Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 9 Defence and National Service Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga taifa 132 2023-11-09

Name

Fakharia Shomar Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FAKHARIA SHOMAR KHAMIS aliuliza:-

Je, Serikali inatoa kauli gani kuhusu kuwasaidia wazee waliopata ulemavu wakati wa kupigana Vita ya Kagera mwaka 1979?

Name

Dr. Stergomena Lawrence Tax

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI K.n.y. WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Fakharia Shomar Khamis, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, takwimu zilizopo zinaonesha kuwa wazee walemavu wa vita ya Kagera wapatao 272 wanalipwa pensheni ya ulemavu. Baada ya vita kumalizika Serikali iliwasaidia wapiganaji wote waliopigana vita. Wengi kati ya wapiganaji hao walipewa ajira katika Vyombo vya Ulinzi na Usalama hususan Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania, Jeshi la Polisi na Jeshi la Magereza. Aidha, wapo walioshindwa kuajiriwa kutokana na sababu mbalimbali.

Mheshimiwa Spika, wazee walemavu waliopigana vita ya Kagera wanaendelea kupata matibabu katika hospitali za Jeshi na wanalipwa pensheni za ulemavu kwa mujibu wa Kanuni za Pensheni na Viinua Mgongo za mwaka 1966. Wizara inaendelea kufuatilia hali halisi za wazee waliopigana vita ili kuchukua hatua stahiki. Endapo kuna wazee na walemavu waliopigana vita ya Kagera ambao hawanufaiki na huduma zinazotolewa inashauriwa wawasilishe taarifa zao kwa ajili ya uhakiki na hatimaye waweze kunufaika na huduma hizo, nashukuru.