wake umeisha kwa kigezo cha kutolipwa:- Je, ni lini Serikali itatoa pesa kukamilisha miradi hiyo?

Supplementary Question 1

MHE. DAIMU I. MPAKATE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kwanza, nashukuru kwa majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri lakini naomba nimuulize maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika Jimbo la Tunduru Kusini kama alivyozungumza, kuna kata 15 kati ya hizo ni vijiji vinne tu vya Kata ya Chiwana na Kata ya Mbesa ndivyo vimepata umeme. Je, kati ya kata hizi zifuatazo ni lini watapatiwa umeme wa REA, Kata za Mtina, Nalasi, Mchoteka, Malumba, Mbati, Ligoma, Namasakata, Mchesi, Lukumbule, Chiwana na Msechela?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kumekuwa na tabia ya mkandarasi anayejenga laini ya Mbesa kuwadai wananchi wetu Sh.200,000/- mpaka Sh.300,000/- kwa ajili ya kupelekewa nguzo na kuunganishiwa umeme katika nyumba zao. Je, ni hatua gani imechukuliwa ili mkandarasi huyu asiendelee na tabia hiyo kwani umeme huu ni haki yao wananchi kupewa bure kwa kulipa Sh.27,000/-? Ahsante

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, nikubaliane na Mheshimiwa Mpakate kwamba kwa kweli ni vijiji vinne tu ambavyo vimepata umeme kwenye jimbo lake lakini vijiji vingine vilivyosalia ambavyo jumla yake kwa kweli ni 67, vikiwemo Vijiji vya Semeni, Angalia, Jiungeni na vijiji vingine vya Mwenge vyote vitapata umeme kwenye REA Awamu ya III inayoanza mwezi Julai, 2016. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mpakate pamoja na wananchi wa Tunduru Kusini kwamba vijiji vyote vilivyosalia vitapata umeme kuanzia mwezi Julai 2016.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la pili kuhusiana na gharama ya nguzo ambayo wananchi wanatozwa, napenda kutumia fursa hii kuwaomba sana Waheshimiwa Wabunge na kuwahakikishia wananchi kama ifuatavyo: Kwanza kabisa, katika Mradi wa REA mteja yeyote hatakiwi kutozwa gharama ya nguzo, si Sh.200,000/- wala Sh.300,000/-. Naomba niwahakikishie wananchi wa Tunduru Kusini na Watanzania wengine, gharama za nguzo kwenye miradi ya REA Serikali imeshagharamia, kwa hiyo, mwananchi hatakiwi kutozwa gharama yoyote ile.
Mheshimiwa Naibu Spika, la pili, niendelee tu kusema kwamba kwenye miradi mingine ya TANESCO, gharama za nguzo ni kama ifuatavyo: Kwa mteja ambaye yuko umbali wa mita 30 -70, gharama yake ni Sh.177,000/- tu kwa vijijini na kwa mijini ni Sh.272,000/- tu. Kwa hiyo, napenda kutoa kabisa hili angalizo kwa wananchi, wasitozwe gharama zaidi ya hiyo kwa umbali ambao nimeutaja hata kwa miradi ya TANESCO.

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Primary Question

MHE. DAIMU I. MPAKATE aliuliza:- Katika Wilaya ya Tunduru iko miradi mingi ya REA ambayo kampuni mbili zimepewa kazi hiyo lakini wakandarasi wanasuasua kukamilisha miradi hiyo na muda wake umeisha kwa kigezo cha kutolipwa:- Je, ni lini Serikali itatoa pesa kukamilisha miradi hiyo?

Supplementary Question 2

MHE. ABDALLAH H. ULEGA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo moja la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa nasi wananchi wa Mkuranga tumeomba miradi ya umeme katika baadhi ya vijiji vyetu zaidi ya 30, vikiwemo Vijiji vya Mlamleni, Lugwadu, Mkola, Kazole, Lukanga, Mwajasi, Vianzi, Malela na vinginevyo, je, miradi hii itakamilika katika muda gani ili wananchi wale waweze kujiandaa kupokea miradi hii ya umeme?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, kama ambavyo nimesema, kwa sasa hivi tunafanya uhakiki katika utekelezaji wa REA Awamu ya II na mradi kabambe wa REA Awamu ya III unaanza Julai, 2016 na kukamilika kwa mradi huu ni miaka mitatu hadi minne. Kwa hiyo, ifikapo mwaka 2018/2019, Watanzania wote ambao watakuwa kwenye miradi ya REA Awamu ya II vikiwemo Vijiji vya Rugumu, Rukola, Malela pamoja na maeneo mengine ya Mkuranga vitapatiwa umeme ndani ya kipindi hicho.

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Primary Question

MHE. DAIMU I. MPAKATE aliuliza:- Katika Wilaya ya Tunduru iko miradi mingi ya REA ambayo kampuni mbili zimepewa kazi hiyo lakini wakandarasi wanasuasua kukamilisha miradi hiyo na muda wake umeisha kwa kigezo cha kutolipwa:- Je, ni lini Serikali itatoa pesa kukamilisha miradi hiyo?

Supplementary Question 3

MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kuniona. Kwa sababu swali la msingi limeongelea kuhusiana na tatizo kubwa la umeme na Wilaya ya Kalambo ni miongoni mwa Wilaya chache ambazo zilikuwa na umeme sifuri, je, Mheshimiwa Waziri anatuambia nini wananchi wa Kalambo juu ya vijiji vile ambavyo havijapata umeme kupatiwa umeme kabla hatujaenda awamu ya III?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, nikubaliane na Mheshimiwa Mbunge wa Kalambo kwamba vijiji 24 vilivyobaki katika eneo la Kalambo ambavyo vilikuwa kwenye REA Awamu ya II vitakamilika ndani ya mwezi huu, siku 10 zilizobaki kwa mwezi wa Juni. Hata hivyo, vijiji ambavyo vimebaki ambavyo ni nje ya vijiji hivyo vitaendelea kupatiwa umeme katika Mradi wa REA unaokuja.
Mheshimiwa Naibu Spika, hali kadhalika bado TANESCO inaendelea kusambaza umeme kama kawaida. Kwa hiyo, vijiji ambavyo vitakuwa bado havijapitiwa umeme kwenye vitongoji vyake kwa umeme wa underline transformer ambao utakuwa unashusha umeme kwenye vijiji na vitongoji Mheshimiwa wa Kalambo bado vitapatiwa umeme. Tunataka kufikia 2025 vijiji vyote, kama nilivyokwisha kusema, vya Watanzania vitakuwa vimepatiwa umeme pamoja na vijiji vyote vya Jimbo la Kalambo.

Name

Zaynab Matitu Vulu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DAIMU I. MPAKATE aliuliza:- Katika Wilaya ya Tunduru iko miradi mingi ya REA ambayo kampuni mbili zimepewa kazi hiyo lakini wakandarasi wanasuasua kukamilisha miradi hiyo na muda wake umeisha kwa kigezo cha kutolipwa:- Je, ni lini Serikali itatoa pesa kukamilisha miradi hiyo?

Supplementary Question 4

MHE. ZAYNABU M. VULU: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kwa kuwa REA inapeleka umeme vijijini na wakandarasi ndiyo wanaosimamia uwekaji wa vifaa vya umeme kwenye vijiji, je, Serikali inaweza ikatuambia kuna tatizo gani katika Kijiji cha Zegero, Kata ya Kurui?
Mheshimiwa Naibu Spika, kuna transformer imekaa pale zaidi ya miezi sita na wakati napita kwenye ziara nimeikuta pale toka 7 Aprili, je, Serikali inasema nini? Wananchi wanaiona ile transformer pale wana mategemeo ya kupata umeme lakini mpaka leo hii hawajapata umeme. Mbali ya hayo, transformer ile inaharibika kwa kunyeshewa na mvua bila kupata usimamizi na watoto kuichezea. Naomba majibu

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa sipendi kukataa, kama kuna transformer imeharibika na iko pale muda mrefu, Mheshimiwa Vulu naomba sana tukitoka hapa mimi na wewe tuongozane tukaone hiyo transformer na ikiwezekana ifanyiwe ukarabati. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini nichukue fursa hii kuwaambia Waheshimiwa Wabunge kwamba kuanzia sasa Serikali imekusudia ma-transformer yote yanayotengenezwa hapa nchini ndiyo yatakayokuwa yanatumika kwa ajili ya kuunganishia umeme wetu. TANESCO sasa haitaagiza transformer kutoka nje, itakuwa inanunua ma-transformer kutoka hapa nchini. Kampuni ya TANELEC sasa hivi ina uwezo wa kuzalisha transformer 883 kwa mwezi ambapo mahitaji ya TANESCO ni ma-transformer 80. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, Mheshimiwa Vulu nikuombe sana, kama transformer bado ipo mimi na wewe tukitoka hapa tuongozane sambamba, tukae tujadiliane tufanye marekebisho ya transformer hiyo ili wananchi waendelee kupata umeme wa uhakika.

Name

Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Primary Question

MHE. DAIMU I. MPAKATE aliuliza:- Katika Wilaya ya Tunduru iko miradi mingi ya REA ambayo kampuni mbili zimepewa kazi hiyo lakini wakandarasi wanasuasua kukamilisha miradi hiyo na muda wake umeisha kwa kigezo cha kutolipwa:- Je, ni lini Serikali itatoa pesa kukamilisha miradi hiyo?

Supplementary Question 5

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Mimi naanza kutia mashaka kidogo kwenye miradi hii ya REA kwa sababu Waziri na Naibu Waziri wanasema mwezi wa sita ndiyo itakuwa mwisho wa REA Phase II lakini vijiji vyangu vya Jimbo la Bunda; Sanzati, Mikomahiro na Mihingo mpaka leo transformer iko moja kwenye Kijiji cha Sanzati na sioni kama kuna miradi inayoendelea pale, sioni kama kuna mafundi pale! Ni lini miradi hii itakwisha?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, tulishakaa na Mheshimiwa Mbunge na tukajadiliana kuhusu vijiji vyake vya Sanzati na vingine. Vijiji alivyotaja Mheshimiwa Mbunge hivi sasa tunapoongea kazi inaendelea. Isipokuwa katika maeneo anayoyataja Mheshimiwa Mbunge nadhani vile vijiji sita kazi ambayo imebakia sasa ni kushusha nyaya chini kabla hawajawasha. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge pamoja na wananchi wa Bunda Vijijini na Bunda Mjini kwa ujumla wake vijiji vyote ambavyo viko kwenye ile Awamu ya II kama ambavyo inatekelezwa itakamilika ndani ya mwezi huu wa Juni.
Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo wananchi wasiwe na wasiwasi kwa vijiji ambavyo itaonekana kazi haitakamilika ndani ya mwezi Juni, tunaendelea kuifanyia kazi kuviwasha katika mradi wa REA Awamu ya III unaoanza Julai, 2016. Kwa hiyo, vijiji vya Bunda vyote vitapata umeme ifikapo mwaka 2017 kama mnavyotarajia.