Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 9 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 129 2023-11-09

Name

Godwin Emmanuel Kunambi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlimba

Primary Question

MHE. GODWIN E. KUNAMBI aliuliza:-

Je, lini Mradi wa Umwagiliaji wa Udagaji katika Kata ya Ching’anda Mlimba utakamilika?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu:-

Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwa niaba ya Waziri wa Kilimo, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Godwin Emmanuel Kunambi, Mbunge wa Jimbo la Mlimba, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Skimu ya Umwagiliaji ya Udagaji/Mgugwe yenye ukubwa wa hekta 1,280 ni miongoni mwa skimu tatu za Bonde la Mto Kilombero ambazo zilifanyiwa upembuzi yakinifu na Serikali kupitia Tume ya Taifa ya Umwagiliaji kwa ufadhili wa Shirika la Maendeleo la Marekani (USAID) mwaka 2016. Skimu zingine zilizofanyiwa upembuzi yakinifu kupitia ufadhili huu ni Mpanga, Ngalamila yenye ukubwa wa hekta 28,141 na Kisegese yenye ukubwa wa hekta 16,130 zilizopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Mlimba katika Bonde la Mto Kilombero.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2023/2024, Serikali kupitia Tume ya Taifa ya Umwagiliaji imetenga bajeti kwa ajili ya kufanya mapitio ya upembuzi yakinifu na kufanya usanifu wa kina wa skimu hizo. Aidha, Tume ya Taifa ya Umwagiliaji ipo katika hatua za manunuzi na kumpata Mshauri Elekezi wa kutekeleza kazi husika. Hivyo, ujenzi wa Skimu ya Udagaji Mlimba unatarajiwa kuanza kutekelezwa katika mwaka wa fedha 2024/2025 baada ya kukamilika kwa kazi ya usanifu wa kina ili kubaini gharama halisi za ujenzi wa miundombinu ya umwagiliaji.