Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 9 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 128 2023-11-09

Name

Catherine Valentine Magige

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CATHERINE V. MAGIGE aliuliza: -

Je, lini Serikali itamaliza changamoto ya upungufu wa Watumishi wa Kada ya Afya katika Vituo ya Afya Karatu Mjini na Kaloleni – Arusha?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Catherine Valentine Magige, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2021/2022 na 2022/2023 Serikali imeajiri na kuwapangia vituo watumishi 83 wa kada mbalimbali za afya katika Halmashauri ya Wilaya ya Karatu, na watumishi 79 katika Halmashauri ya Jiji la Arusha. Aidha, watumishi 14 walipangwa katika kituo cha afya Karatu Mjini na watumishi 18 katika kituo cha afya Kaloleni Halmashauri ya Jiji la Arusha.

Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kuajiri wataalam wa kada mbalimbali za Afya na kuwapanga katika vituo vyenye upungufu mkubwa kote nchini, zikiwemo halmashauri za Karatu na Jiji la Arusha.