Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Fakharia Shomar Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FAKHARIA SHOMAR KHAMIS aliuliza:- Je, Serikali inatoa kauli gani kuhusu kuwasaidia wazee waliopata ulemavu wakati wa kupigana Vita ya Kagera mwaka 1979?

Supplementary Question 1

MHE. FAKHARIA SHOMAR KHAMIS: Mheshimiwa Spika, ahsante. Sina budi kumshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri kwa jawabu lake zuri, litatoa matumaini kwa wazee wetu ambao kwa umri waliokuwanao sasa hivi hali yao kweli siyo nzuri tena.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa baadhi ya wazee hawa hawana familia, wanahitaji kuishi, lakini na bado wanaendelea kupita maofisini kuomba misaada: Je, kwa nini Serikali haiwezi kufanya mpango wa kuwatafutia mahala pa kuwaweka na kuwatunza wazee hawa ili kumaliza maisha yao?

Mheshimiwa Spika, swali la pili. Kwa kuwa wastaafu Serikalini hulipwa pension ya uzeeni hadi kufariki kwao, lakini kwa wazee hawa wanalipwa pension ya ulemavu: Kwa nini nao wasichanganywe katika kupewa pension ya uzeeni kama wanavyolipwa wastaafu wengine? (Makofi

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI K.n.y. WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA): Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, naomba kujibu maswali ya nyongeza ya Mheshimiwa Fakharia Shomar Khamis, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, moja, mapendekezo ya kuwatafutia mahali au kwa maneno mengine wajengewe makazi kwa sababu hawana familia; mfumo wa uendeshaji wa Serikali zetu za Mitaa na mambo ya Ustawi wa Jamii yanaruhusu pale ambapo mtu anakuwa hajiwezi kabisa, yapo makazi yaliyokuwa dedicated kwa ajili ya wazee hao. Pengine naomba wale ambao wameshindwa kabisa, wawasiliane na halmashauri zao ili kuona namna ya kuweza kuwasaidia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kisera tunapendelea zaidi wazee walelewe na vijana au ndugu zao kama utamaduni na maadili mema ya Watanzania yanavyofanyika.

Mheshimiwa Spika, kuhusu kuwachanganya hao ambao ni wapiganaji wa vita na wazee wengine wapate pension ya uzeeni, hili ni suala la kisera, litafikiriwa na Wizara husika ili tuweze kuona uwezekano wa kulitekeleza, nashukuru.

Name

Fatma Hassan Toufiq

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FAKHARIA SHOMAR KHAMIS aliuliza:- Je, Serikali inatoa kauli gani kuhusu kuwasaidia wazee waliopata ulemavu wakati wa kupigana Vita ya Kagera mwaka 1979?

Supplementary Question 2

MHE. FATMA H. TOUFIQ: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa fursa nami niulize swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, je, Serikali inatoa tamko gani kwa wale maaskari wapiganaji waliopigana Vita vya Kagera ambao hawakuajiriwa na sasa wana maisha duni? (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI K.n.y. WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA: Mheshimiwa Spika, kama nilivyojibu kwenye jibu la msingi, ni kwamba kwa mujibu wa takwimu tulizonazo, wazee wote ambao wanapata huduma ya pension na usaidizi wa kimatibabu ni 272. Kama wapo wazee ambao kwa bahati mbaya hawakuingia kwenye orodha hiyo, tumeelekeza waende karibu na vikosi vya Jeshi vilivyoko jirani na makazi waliyopo ili taarifa zao zihakikiwe na hatimaye waweze kupata huduma kama zile wanazopata wazee wenzao waliopigana vita hii, ahsante.

Name

Cecil David Mwambe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ndanda

Primary Question

MHE. FAKHARIA SHOMAR KHAMIS aliuliza:- Je, Serikali inatoa kauli gani kuhusu kuwasaidia wazee waliopata ulemavu wakati wa kupigana Vita ya Kagera mwaka 1979?

Supplementary Question 3

MHE. CECIL D. MWAMBE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Kumekuwa na utaratibu sasa hivi, wazee wanatufuata kule vijijini au watoto wao wakiamini kwamba wanadai fidia kutokana na ushiriki wao kwenye Jeshi lile la Mkoloni (KAR) au Vita ya Kagera. Nataka kufahamu kutoka Serikalini, hivi ni kweli kuna watu wanaodai fidia kutokana na maeneo hayo mawili niliyoyataja kwa maana Jeshi la KAR pamoja na Jeshi la waliokwenda kupigana kwenye Vita ya Kagera?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI K.n.y. WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA: Mheshimiwa Spika, kwa sababu swali la msingi ni Vita ya Kagera, naomba suala la KAR liweze kuletwa kama swali la msingi ili tuweze kulifanyia utafiti na hatimaye tutoe majibu fasaha katika Bunge lako. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kuhusu uwepo wa Wazee wa Vita ya Kagera ambao pengine wanalalamika kutopata fidia, ndiyo maana nimesema, tunazo takwimu kwamba wapo 272, kama wapo wazee wa namna hiyo Mheshimiwa Mbunge, nimeeleza hapa katika moja ya jibu la msingi kwa Mbunge aliyetangulia, waripoti kwenye Makambi ya Jeshi yaliyoko karibu na maeneo yao ili taarifa zao zihakikiwe, hatimaye waweze kapata haki wanayostahili, ahsante.

Name

Kasalali Emmanuel Mageni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sumve

Primary Question

MHE. FAKHARIA SHOMAR KHAMIS aliuliza:- Je, Serikali inatoa kauli gani kuhusu kuwasaidia wazee waliopata ulemavu wakati wa kupigana Vita ya Kagera mwaka 1979?

Supplementary Question 4

MHE. KASALALI E. MAGENI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Hili suala la wazee waliopigana vita vyetu kuidai Serikali limekuwa ni suala la muda mrefu na limekuwa kila siku likitolewa majibu: Je, ni lini sasa Serikali inaliahidi Bunge hili kwamba suala la wazee hawa litatolewa majibu ya mwisho na kutatuliwa liishe kabisa? (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI K.n.y. WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nikirejea majibu yangu ya swali la msingi, kwa mujibu wa takwimu zilizopo kwenye Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania ni kwamba wako wazee 272. Sasa kama wapo wazee wengine ambao kwa bahati mbaya wanaamini kwamba wana madai ya msingi, lakini hawamo kwenye orodha hii, tuko tayari kushirikiana na Mheshimiwa Mbunge ili wazee hawa wahahakikiwe taarifa zao, ikithibitika kwamba wanastahili Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, itawalipa hizo haki stahiki, ashante sana.