Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Catherine Valentine Magige

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CATHERINE V. MAGIGE aliuliza: - Je, lini Serikali itamaliza changamoto ya upungufu wa Watumishi wa Kada ya Afya katika Vituo ya Afya Karatu Mjini na Kaloleni – Arusha?

Supplementary Question 1

MHE. CATHERINE V. MAGIGE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Naomba sasa kupata nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Kwa kuwa Hospitali hii ya Kaloleni inahudumia wananchi wengi wa Jiji la Arusha lakini Kituo hiki cha Afya kina watumishi saba ambao wamefanya kazi kwa muda mrefu sana kwa mkataba.

Je, Serikali haioni sasa ni wakati muafaka wa kuwapa watumishi hawa ajira ya kudumu?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, kwa kuwa mtaani kuna wahitimu wengi wa kada hii wamekuwa wakisubiri ajira Serikalini na binafsi, je, Serikali haioni umuhimu wa kuwatumia wahitimu hawa wa hii Kada ya Afya wafanye kazi kwa kujitolea kwa sababu tuna upungufu mwingi katika sekta hii baadaye waje wapewe ajira rasmi?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Catherine Magige, kama ifuatavyo:-

Kwanza nampongeza Mheshimiwa Mbunge kwa namna ambavyo amekuwa akifuatilia huduma za afya kwa wananchi wa Mkoa wa Arusha. Namuhakikishia tu kwamba tunatambua kwamba Kituo cha Afya cha Kaloleni kinahudumia wananchi wengi lakini pia kina watumishi wanaojitolea ambao wapo pale kwa mkataba na Jiji la Arusha.

Mheshimiwa Spika, namhakikishia tu kwamba Serikali imeweka utaratibu mzuri wa kutoa kipaumbele cha ajira kwa watumishi ambao wanajitolea. Tutahakikisha pia watumishi hawa kama vigezo vyao kwa maana ya umri tangu wamehitimu vyuo uko ndani ya kipindi ambacho tunaajiri, basi tutahakikisha kwamba tunawapa kipaumbele ili waweze kupata ajira za kudumu.
Mheshimiwa Spika, pili, tayari Serikali ishatoa Mwongozo wa wahitimu wote wa kada mbalimbali za afya kuomba kujitolea kwenye vituo vyetu vya huduma za afya na Wakurugenzi ambao wana mapato wanaoweza kuwalipa, wawaajiri kwa mikataba waendelee kutoa huduma wakati wanasubiri ajira za kudumu. Jambo hili, namuhakikishia Mheshimiwa Mbunge, Serikali itaendelea kulisimamia kuhakikisha kwamba wataalamu hao wanajitolea katika maeneo hayo, ahsante. (Makofi)

Name

Njalu Daudi Silanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Itilima

Primary Question

MHE. CATHERINE V. MAGIGE aliuliza: - Je, lini Serikali itamaliza changamoto ya upungufu wa Watumishi wa Kada ya Afya katika Vituo ya Afya Karatu Mjini na Kaloleni – Arusha?

Supplementary Question 2

MHE. NJALU D. SILANGA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Tatizo lililoko Karatu linafanana kabisa na tatizo lililoko Wilaya ya Itilima. Zaidi ya zahanati 10 tumepata vibali lakini hatuna watumishi kada ya afya, nini kauli ya Serikali?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Njalu, Mbunge wa Jimbo la Itilima kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba Halmashauri ya Wilaya ya Itilima ni moja ya halmashauri nchini zenye upungufu mkubwa zaidi wa watumishi ukilinganisha na halmashauri nyingine.

Mheshimiwa Spika, ndiyo maana Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika ajira za watumishi wa sekta ya afya ametoa kipaumbele katika Halmashauri na Mikoa yenye upungufu mkubwa zaidi wa watumishi ikiwemo Mkoa wa Simiyu na ikiwemo Halmashauri ya Itilima.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge, kama ambavyo ajira zilizopita wamepata kipaumbele cha watumishi wengi, mara fursa za ajira zitakapojitokeza tutahakikisha tunapeleka watumishi wengi zaidi Itilima ili wapate kutoa huduma bora za afya kwa wananchi, ahsante.

Name

Munde Abdallah Tambwe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CATHERINE V. MAGIGE aliuliza: - Je, lini Serikali itamaliza changamoto ya upungufu wa Watumishi wa Kada ya Afya katika Vituo ya Afya Karatu Mjini na Kaloleni – Arusha?

Supplementary Question 3

MHE. MUNDE T. ABDALLAH: Mheshimiwa Spika, ahsante, niungane na wenzangu tatizo lililopo kwenye mikoa yao, hususani katika Mkoa wetu wa Tabora hasa kwenye zahanati za pembezoni kwenye wilaya pamoja na kwenye manispaa, watumishi wa afya ni wachache sana.

Mheshimia Spika, ni lini Serikali itatuletea watumishi wa afya wa kutosha kwenye zahanati na vituo vyetu vya afya katika Mkoa mzima wa Tabora?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, kwa hakika Waheshimiwa Wabunge lakini na Wananchi wa Tanzania kwa ujumla ni mashahidi kwamba Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kipindi cha miaka hii mitatu, ameajri watumishi wengi sana wa Kada za Afya na kuwapeleka kwenye vituo vyetu vya huduma za afya.

Mheshiwa Spika, zoezi hili ni endelevu, kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Munde kwamba, mara ajira za Kada mbalimbali za afya zitakapojitokeza, tutahakikisha pia tunatoa kipaumbele katika Mkoa wa Tabora lakini hasa katika vituo ambavyo viko pembezoni na vina upungufu mkubwa wa watumishi.

Name

Emmanuel Adamson Mwakasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Primary Question

MHE. CATHERINE V. MAGIGE aliuliza: - Je, lini Serikali itamaliza changamoto ya upungufu wa Watumishi wa Kada ya Afya katika Vituo ya Afya Karatu Mjini na Kaloleni – Arusha?

Supplementary Question 4

MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Kituo kipya cha Afya ambacho kipo katika Kata ya Misha katika Manispaa ya Tabora Mjini kina upungufu mkubwa wa watumishi lakini pamoja na vifaa. Sijui Serikali inajipangaje kukisaidia kituo kile?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mwakasaka, Mbunge wa Jimbo la Tabora Mjini, kama ifuatavyo. Katika kipindi cha mwaka huu wa fedha 2023/2024, tayari Manispaa ya Tabora imeshapokea zaidi ya shilingi 750,000,000 kwa ajili ya ununuzi wa vifaatiba katika vituo vya huduma za afya.

Mheshimiwa Spika, nimuhakikishie kwamba, katika eneo la vifaatiba, Serikali inaendelea kutenga fedha kwa ajili ya kuhakikisha vituo vyetu vilivyokamilika lakini na vituo vya zamani vinapata vifaatiba vya kutosha kwa ajili ya kuwahudumia wananchi.

Mheshimiwa Spika, pili, ni kweli kituo ambacho amekitaja kina upungufu wa watumishi lakini kama ilivyo utaratibu wa Serikali, tunaendelea kupeleka watumishi kwa awamu, na tutahakikisha pia kituo kile kinapata watumishi ili waweze kutoa huduma bora zaidi kwa wananchi, ahsante.