Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Godwin Emmanuel Kunambi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlimba

Primary Question

MHE. GODWIN E. KUNAMBI aliuliza:- Je, lini Mradi wa Umwagiliaji wa Udagaji katika Kata ya Ching’anda Mlimba utakamilika?

Supplementary Question 1

MHE. GODWIN E. KUNAMBI: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa fursa ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; Skimu ya Umwagiliaji ya Njage ilisanifiwa kutoa huduma kwenye hekta 1,750, mpaka sasa ni hekta 750 tu ambazo miundombinu ya umwagiliaji imefika.

Je, ni lini Serikali itakamilisha hizi hekta 1,000 zilizobaki?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; Skimu ya Idete ni skimu inayonufaisha Jeshi la Magereza tu na Idete, wananchi wa Kata ya Idete hawanufaiki; je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha wananchi pia wa Idete wawe sehemu ya kunufaika kwenye mradi huu? Ahsante.

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kumjibu Mheshimiwa Kunambi Mbunge wa Jimbo la Mlimba, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, moja, tunatambua kwamba Skimu ya Njage ambayo hekta ambazo zinatumika mpaka sasa hivi ni 750 na 1,000 bado hazijafanyika. Nimwondoe hofu kwamba nimezungumza na DG wa Tume ya Umwagiliaji kuhusu expansion ya mradi huu kumalizia hizi 1,000. Kwa hiyo, amesema tutaliweka katika mipango yetu ya kibajeti ili kuhakikisha tunalikamilisha kwa wakati ili wananchi wake waweze kupata faida ya kulima katika eneo kubwa zaidi.

Mheshimiwa Spika, kuhusu Skimu ya Idete ambayo inatumika na Magereza na yenyewe tumekubaliana kwamba tutakwenda kufanya usanifu wa kina kuongeza expansion ili wananchi wa Kata ya Idete waweze kufaidika. Magereza watumie na wananchi wa kawaida wa Kata ya Idete na wenyewe waweze kunufaika na skimu hiyo. Ahsante sana.

Name

Deo Kasenyenda Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makambako

Primary Question

MHE. GODWIN E. KUNAMBI aliuliza:- Je, lini Mradi wa Umwagiliaji wa Udagaji katika Kata ya Ching’anda Mlimba utakamilika?

Supplementary Question 2

MHE. DEO K. SANGA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kuniona, kwa sababu Serikali imefanya kazi nzuri ya kuhimiza umwagiliaji na kadhalika. Njombe tumepata miradi hiyo na wananchi wamefaidika, wamelima mahindi na wamepata mazao mengi sana. Serikali imenunua mahindi tunaishukuru. Je, Serikali ni lini itawatamkia wananchi wa Mkoa wa Njombe itakuwa tayari kuwalipa hela walizouza mahindi yao?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kumjibu Mheshimiwa Deo Kasenyenda Sanga, Mbunge wa Makambako, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kwamba Serikali ilinunua mahindi karibu tani 202,000 na thamani ya tani ambazo tulikuwa tumenunua ilikuwa ni karibu bilioni 187 na tumeshalipa na mpaka sasa hivi tudaiwa kama bilioni 56 ili kumaliza katika deni la awali. Tuko katika mchakato wa mwisho wa kuwalipa wakulima wote nchini wenye thamani ya hilo deni ambalo nalizungumzia la bilioni 56. Kwa hiyo nimwondoe shaka Mheshimiwa Mbunge na baada ya kumaliza malipo, Serikali kupitia NFRA tutaendelea kununua tena mahindi ili kutimiza lengo ambalo tumejiwekea kwa mwaka, ahsante sana.

Name

Aysharose Ndogholi Mattembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GODWIN E. KUNAMBI aliuliza:- Je, lini Mradi wa Umwagiliaji wa Udagaji katika Kata ya Ching’anda Mlimba utakamilika?

Supplementary Question 3

MHE. AYSHAROSE N. MATTEMBE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kuniona. Kwa kuwa wananchi wa Kata ya Muhamo na Msange katika Jimbo la Singida Kaskazini wamesubiri kwa muda mrefu mradi wa umwagiliaji. Je, ni lini Serikali itatangaza mradi huo? Ahsante sana.

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Ni kwamba Mradi wa Muhamo upo katika mpango wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji na nimwondoe tu shaka Mbunge kwamba, sasa hivi tuko katika mchakato na tukishakamilisha tu watapata matokeo, ahsante sana.

Name

Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. GODWIN E. KUNAMBI aliuliza:- Je, lini Mradi wa Umwagiliaji wa Udagaji katika Kata ya Ching’anda Mlimba utakamilika?

Supplementary Question 4

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipatia nafasi hii, niulize swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa Mradi wa Umwagiliaji wa Luamfi ni mradi muhimu sana kwa wakulima wa Ziwa Tanganyika. Je, ni lini mradi huu utakamilika kwa kuwa umekuwa unasuasua sana?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Nimwondoe tu shaka Mheshimiwa Mbunge Aida Khenani kwamba, maeneo yote yanayofaa kwa umwagiliaji ikiwemo mradi ambao ameutaja wa Luamfi ni kwamba yote tumeweka katika mipango yetu, ambayo Tume ya Taifa ya Umwagiliaji inaitekeleza. Nimhakikishie pia kwamba, bahati nzuri Mheshimiwa Rais anatuunga mkono sana na ameweka jitihada kubwa pamoja na fedha kuhakikisha maeneo yote yanayofaa yanafikiwa. Kwa hiyo hata hilo lenyewe tutalikamilisha kwa wakati, ahsante sana.