Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 9 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 133 2023-11-09

Name

Rashid Abdalla Rashid

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiwani

Primary Question

MHE. RASHID ABDALLA RASHID aliuliza: -

Je, lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Ofisi ya Polisi Jamii Shehia ya Kendwa?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-

Mheshiniwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Rashid Abdalla Rashid, Mbunge wa Kiwani, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Ujenzi wa Ofisi ya Polisi Jamii inayojengwa Jindamiti katika Shehia ya Kendwa, inajengwa kwa nguvu na michango ya wananchi na wadau na ujenzi wake umefikia hatua ya lenta. Lengo la kujenga ofisi hiyo ni kutumiwa na vikundi vya ulinzi shirikishi vya Shehia ya Kendwa. Wajibu wa Serikali ni kujenga Ofisi na Vituo vya Polisi ambavyo hutumiwa na Askari Polisi katika kudhibiti uhalifu.

Mheshimiwa Spika, naomba kutumia fursa hii kumshauri Mheshimiwa Mbunge aendelee na jitihada za kuwahamasisha wananchi na wadau kukamilisha ujenzi wa ofisi hiyo ili iweze kutumiwa na vikundi vya ulinzi shirikishi kama walivyofanya wananchi wa Chambani, ahsante.