Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Rashid Abdalla Rashid

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiwani

Primary Question

MHE. RASHID ABDALLA RASHID aliuliza: - Je, lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Ofisi ya Polisi Jamii Shehia ya Kendwa?

Supplementary Question 1

MHE. RASHID ABDALLA RASHID: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Suala hili lilikuwa ni kama ukumbusho. Kipindi kilichopita niliuliza suala hili na jawabu likatoka kwamba wananchi wavute Subira, tutatumia Mfuko wa Tuzo na Tozo katika kipindi hiki ili tuweze kuikamilisha ofisi; lakini sasa majibu wa Mheshimiwa Naibu Waziri yanasema, sasa nitafute wadau; je, ni lipi jawabu sahihi la kushika? Nitafute wadau au Mfuko wa Tuzo na Tozo? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili. Mheshimiwa Naibu Waziri yupo tayari kufuatana nami baada ya Bunge hili ili aende akaone nguvu za wananchi walizozitumia katika ujenzi huo ili naye aweze kuona kwamba tutumie wadau au wa tuzo na tozo? (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, nakiri swali la Mheshimiwa Mbunge kuhusu kutumia wadau au tuzo na tozo, kama nilivyojibu kwenye swali la msingi, ni kweli kwamba tuzo na tozo hutumika kukamilisha Vituo vya Polisi vya ngazi ya jamii kuunga mkono nguvu za wananchi au ngazi ya Wilaya, Tarafa na Mkoa kwa ajili Askari wa Jeshi la Polisi.

Mheshimiwa Spika, kuhusu hivi vituo vya ulinzi shirikishi ambapo ni juhudi zinazotokana na utashi wa wananchi wenyewe, tumekuwa tukishauri watumie nguvu za wananchi na wadau kuliko kazi ya msingi ya Jeshi la Polisi haijakamilika tuhamishie rasilimali kidogo tulizonazo kwenye jambo ambalo kimsingi lingeweza kufanywa na wananchi.

Mheshimiwa Spika, kuhusu kufuatana naye, nipo tayari. Kwa kweli maeneo yake nimeshafika mara kadhaa, nadhani ratiba itakavyoruhusu tutakwenda kuangalia tushirikiane naye kuhamasisha wananchi ili waweze kukamilisha kituo hicho, ahsante.

Name

Dr. Charles Stephen Kimei

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vunjo

Primary Question

MHE. RASHID ABDALLA RASHID aliuliza: - Je, lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Ofisi ya Polisi Jamii Shehia ya Kendwa?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba nimwulize Mheshimiwa Waziri: Ni lini atawezesha wananchi wa Mwika Kaskazini kwa kumalizia kituo chao ambacho alikitembelea na akaahidi kwamba tukimaliza kupaua, basi tutapata uwezeshaji? (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, baada ya kauli ile kama unavyokumbuka tulikuwa wote Mheshimiwa Dkt. Kimei, tukasema IGP na imewekwa kwenye mpango wa ukamilishaji katika mwaka wa fedha unaoanza 2024/2025. Hiyo ni commitment, tutalitekeleza Mheshimiwa Mbunge. (Makofi)